26 March 2013

WAMA yapongezwa kwa kusaidia wanawake


Na Anna Nkinda, Maelezo

MKE wa Rais wa China Mama Peng Liyuan, amezipongeza kazi zinazofanywa na Mke wa Rais Tanzania, Mama Salma Kikwete kupitia taasisi anayoiongoza ya Wanawake na Maendeleo (WAMA).

Mbunge kuweka umeme shule za Chalinze


Na Omary Mngindo, Chalinze

MBUNGE wa Chalinze, Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani, Bw. Said Bwanamdogo, anataraji kugawa vifaa vinavyozalisha umeme unaotumia mionzi ya jua (sola), katika shule mbalimbali za msingi na sekondari zilizopo jimboni kwake.

Viongozi wa dini waombea mradi wa maji


Na Steven William, Muheza

VIONGOZI wa dini ya Kikristo na Kiislamu, katika Kijiji cha Lusanga, Wilaya Muheza, mkoani Tanga, wameshiriki katika
ibada ya kuombea mradi wa kisima kirefu cha maji ili ujenzi
wake uweze kukamilika haraka na kuwasaidia wananchi.

Uwamsho wasomewa mashtaka upya



Na Mwajuma Juma, Zanzibar

KESI ya jinai inayowakabili viongozi wa Jumuiya ya Uwamsho, jana imeanza kusomwa upya katika Mahakama Kuu ya Zanzibar,
mbele ya Jaji Fatma Hamid Mohmoud.

Tuilinde amani yetu kuvutia wawekezaji kutoka China


RAIS wa China Xi Jinping, jan alimaliza ziara yake ya siku mbili nchini na kusisitiza umuhimu wa nchi hizo, kuendeleza uhusiano uliodumu muda mrefu.

20 March 2013

Bunduki yatumika kuombea rushwa *Wananchi walalamika kubambikiwa kesi na polisi *Viongozi CCM wataka iundwe tume kuchunguza

Na Mwandishi Wetu, Tabora

BAADHI ya wananchi katika Wilaya ya Kaliua, mkoani Tabora, wamelalamikia kitendo cha baadhi ya askari wa vituo vya polisi Usinge na Kaliua, kuomba rushwa kwa mtutu wa bunduki.

Papa asimikwa,atoa ujumbe mzito

ROME, Italia

KIONGOZI Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis I, jana amesimikwa rasmi kutumikia wadhifa huo na kutumia fursa hiyo kuwataka viongozi mbalimbali, kuwalinda wanyonge na masikini.

Kikwete aomboleza kifo cha trafiki

Na Jesca Kileo

RAIS Jakaya Kikwete, amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Said Mwema, kuomboleza kifo cha askari WP 2494 Koplo Elikiza ambaye amepoteza maisha kwa kugongwa na gari juzi mchana katika eneo la Bamaga, Dar es Salaam.

Hukumu wafuasi a ponda

Na Rehema Mohamed

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, kesho inatarajia kutoa hukumu ya washtakiwa wa kesi ya kufanya maandamano haramu kwenda kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), inayowakabili wafuasi 53 wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Shekhe Ponda Issa Ponda.

Kituo kikubwa cha kuzalisha gesi kujengwa nchini


OSLO, Norway

KAMPUNI za Statoil na BG Group, zinatarajia kutumia dola za Marekani bilioni 10 kujenga kituo cha kuzalisha na kusafisha
gesi ya asili nchini Tanzania ili kuiuza Asia.

KATUNI


19 March 2013

Lwakatare apanda kortini kwa ugaidi *Akabiliwa na mashtaka manne, anyimwa dhamana *Mawakili wake wakwama, Machi 20 kurudi tena



Na Grace Ndossa

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, jana limewafikisha kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Wilfred Lwakatare pamoja
na Bw. Ludovick Joseph.

JK: Nataka hospitali ya wazazi Dar



Rachel Balama na Rehema Mohamed

RAIS Jakaya Kikwete, ameziagiza Halmashauri za Jiji la Dar es Salaam kujenga hospitali ya wazazi ya Mkoa ili kupunguza mrundikano wa wagonjwa katika baadhi ya hospitali.

NCCR-Mageuzi wamsamehe Kafulila


Na Mwajabu Kigaza, Kigoma

MBUGE wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi, Bw. David Kafulila, amekiri kufanya kosa la utovu wa nidhamu ndani ya chama hicho na kusababisha uongozi kutaka kumvua uanachama.

IGP Mwema: Leteni taarifa za uhalifu tuzifanyie kazi


Na Anneth Kagenda

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, amewataka wananchi na waandishi wa habari, kutozungumzia na kuandika matukio ya uhalifu ambayo upelelezi wake haujakamilika badala yake kama wana taarifa zozote, waziripoti Kituo cha Polisi ili
ziweze kufanyiwe kazi.

Papa mpya kusimikwa rasmi leo



ROME, Italia

VIONGOZI mbalimbali duniani wanatarajiwa kushiriki misa ya kusimikwa kwa Papa mpya wa kanisa hilo duniani Francis I ambayo itafanyika leo Vatican.

Trafiki agongwa, afa akiwa kazini Dar


Na Waandishi Wetu

ASKARI wa Kitengo cha Usalama Barabarani, WP 2492 Elikiza Nko, amefariki dunia baada ya kugongwa na gari yenye namba 
T 328 BML, aina ya Land Rover Discover, mali ya Kanisa la
TAG wakati akiongoza msafara wa Rais Jakaya Kikwete.

Marekani kupambana na rushwa nchini



Na Godfrey Ismaely

BALOZI wa Marekani nchini, Bw. Alfonso Lenhardt, amesema kuanzia sasa Serikali yake itashiriki kikamilifu kupambana na rushwa nchini hasa kwa viongozi.

Moat yaitaka Serikali kutumia analojia, digitali


Na Goodluck Hongo

WAMILIKI wa Vyombo vya Habari Nchini (Moat) wameitaka Serikali kutumia mifumo yote miwili ya analojia na digitali kwa wakati mmoja hadi kufikia mwaka 2015 ambapo itakuwa mwisho wa kutumia analojia.

DAWASA ina mpango wa kuongeza mitambo


Na Darlin Said

MAMLAKA ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA) ina mpango wa kuongeza mitambo mikubwa ya maji taka mipya mitatu ya kusafisha mfumo wa maji kwa ajili ya kutatua tatizo la maji jijini Dar es Salaam.

Utumishi yaonya matangazo feki ya ajira



Na Peter Mwenda

SEKRETARIETI ya Ajira imeonya kuwa wao pekee ndiyo wenye jukumu la kutoa matangazo mbalimbali yanayohusiana na mchakato wa ajira katika Utumishi wa Umma.

Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano Ofisi ya Rais,Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa vyombo vya habari jana Dar es Salaam ilisema kuwa matangazo yanayochapishwa au kuandikwa katika mitandao ya kijamii hazijatolewa na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

Madawa ya kulevya bado yanaingizwa nchini- Nzoa


Na Veronica Ikonga

JESHI la Polisi nchini limewataka wananchi kutoa ushirikiano pale wanapoona ama kuwahisi watu wanaojihusisha na uingizaji dawa ya kulevya nchini watoe taarifa sehemu husika.

Chadema :Hatutoki tena Bungeni


Na Suleiman Abeid, Shinyanga
 
WABUNGE wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wametangaza kubadili utaratibu wao wa kutoka nje ya vikao vya Bunge kutokana na kutoridhishwa na baadhi ya mambo na badala yake sasa watakuwa wakikomaa ndani mpaka kieleweke.

Kamati yawarejesha walioacha tiba ya VVU



Na Pendo Mtibuche,Dodoma

KAMATI ya afya katika Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na programu ya Tunajali imeanzisha mkakati wa kuwarejesha kwenye tiba watu 5,358  wanaoishi na VVU (WAVIU) ambao walipotea na kuacha huduma hizo mkoani hapa.

Polisi yawashikilia tisa kwa ujambazi


Na Masau Bwire, Bagamoyo

JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani linawashikilia watu tisa wanaodaiwa kuwa majambazi baada ya kupora sh.milioni 7.5 na kuwajeruhi familia kwa kuwakataka kata mapanga.

CCM wagawanyika makundi Shinyanga


Na Suleiman Abeid,Shinyanga

SAKATA la kuachishwa uongozi kwa Katibu wa Siasa na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini, Charles Shigino limepokelewa kwa mawazo tofauti na wanachama wa CCM mjini hapa huku wengi wakipinga maamuzi hayo na wengine wakiunga
mkono.

Sote tuwajibike kukomesha tatizo la mimba shuleni


TATIZO la mimba kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini, linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya elimu.

Takwimu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinathibitisha kuwa tatizo hili limekuwa likiongezeka siku hadi siku hasa baada ya kuanzishwa shule za kata.

18 March 2013

Majambazi yapora gari, milioni 200/-*Wachina wanne wajeruhiwa,msako mkali waanza *TANROADS YADAI FEDHA ZILIZOPORWA NI MIL.7.9

Na Eliasa Ally, Iringa

MAJAMBAZI 10 wakiwa na bunduki tatu pamoja na mapanga, wamevamia kambi ya Mkandarasi wa Kampuni ya SIETCO kutoka nchini China, iliyopo eneo la Igingilanyi, mkoani Iringa na kupora fedha taslimu sh. milioni 100, dola za Marekani 11,560, euro 54,910 na kuwajeruhi wachina wanne kwa mapanga.

Ridhiwani amshukia Mbunge wa Korogwe

Na Yusuph Mussa, Korogwe

MJUMBE wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani, Bw. Ridhiwan Kikwete, amesema Mbunge Korogwe Mjini, Bw. Yusuph
Nassir, anahatarisha jimbo hilo kwenda upinzani.

Waislamu Morogoro wampinga Mufti Simba

Na Aziz Msuya, Morogoro

SAKALA la Shekhe Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Bin Shaaban Simba, kumvua uongozi Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Yahaya Samwali, sasa limeanza kuchukua sura mpya.

MAKAZI


Mkazi wa Bonde la Jangwani, Dar es Salaam, ambaye hakufamika jina lake akiwa amelala nje ya nyumba yake kama alivyokutwa jana.  Pamoja na Serikali kutoa amri ya kuwataka waondoke eneo hilo ambalo ni hatarishi kwa maisha yao na mali zao, bado wameendelea kukaidi. Picha na Peter Twite)

Lowassa akusanya mil.85/-za ajira kwa vijana


Richard Konga, Arusha

WAZIRI Mkuu mstaafu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, mkoani Arusha, Bw. Edward Lowassa, amekusanya sh. milioni
85 katika harambee ya uzinduzi wa Mfuko wa Maendeleo ya Waendesha Pikipiki mkoani Arusha (UWAPA), maarufu
kama 'bodaboda'.

IGP Mwema kufungua mkutano wa makachero



Na Frank Geofray, Jeshi la Polisi

WAKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI’s) kutoka Umoja wa Wakuu wa Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCCO), leo wanatarajia kuanza mkutano wa siku mbili jijini Dar es Salaam, chini ya Uenyekiti wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa
ya Jinai nchini.

Katibu Uenezi CCM Shy avuliwa uongozi


Na Suleiman Abeid, Shinyanga

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Shinyanga Mjini,  kimemuondoa katika nafasi ya uongozi Katibu wake wa Itikadi, Siasa na Uenezi, Bw. Charles Shigino ikiwa ni miezi michache tangu achaguliwe katika wadhifa huo.

Mbunge afichua siri kutojiunga na JKT


Na Benedict Kaguo

MBUNGE wa Kisesa, mkoani Simiyu, Bw. Luhaga Mpina, ametoboa siri ya kukataa kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kutokana na wananchi wa jimbo hilo kukubwa na baa la njaa hali iliyowalazimu wengine kuzikimbia familia zao.

Waibuka 'kidedea' Shinda Biashara na Majira


Na Anneth Kagenda

WAJASIRIAMALI watatu akiwamo mwanafunzi wa Chuo cha St. Yohana kilichopo mjini Dodoma, Bw. Andrew Manjira, wameibuka washindi wa shindano la “Shinda Biashara na Majira”.

Mkuchika ataka gesi ichochee maendeleo

Na Casmir Ndambalilo, Newala

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Kapteni mstaafu George Mkuchika, ameiomba Serikali kupitia Shirika la Umeme nchini (TANESCO), kuongeza muda na kasi ya kusambaza umeme unaotokana na gesi iliyogundulika mkoani Mtwara ili kuchochea
maendeleo ya wananchi.

Raila Odinga afungua kesi kumpinga Kenyatta


Na Isaac Mwangi, EANA

ALIYEKUWA mgombea urais nchini Kenya kutoka Muungano
wa CORD, Bw. Raila Odinga, amefungua kesi katika Mahakama
ya Juu nchini humo kupinga ushindi wa Bw. Uhuru Kenyatta, ambaye alishinda kiti hicho kwenye Uchaguzi Mkuu uliofanyika
Machi 4 mwaka huu.

Wajawazito Amana wapatiwa vifaa vya kujifungulia



Na Heri Shaaban

MADIWANI Wanawake wa Maniaspaa ya Ilala wametoa vifaa vya kujifungulia wanawake wajawazito katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa iliyopo Amana.

UZINDUZI


Mkuu wa Wilaya ya Misenyi, mkoani Kagera, Kanali mstaafu Issa Njiku, akikata utepe ili kuzindua vyumba viwili vya madarasa kwenye Shule ya Msingi Kyaka, vilivyojengwa kwa msaada wa Taasisi ya Vodacom Foundation wilayani humo. Taasisi hiyo pia imetoa madawati tisini ikiwa ni jitihada za Kampuni ya
Vodacom Tanzania kuchangia maendeleo ya elimu nchini.
(Na Mpigapicha Wetu).

Rais Kikwete awashukia wanaokejeli Serikali


Na David John

RAIS Jakaya Kikwete, amewataka baadhi ya wananchi kuacha tabia ya kukejeli jitihada zinazofanywa na Serikali na hasa za kuwasogezea huduma za kijamii wananchi wake ,badala yake waunge mkono jitihada hizo.

'Serikali angalieni upya maslahi ya walimu'


Na Mercy James,
Mufindi

SERIKALI imetakiwa kuangalia upya maslahi ya walimu ili kuboresha taaluma katika shule za msingi na sekondari kwa lengo la kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Ajeruhiwa vibaya na mamba wakati akichota maji mtoni


Na Joseph Mwambije,Namtumbo

MKAZI mmoja wa kijiji cha Likuyu wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Bw.Rashid Almasi(59)amejeruhiwa vibaya na mamba baada ya kupambana na mamba huyo na hatimaye kumshinda nguvu.

Vijana watakiwa kuacha propaganda,wachape kazi


Na Florah Temba,
Moshi.

UMOJA wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) mkoani Kilimanjaro,umewataka vijana wa chama hicho kufanya kazi na kuacha propaganda, hatua ambayo itakiwezesha chama cha CCM kushinda katika uchaguzi wa serikali za mitaa, unaotarajiwa kufanyika mwakani 2014, na kuyakomboa majimbo yaliyochukuliwa na upinzani katika uchaguzi wa mwaka 2015.

Mkuchika azungumzia vurugu za wanasiasa Masasi



Na Casmir Ndambalilo, Masasi

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Kapteni mstaafu George Mkuchika, amekemea vurugu zinazoanzishwa na baadhi ya wanasiasa na wanaharakati nchini ili kujipatia umaarufu kwa kuwapotosha wananchi juu ya uendeshwaji wa Serikali iliyoko madarakani inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Watoto wachomwa midomo wakidaiwa kula karanga



Na Lilian Justice, Morogoro

JESHI la Polisi mkoani Morogoro, linamsaka mkazi wa Ujenzi, katika Kata ya Ndege, Bw. Jaribu Bakari, kwa kosa la kuwachoma moto mdomoni wanawe wawili kwa banio lenye mkaa.

Mhariri Majira kuwania tuzo uandishi mahiri


Na David John

MHARIRI Mtendaji wa Gazeti la Majira Imma Mbuguni ameteuliwa kuwania Tuzo za Uandishi mahiri wa habari,ambapo sherehe zake zitafanyika Aprili 5, mwaka huu Dar es salaam

Askofu awakemea wanaochoma makanisa


Na Ramadhan Libenanga, Morogoro

ASKOFU wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Morogoro, Telesphor Mkude, amewataka baadhi ya watu wanaodaiwa kuwa waumini  wa Kiislamu nchini, kuacha kuchoma makanisa kwani kufanya hivyo watavuruga amani na utulivu uliopo.

Wajumbe Mara waipongeza TRA

Na Veronica Modest

Musoma.



MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imepongezwa na wajumbe wa
Halmashauri kuu  ya CCM mkoa wa Mara kwa
kufanikisha kutekeleza ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010 kwa kipindi cha julai
2011 hadi June 2012.

Wanawake washauriwa kudai haki kwa utaratibu

Na Raphael Okello,Bunda.
WANAWAKE wametakiwa kutosababisha  vurugu ndani ya ndoa zao kwa
kigezo cha kudai haki sawa badala yake wameshauriwa kufuata taratibu katika
kudai haki hizo.

Wakazi wa Majengo walalamika nyumba zao kujaa maji

Na  Patrick Mabula,
Kahama,


Wananchi wanaoishi eneo la mitaa  ya majengo  mjini Kahama wamelalamikia kero ya
mafuriko yanayotokana na mvua zinaponyesha  na kufanya mitaro kumwaga maji ambayo
huingia na kujaa ndani ya nyumba zao na kuwafanya wazikimbie na kulala nje huku
wengine wakilala kwa majirani.

TAKUKURU kushirikiana na asasi za dini

Na Rehema Maigala

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)wameungana na asasi za dini katika kuzuia na kupambana na rushwa Tanzania.

15 March 2013

Lwakatare ibua mapya Chadema *Dkt. Slaa adai mpango wa kumkamata waliujua *Asema propaganda zinatumika ili kuwachafua


Na Anneth Kagenda

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kukamatwa kwa Mkurugenzi wake wa Ulinzi na Usalama, Bw. Wilfred Lwakatare ni mkakati wa Jeshi la Polisi nchini.

Papa Mpya: Nimeanza kazi rasmi



ROAMA, Italia

PAPA mpya wa Kanisa Katoliki duniani, Francis I, ambaye ni wa kwanza kuchaguliwa kutoka Amerika ya Kusini, ameanza kazi
rasmi akitangaza kulileta kanisa hilo pamoja.

Membe: Sihusiki kumtesa Kibanda *Afananisha jambo hilo na kuchafuliwa kisiasa


Na Rachel  Balama

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe, amesema hausiki na hana sababu ya kuhusika
na vitendo vya ukatili na unyama aliofanyiwa Mwenyekiti wa
Jukwaa la Wahariri (TEF), ambaye pia ni Mhariri Mtendaji
Mkuu wa Kampuni ya New habari, Bw. Absalom Kibanda.

Moravian laguswa na shambulizi la Kibanda


Na Mwandishi Wetu

UONGOZI wa Kanisa la Moravian Tanzania (KMT), Jimbo la Kusini, umelaani vikali tukio la kuvamiwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Bw. Absalom Kibanda na kudai vyombo vya Ulinzi na Usalama, vinapaswa kuwafuatilia na kuwakamata watuhumiwa hao.

Polisi aliyeua Mwalimu afukuzwa


Na Mercy James, Njombe

JESHI la Polisi mkoani Njombe, limemfukuza kazi askari wake PC Gelvas Joseph, mwenye namba 9790, kwa kosa la kufanya mauaji
ya mwalimu wa Shule ya Sekondari Kitulo, wilayani Makete.

Pinda ashauri njia za kuepuka tatizo la figo


Na Mwandishi Wetu, Arusha

WAZIRI Mkuu Bw. Mizengo Pinda, amewahimiza Watanzania kuwa na tabia ya kunywa maji mengi kila siku ili kujikinga na matatizo ya figo yanayozini kuongezeka kila siku.

Mtoto auawa, kunyofolewa macho


Na Elizabeth Joseph, Dodoma

MTOTO Happyness Paulo (3), mkazi wa Kijiji cha Handali,
Wilaya ya Chamwino, mkoani Dodoma, ameuwawa na watu wasiofahamika na kumchuna ngozi.

Mbwa mwenye kichaa awauma watu watano



Na Israel Mwaisaka, Chunya

WATU watano wakiwemo wanafunzi wawili, wakazi wa Wilaya
ya Chunya, mkoani Mbeya, wameng’atwa na mbwa mwenye kichaa na kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya kwa matibabu.

Muhubiri mbaroni kwa uchochezi



Na Suleiman Abeid, Shinyanga

MUHUBIRI wa dini ya Kikristo, mkazi wa Kigogo, Dar es Salaam, Damian Ndhimbo (35), juzi alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Maswa, mkoani Simiyu, akituhumiwa kusambaza nyaraka mbalimbali zinazodaiwa kuwa za uchochezi.

13 March 2013

Mauaji ya waandishi yawagusa wadau

Na Rehema Maigala

WADAU wa habari nchini, wamekubaliana kuunda kamati ya watu 16 ambayo itakutana na wakuu wa vyombo vya  usalama nchini ili kuzungumzia undani wa suala la usalama wa waandishi wa habari nchini.

TAMKO MOAT


Mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya Ufuatiliaji wa kuzorota kwa mazingira ya usalama wa wahariri na waandishi wa habari, ambaye pia ni Meneja Mkuu wa Kampuni ya Business Times Limited, Bw. Aga Mbuguni (kushoto), akisoma moja ya matamko ya Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dar es Salaam jana, kuhusu matukio ya utekaji na utesaji kwa waandishi na wahariri yanayoendelea kutokea nchini na hatua zitakazochukuliwa kudhibiti vitendo hivyo. Wengine ni baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo. (Picha na Charles Lucas)

Wabunge Chadema kuhojiwa kwa pingu *Polisi wapewa kazi hiyo kuhakikisha wanahojiwa *Ndugai asema kamati wasiyoitambua ipo kisheria *Dkt. Slaa, Lissu wajibu mapigo, wamtega Makinda



Grace Ndossa na Gladness Theonest

OFISI ya Bunge imesema, wabunge ambao watagoma kwenda kuhojiwa katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Jeshi la Polisi litawapeleka kwa pingu katika kamati hiyo.

BAJETI MANISPAA


Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Mstahiki Yusuph Mwenda (katikati), akisoma tamko la kuidhinisha bajeti ya manispaa hiyo ya mwaka 2013-2014, mara baada ya kuungwa mkono kwa kauri moja na Baraza la Madiwani Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Naibu Meya, Bw. Songoro Mnyonge na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Mhandisi Mussa Natty. Zaidi ya sh. Bilioni 156 zitatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya manispaa hiyo. (Picha na Charles Lucas)

MATOKEO IV Walimu waliopengezana kuchunguzwa *TCRA kusaka ujumbe waliotumiana katika simu zao



Na Rose Itono

SERIKALI itashirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), ili kuwabaini walimu waliopongezana kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka 2012.

JOHO

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharrif Hamad, akivikwa joho na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, Bw. Abdul Kambaya (kushoto), lililoandaliwa na wanawake wa chama hicho, wakati wa mkutano wa hadhara Dar es Salaam jana. (Picha na Peter Mwenda)

Abiria reli ya kati Dom wakwama




Na Elizabeth Joseph, Dodoma

MVUA zinazoendelea kunyesha na kusababisha mafuriko katika maeneo ya Godegode, Miganga na Gulwe, mkoani Dodoma, zimesababisha abiria zaidi ya 1,000 ambao wanatumia reli ya kati, kushindwa kuendelea na safari kutokana na njia za reli kuharibika.

Mwenyekiti CHADEMA asimamishwa uongozi



Na Wilhelm Mulinda, Mwanza

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kata ya Ilemela, mkoani Mwanza, kimemsimamisha uongozi aliyekuwa Mwenyekiti wa kata kwa tiketi ya chama hicho, Bw. Isack
Nyatega, kutokana na tuhuma mbalimbali.

Wawakilishi Z'bar wamuomba IGP Mwema kuboresha makazi ya askari




Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, jana amefanya mazungumzo na wajumbe tisa wa Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi kutoka Zanzibar chini ya Mwenyeketi wake Bw. Hamza Hassan Juma.

BANGI


Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), Mkaguzi Uforo (kulia), akiangalia shamba la bangi, wakati wa msako uliofanyika kwenye Kijiji cha Kwenkeyu Kata ya Kizara wilayani Korogwe mkoani Tanga hivi karibuni. (Picha na Mashaka Mhando)

Viroba 53 vya mirungi vyakamatwa Arusha



Na Pamela Mollel, Arusha

JESHI  la Polisi mkoani Arusha, limekamata shehena ya dawa za kulevya aina ya mirungi viroba 53, katika matukio mawili tofauti.

TCRA: Mionzi ya simu haina madhara


Na Darlin Said

MAMLAKA ya Mawasiliano nchini (TCRA), imekanusha taarifa zinazodai mionzi inayotumika katika vyombo vya mawasiliano ikiwemo simu za mkononi, ina madhara kwa afya ya binadamu.

TCRA


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Profesa John Nkoma, akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya warsha ya wahariri na waandishi Dar es Salaam jana, iliyohusu mionzi inayotumika katika vyombo vya mawasiliano zikiwamo simu za mikononi ambapo alikanusha kuwa mionzi hiyo haina athari kwa watumiaji. (Picha na Prona Mumwi)

12 March 2013

Washtakiwa kesi ya uchochezi, wizi wakana waelezo ya awali


Rehema Mohamed na Rehema Maigala

WASHTAKIWA wa kesi ya wizi na uchochezi inamkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Shekhe Issa Ponda na wenzake, jana waliendelea kujitetea baadhi yao wakikana maelezo ya awali waliyotoa katika Kituoa cha Polisi Mabatini, Kijitonyama.

DC Korogwe apinga taarifa ya Ofisa Elimu matokeo kidato IV


Na Yusuph Mussa, Korogwe

MKUU wa Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, Bw. Mrisho Gambo, ameungana na vyama vya upinzani kuikataa taarifa ya Kaimu Ofisa Elimu Sekondari wilayani humo Bw. Shabaan Shemzigwa, kuhusu chanzo cha kufeli kwa wanafunzi wa
kidato cha nne mwaka 2012 na kudai haina mashiko.

Mtikila ampongeza Dkt .Nchimbi

Na Kassim Mahege

SIKU moja baada ya Waziri wa Mambo ya ndani Dkt.Emmanuel Nchimbi kuwasimamisha kazi maofisa wa Jeshi la Polisi kwa tuhuma mbalimbali, Mwenyekiti wa Chama Cha Democratic Party(DP) Mchungaji Christopha Mtikila amempongeza kwa hatua hiyo na kumtaka asiishie hapo.

Mbatia amtaka Raila Odinga kuheshimu matokeo



Na David John

MWENYEKITI wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Bw. James
Mbatia, amemshauri aliyekuwa mgombea urais nchini Kenya
kwa tiketi ya Chama cha Muungano CORD, Bw. Raila Odinga kuheshimu matokeo ambayo ndio maamuzi ya wananchi.

Serikali iwasaidie wajasiliamali kwa kuwapa mafunzo




KUJIAJIRI ni suala linalopewa kipaumbele na mamlaka
mbalimbali nchini pamoja na mataifa yaliyoendelea.


Mabadiliko makubwa katika mifumo ya uchumi, yamechangia
wananchi wengi kukosa kazi za kuajiriwa ambapo ajira binafsi

11 March 2013

Vigogo 6 polisi wasimamishwa *Dkt. Nchimbi afichua tuhuma nzito dhidi yao *Wadaiwa kupokea rushwa, kubambikia kesi *Wengine wabadili vidhibiti dawa za kulevya


Na Rehema Maigala

WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imewasimamisha kazi maofisa sita wa Jeshi la Polisi nchini kwa tuhuma mbalimbali
za ukiukwaji wa maadili na taratibu za jeshi hilo.

Hali ya Kibanda sasa yaimarika *Taya, meno vyafungwa waya maalumu


Na Mwandishi Wetu

HALI ya Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Bw. Absalom Kibanda, inaendelea kuimarika baada ya kufanyiwa oparesheni ya kuondoa jicho la kushoto na kurekebisha taya.

UZINDUZI



Balozi Khamisi Kagasheki akikata utepe kwenye kasha la kuhifadhia fedha ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Kikundi cha Habari Group uliofanyika mwishoni mwa wiki Jijini Dar es Salaam, Kushoto ni mlezi wa Kikundi hicho Bi. Angela Kairuki ambaye ni Naibu Waziri wa Sheria na Katiba, wa pili kushoto ni Mbunge wa Busega Bw. Titus Kamani (Picha na Gladness Theonest).

'Waumini Anglikana tumuombee Dkt. Mokiwa'



Na Anneth Kagenda

WAUMINI wa Kanisa la Anglikana nchini, wameshauriwa kuzama katika maombi na kuiombea familia ya Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Dkt. Valentino Mokiwa, ambaye mwishoni mwa wiki alivamiwa nyumbani kwake Mbezi Luis, Dar es Salaam,
eneo la Mashirikiano na watu wasiofahamika.

Maalim Seif ambana JK ripoti za mauaji



Peter Mwenda na Anneth Kagenda

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, ameitaka Serikali ya Rais Jakaya Kikwete iweke hadharani matokeo ya uchunguzi wa matukio mbalimbali ya
mauaji na utekwaji nyara uliotokea hivi karibuni nchini.

CCM watoa tamko gesi ya Mtwara



Na Casmir Ndambalilo, Newala

HALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Newala, mkoani Mtwara, imeunga mkono tamko la Halmashauri Kuu ya Taifa ya kukubali ujenzi wa bomba la gesi kwenda Dar es Salaaam baada ya kubaini wakazi wa Mkoa huo watanufaika na mradi wa gesi uliopo mkoani humo.

TURUBAI


Mfanyabiashara ambaye hakufahamika jina akifunga kamba katika nguzo ya Umeme kwa ajili ya kuweka turubai, kuzuia biashara yake kunyeshewa na mvua kama alivyokutwa mtaa wa Kongo Dar es Salaam jana.(Picha na Prona Mumwi)

Wanafunzi kidato cha II wakimbia masomo


Na Masau Bwire, Rufiji

ZAIDI ya nusu ya wanafunzi waliofeli mtihani wa kidato cha pili mwaka 2012 na kutakiwa kurudia masomo mwaka huu katika Wilaya ya Rufiji, mkoani Pwani, hawajaripoti shuleni na hawajulikani waliko.

DC ambana Mbunge wa Korogwe kuelezea kazi za Mfuko wa Jimbo



Na Yusuph Mussa, Korogwe

MKUU wa Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, Bw. Mrisho
Gambo amemtaka mbunge wa Korogwe Mjini, Bw. Yusuph
Nassir, kuzunguka jimboni kwake ili kuwaeleza wananchi
kazi zinazofanywa na Mfuko wa Jimbo.

ABIRIA


Abiria wanaosafiri wa treni na kutoka Stesheni Kuu ya  Dar es Salaam kwenda Ubungo wakisukumana kugombea kuingia saa za ajioni ambako abiria huongezeka baada ya kutoka kazini kama inavyonekana mwishoni mwa wiki katika Kituo cha Kamata Dar es Salaam mwishoni mwa wiki (Picha na Peter Mwenda)

RC Moro awabana Ma DC, DED


Na Severin Blasio, Morogoro

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Bw. Joel Bendera, ameahidi kuwachukulia hatua za kinidhamu Wakuu wote wa Wilaya na Wakurugenzi mkoani humu ambao watashindwa kusimamia
usafi wa mazingira katika maeneo yao.

Rasimu ya Katiba Mpya kukamilika Mei-Warioba


Na Grace Ndossa

MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba, amesema rasimu ya Katiba Mpya inatarajiwa kukamilika ifikapo Mei mwaka huu.

KATUNI


Viongozi wa dini walaani wanaohatarisha amani



Na Christina Mokimirya

VIONGOZI wa Jumuiya na Taasisi mbalimbali za kislamu nchini zimeshauri Serikali kuweka utaratibu wa kutambua Jumuiya au Taasisi za kidini kwa nafasi sawa katika uwakilishi wa masuala ya kidini ndani ya serikali.

INAUZUNISHA*Mwalimu Mkuu ampa mimba mwanafunzi wake *Amefaulu kidato cha kwanza, akwama kuendelea *Mtuhumiwa yupo uraiani,Polisi watupiwa lawama


Na Gift Mongi

MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Kigwe, iliyopo Wilaya
ya Bahi, mkoani Dodoma, Bw. Martin Mbowe, anadaiwa kumpa mimba wanafunzi wake mwenye umri wa miaka 15 (jina tunalo),
hivyo kushindwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza
katika shule ya Serikali mwaka huu.

Mbuge CHADEMA kortini kwa uchochezi

Na Jovither Kaijage, Ukerewe

MBUNGE wa Jimbo la Ukerewe, mkoani Mwanza, Bw. Salvatory Machemli (CHADEMA), jana alipandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Wilaya hiyo akikabiliwa na shitaka la uchochezi.

DC Korogwe amseka ndani Ofisa Misitu

Na Yusuph Mussa, Korogwe

MKUU wa Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, Bw. Mrisho Gambo, jana alimuamuru Mkuu wa Polisi wilayani humo,
Madaraka Majiga, kumkamata na kumuweka ndani Ofisa
Misitu Wilaya, Bw. Damas Mumwi baada ya kubishana
naye katika Kikao cha Kamati ya Ushauri Wilaya (DCC).

SIKU YA FIGO


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Hussein Mwinyi,  akizungumza na waandishi wa habari,(hawapo pichani) Dar es Salaam jana, kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Afya ya Figo Duniani Machi 14, mwaka huu. Kulia ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema. (Picha na Prona Mumwi)

Kigogo scania kortini akidaiwa kuiba milioni 177/-


Na Judith Michael

OFISA Utawala wa Kampuni ya Scania (T) Limited tawi la Dar es Salaam, Didier Abdallah Mlawa(38) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa tuhuma za kughushi saini ya Mkurugenzi wa Kampuni hiyo na kujipatia kiasi cha sh. Milioni 177

Balozi Sefue aifagilia NHC

Na Mwandishi Wetu

KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Sefue Ombeni, amelipongeza Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) kwa kufanyakazi nzuri katika miradi yake ya nyumba nchi nzima na kwamba ikikamilika yote baada ya  miaka mitano itasaidia kuboresha maisha ya Watanzania.

Mbowe amaliza mgogoro Ktavi

Na Goodluck Hongo

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bw.Freeman Mbowe amemaliza mgogoro mkubwa uliokuwa ukifukuta na kutishia mpasuko ndani ya Chama hicho mkoani Katavi, hadi kusababisha Makamu Mwenyekiti wa chama hicho (Bara), Said Arfi kuripotiwa kutupa kadi yake ya uanachama kwenye kikao cha ndani na kutishia kujitoa,

MAKTABA YA BUSINESS TIME


Meneja Usambazaji wa Kampuni ya Business Times Ltd, Bi. Sophia Mshangama akimuonesha Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto), baadhi ya vitabu na magazeti katika maktaba ya kampuni hiyo. (Picha na Zourha Malisa)

Mchungaji mbaroni kwa kutorosha wanafunzi

 Na Heckton Chuwa,
Moshi

JESHI la Polisi mkoani Kilimanjaro,linamshikilia mtu mmoja anaedaiwa kuwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,(DRC), kwa tuhuma ya kuwatorosha wanafunzi wawili, (majina yanahifadhiwa), kwa lengo la kuwasafirisha nje ya
nchi.

Wasilisheni maombi wajumbe wa baraza-Warioba


Na Grace Ndossa

MWENYIKITI wa Tume ya mabadiliko ya Katiba Mpya Jaji Joseph Warioba amewataka wananchi wenye sifa za kuwa wajumbe wa mabaraza  ya katiba ya Wilaya na ambao wangependa kuwa wajumbe wa mabaraza hayo  kuwasilisha maombi yao kwa maofisa watendaji wa  vijiji au mitaa kuanzia kesho hadi  machi 20 mwaka huu.

WAFANYAKAZI WA BUSINESS TIME SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (wa pili kulia), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanykazi wa Kampuni ya Business Times Ltd, mara baada ya kutembelea kampuni hiyo. (Picha na Zourha Malisa)

Serikali yataka uangalizi maalum kwa watuhumiwa.



Na Rehema Mohamed

SERIKALI imewasilisha maombi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, kutaka watu wanne wanaotuhumiwa kukutwa na nyaraka za uchochezi, wawe chini ya uangalizi maalumu.

Manyanyaso ya wanawake duniani yakomeshwe



PAMOJA na umri mkubwa tangu kuanza kwa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, bado tunachoshuhudia katika jamii zetu ni manyanyaso mbalimbali wanayofanyiwa akina mama duniani.

UANDAAJI


Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Bi. Ummy Mwalimu (kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa  Mhariri wa Habari za Michezo wa gazeti hili, Bi. Elizabeth Mayemba, kuhusu uandaaji wa kurasa za michezo, wakati waziri huyo alipotembelea Kampuni ya Business Times Ltd, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Dar es Salaam jana. Katikati ni Meneja Usambazaji wa kampuni hiyo. Bi. Sophia Mshangama. (Picha na Anna Titus)

Sekondari yaanzisha jela ya mateso *Inaitwa “Guantanamo”, siri nzito yafichuka


Na Rashid Mkwinda, Mbeya

WALIMU wa Shule ya Sekondari Forest, iliyopo jijini Mbeya, wanadaiwa kutumia moja ya ofisi za walimu kama chumba cha
mateso kilichopewa jina la “Guantanamo”, ambacho hutumiaka
kutoa adhabu kwa wanafunzi wanaoshindwa kutoa hongo ya
sh. 500 hadi 1,000 wanapofanya makosa shuleni hapo.

4 mbaroni wakidaiwa kuchochea udini Dar



Rehema Maigala na Leah Daudi

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linawashikilia watu wanne kwa tuhuma za uchochozi wa kidini baada ya kunaswa katika msako mkali uliofanyika jiji hilo.

Mbatia akataa ujumbe tume ya Pinda



Na Darlin Said

MWENYEKITI wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Bw. James
Mbatia ambaye pia ni mbunge wa kuteuliwa, amesema hakubaliani na uteuzi uliofanywa na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, kuwa mmoja wa wajumbe katika tume ya kuchunguza sababu za kushuka kwa ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012.

CCM yabaini 'madudu' katika miradi yake



Na David John

KATIBU wa Uchumi na Fedha wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Zakia Meghji, amesema mikataba ya muda mrefu iliyosainiwa
na viongozi mbalimbali wa chama hicho katika vitega uchumi vyake, imechangi wakose mapato ya uhakika.

Lipumba ataka wakazi wa Mtwara wasikilizwe


Na Said  Hauni, Lindi

CHAMA cha Wananchi (CUF), kimeishauri Serikali kutopuuzia madai ya wakazi wa Mtwara kupinga usafirishaji wa gesi asilia
kwa njia ya bomba kutoka Kijiji cha Mnazi Bay, mkoani humo
na kuipeleka mikoa mingine ili kuzalisha umeme.

Polisi wakiri kuua raia kwa risasi


Na Damiano Mkumbo, Singida

MKAZI wa Bariadi, mkoani Simiyu, Methusala Shing'oma (36), amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na polisi ambao walikuwa wakipambana na majambazi walioyateka magari mawili moja likiwa na maiti mbili pamoja na lori la mbao kwenye Kijiji Milade, Wilaya
ya Mkalama, Barabara ya Singida-Nzega.

Wafariki papo hapo katika ajali



Na Steven William, Muheza

WATU wawili wamefaliki dunia papo hapo baada ya malori
mawili kugongana uso kwa uso na kuwaka moto katika Kijiji
cha Kilapula, kilichopo Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga.

05 March 2013

MSAADA

Wasamaria wakisaidia kulinasua gari la polisi lenye namba PT 1448,  Dar es Salaam jana, lililotumbukia katika mtaro uliofunikwa kwa maji ya mvua zilizoendelea kunyesha jijini, kamaabara ya Msimbazi eneo la KAMATA. Elimu ya Ulinzi Shirikishi Polisi Jamii imesaidia kuleta mahusiano mazuri kati ya jeshi hilo na wananchi. (Picha na Prona Mumwi)

Issa Ponda ana kesi ya kujibu *Mahakama yathibitisha mashtaka dhidi yao *Sasa kuanza kujitetea kuanzia Jumatano


Na Rehema Mohamed

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewaona Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Shekhe Issa Ponda na wenzake 49, wana kesi ya kujibu.

SHEKHE PONDA


Katibu Mkuu wa Taasisi ya Kisilamu Shekhe Issa Ponda akiwa chini ya ulinzi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  Dar es Salaam jana,wakati akirudishwa mahabusu baada mahakama hiyo kushindwa kutoa maamuzi hadi Jumatano wiki hii wakati washitakiwa watano wa kesi hiyo watakapojitetea upya.(Picha na Heri Shaaban)

Polisi wauawa Uchaguzi Mkuu Kenya


NAIROBI, Kenya

KATIKA hali isiyo ya kawaida, watu wasiopungua 17 wameuawa wakiwemo Maofisa sita wa polisi katika Mkoa wa Pwani, nchini Kenya siku moja kabla ya Uchaguzi Mkuu ulioanza jana.

Mapya zaidi yabuka kifo cha kigogo UVCCM



Na Pamela Mollel, Arusha

TUKIO la kufariki kwa aliyekuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, mkoani Arusha, Benson Mollel (26), limevuta hisia za wakazi
wa Mkoa huo baada ya vitu mbalimbali kupatikana katika
chumba alichokuwa amelala.

ZIARA


Naibu waziri wa Katiba na Sheria, Bi. Angella Kairuki (katikati), akikagua choo cha watumishi wa mahakama ya Ukonga, Dar es Salaam jana, wakati wa ziara ya kutembelea Mahakama za Mwanzo. (Picha na Prona Mumwi)

Mwalimu Mkuu Ifunda anusurika kuuawa



Na Eliasa Ally, Iringa

WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Ifunda, iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Vijijini, jana walifanya vurugu kubwa shuleni hapo na kutaka kumuua Mkuu wa shule hiyo, Bw. Shaaban Nsute.


Na Grace Ndossa

MAHAKAMA ya Rufaa nchini, jana imetupilia mbali ombi la Kampuni ya Kufua Umeme wa Dharura ya DOWANS, kutaka Shirika la Umeme nchini (TANESCO), liilipe zaidi ya sh.
bilioni 122, kwa kuvunja mkataba kinyume cha sheria.

GEMA HATARI


Wapitanjia wakipita kando ya gema eneo la Magomeni Mapipa, Dar es Salaam jana. Gema hilo linalotishia usalama wa nyumba zilizopo karibu limesababishwa na mmomonyoko wa udongo kutokana na mvua za masika zinazoendelea kunyesha jijini. (Picha na Charles Lucas)

Rais Kikwete ahimiza ufugaji wa kisasa


Na Freddy Maro, Bagamoyo

RAIS Jakaya Kikwete, amewataka wafugaji nchini kupima na kupanga ardhi kwa ajili ya ufugaji bora wenye tija ili kuepusha
migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

Bodo Mpya TBS ilete mabadiliko-Dkt. Kigoda


Na Reuben Kagaruki

SERIKALI imeiagiza Bodi ya Mpya ya Shirika la Viwango nchini  (TBS), kufanya haraka mabadiliko ya Menejimenti ya shirika hilo na idara zake ili kukirejesha chombo hicho kwenye hadhi yake.

MSHANGAO


Baadhi ya wapitanjia wakilishangaa tingatinga lililokuwa likiondoa tope chini ya daraja la Jangwani, Dar es Salaam jana. Tabia ya baadhi ya wananchi kushangaa hata mambo ya kawaida linasababisha kupoteza muda wa kujishughulisha katika masuala muhimu ya maendeleo yao. (Picha na Charles Lucas)

Jela miaka 30 kwa ujangili



Na Mary Margwe, Babati

MAHAKAMA ya Wilaya ya Babati, mkoani Manyara, imemuhukumu Bw. Hamis Said (32), kutumikia kifungo
cha miaka 30 jela na kulipa faini ya sh. milioni 10.

Dkt. Bilal: Muungano usidharauliwe


Na Veronica Modest, Butiama

MAKAMU wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilal, amewataka Watanzania kutoudharau Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar badala yake uheshimiwe na kulindwa.

04 March 2013

AJIRA


Wasichana hawa walikutwa na mpigapicha wetu wakisafisha vioo vya magari yaliyokuwa katika foleni katika makutano ya Barabara za Nyerere na Msimbazi, Dar es Salaam jana, tatizo la ajira kwa vijana linachangia baadhi yao kubuni ajira zisizo rasmi ili kujipatia kipato. Hata hivyo malipo ya kazi hiyo ambayo hufanyika bila makubaliano hutegemea huruma ya mwenye gari. (Picha na Charles Lucas)

Kagasheki, Meya 'waipasua' CCM *Mgogoro wao wadaiwa kuvuka mipaka *Nape: Tume iundwe kuchunguzi tuhuma



Na Theonestina Juma, Bukoba

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, kimesema mgogoro wa kisiasa katika Manispaa ya Bukoba, mkoani Kagera, kati ya Meya wa Manipaa hiyo Dkt. Anatory Amani na mbunge wa jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kashakeki, umevuka mpaka.

SAMAKI


Mfanyabiashara akiwa amenyenyua samaki juu akinadi bei ya samaki huyo kwa sh. 4,000 katika Soko la Kimataifa Feri Dar es Salaam juzi.(Picha na Prona Mumwi)

Mbowe apewa ushauri wa bure *Viongozi wa dini wamtaka asitishe maandamano



Na Mwandishi Wetu, Mbeya

KAMATI ya Maadili na Haki za Binadamu kwa Jamii inayoongozwa na Maaskofu, Mapadre, Wainjilisti na walimu, imekiomba Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kusitisha maandamano waliyopanga kuyafanya jijini Mbeya wiki hii.

Maandamano kumpinga Muingereza yaandaliwa


Na Rose Itono

SIKU chache baada ya baadhi ya vyombo vya habari nchi kutoa matangazo yanayohusu udhalilishaji unaodaiwa kufanywa na raia
wa Uingireza dhidi ya Watanzania, taasisi isiyo ya kiserikali ya Human Settlement of Tanzania (HUSETA), imeamua
kuchukua hatua ya kupinga udhalilishwaji huo.

Moravian: Msemaji wa Kanisa ni M/kiti tu



Na Charles Mwakipesile, Mbeya

KANISA la Moravian nchini, Jimbo la Kusini, limemkana Mchungaji Emaus Mwamakula na kusema yeye si msemaji wa kanisa hilo Jimbo la Misheni, kama anavyodai.

MVUA


Gari lenye namba T 450 AFK likipita katika maji yaliyotuama katikati ya Barabara ya Uhuru, mtaa wa Kongo ambapo maji hayo yametokana na mvua zilizonyesha maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam jana.

Mwanafunzi kidato cha nne awaua


Na Mercy James, Njombe

MWANAFUNZI wa kidato cha nne katika Sekondari ya Ikuwo, Tarick Mbwilo (18), ameuawa na watu wasiofahamika pamoja
na mama yake mzazi Ester Mwalukolo (49).

Makamba: Nachonganishwa na CCM


Na Yusuph Mussa, Korogwe

KATIBU Mkuu mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Yusuf Makamba, amesema baadhi ya vyombo vya habari nchini vinamchonganisha na chama chake.

Wauza samaki Feli wafungiwa geti na uongozi




Na Anneth Kagenda

MAGARI yaliyobeba samaki, jana yalifunga babaraba katika Soko
la Kimataifa la Feli baada ya uongozi wa soko hilo, kufunga geti ambalo hutumiwa na magari hayo kuingiza samaki sokoni hapo.

FERI


Wafanyabiashara wa Soko la Kimataifa la Samaki Feri jijini Dar es Salaam wakitishia kuvunja geti baada ya kufungwa kama wanavyoonekana wafanyabiashara hao wakishinikiza kufunguliwa kwa geti hilo.(Picha na Prona Mumwi)

'Mfumo wa elimu sasa uangaliwe upya'


Na Raphael Okello, Bunda

MFUMO wa Elimu nchini, bado haujawawezesha wahitimu
kuwa wabunifu na kuwapa maarifa ya kupambana na maadui
watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini.

Hatima ya Ponda kujulikana leo




HATMA ya Katibu wa Junuiya za Taasisi za Kiislam nchini Sheikh Issa Ponda na wenzake 49 itajulikana leo ambapo  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu itatoa uamuzi kama wana kesi ya kujibu au la, anaripoti Rehema Mohamed.

PAMBO


Mmoja wa mafundi Ujenzi, Bw. Sadick Ally akiangalia sanamu ya samaki aina ya papa lililopo katika makutano ya Barabara za Uhuru na Msimbazi, Dar es Salaam jana. Sanamu hiyo imewekwa kwa ajili ya mapambo katika eneo hilo. (Picha na Peter Twite)

JK ashangazwa na matokeo IV *Asema tume ya Pinda itatoa majibu stahiki *Adai vurugu za kidini kamwe hazivumiliki



SAKATA la matokeo mabaya ya wanafunzi waliomaliza kidato
cha nne mwaka 2014, limeigusa Serikali ambayo imekiri kuwa, jamii inahitaji kupatiwa majibu ya uhakika kuhusu anguko hilo.

Siri ya ushindi CCM-2015 yafichuka *Lowassa: Ipo siku Mungu atanipa utajiri



Na Daud Magesa, Mwanza

WAZIRI Mkuu mstaafu, Bw. Edward Lowassa, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM), kitashinda vizuri uchaguzi Mkuu wa 2015, kama Serikali itarejesha utaratibu wa kuwapa mikopo wajasiliamali kupitia ‘Mabilioni ya JK’, ili waweze kujikomboa kiuchumi.

KEKI


Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda (kushoto), akikata keki kuashiria kutimiza Miaka 2 ya GS1 Tanzania, Dar es Salaam (Na Mpigapicha Wetu)

Mganga wa kienyeji azua 'kizaazaa'



Na Steven William, Muheza

KUNDI la wakazi waishio Kijiji cha Kibanda, Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga, juzi waliandamana hadi katika Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya hiyo kushinikiza mganga wa kienyeji aliyefahamika kwa jina la Aweso Kipaku, apewe kibali cha kuwasaka na kuwafichua wachawi waliopo kijijini hapo.

Shibuda 'awalipua' viongozi wa CCM


Na Suleiman Abeid, Maswa

MBUNGE wa Maswa Magharibi, mkoani Simiyu, Bw. John Shibuda (CHADEMA), amekebea tabia ya baadhi ya viongozi
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayi humi wanaolitumia vibaya jina la Rais Jakaya Kikwete kuwatisha watendaji wa
Serikali.

Shahidi 'amkaanga' Mbunge Badwel



Na Rehema Mohamed

MENEJA wa Idara ya Mapokezi katika Hoteli ya Peacock, Bw. Casto Crales, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa, yeye ni miongoni mwa watu waliozithibitisha fedha za mtego wa rushwa alizokamatwa nazo Mbunge wa Bahi, mkoani Dodoma, Bw. Omary Badwel, kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU).

UZINDUZI


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Freeman Mbowe akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Baraza la Nyanda za Juu Kusini, Jijini Mbeya jana. (Picha na Rashid Mkwinda)

Bila Serikali kuchukua hatua, vita ya rushwa kamwe haitakoma



TATIZO la rushwa nchini lipo katika sekta mbalimbali lakini
hali hiyo haina maana kuwa inakubalika katika jamii.