04 December 2013

MPASUKO ZAIDI CHADEMA

  • M/KITI SINGIDA AJIUZULU, ASEMA HAKUNA DEMOKRASIA


Damiano Mkumbo na Darlin Said

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mkoani Singida, Wilfred Kitundu, amejiuzulu rasmi nafasi hiyo akipinga mambuzi ya Kamati Kuu kuwavua nyadhifa za uongozi viongozi wake watatu.


Viongozi hao ni aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Zitto Kabwe, Dkt. Kitila Mkumbo na Bw. Samson Mwigamba ambao wanadaiwa kukisaliti chama hicho.Akikzungumza na waandishi wa habari jana, Bw. Kitundu alisema kinachoendelea ndani ya chama hicho kwa sasa ni udhalilishaji wa demokrasia ya kweli.

Alisema uamuzi aliochukua ni hiari yake bila kushawishiwa na mtu akiwa na dhamira ya kulinda demokrasia ya kweli ili kuhakikisha inaimbwa na kutekelezwa kwa vitendo."Mimi ni mwanachama wa kwanza kujiunga na CHADEMA, mkoani hapa pia ni mwanachama wa 300 kitaifa, ninayo heshima kubwa kwangu, sipo tayari kuipoteza heshima hiyo kwa kukubali kuwa sehemu ya udharirishaji huu wa demokrasia.

"Nitaendelea kuwa mwaminifu na mwadilifu ili kutetea haki na Demokrasia siku zote bila kurudi nyuma," alisema na kuongeza kuwa, kitendo cha kumvua nyadhifa za uongozi Bw. Kabwe na wenzake si kizuri na kimeacha maswali mengi yanayoulizwa na wanachama wake," alisema Kitundu.

Aliongeza kuwa, msimamo wa CHADEMA mkoani humo ni kulaani, kupinga na kukemea maamuzi hayo ambayo yamejaa chuki, hofu na wasi wasi mwingi hasa kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu ndani ya chama.

Katika barua yake ya kujiuzulu ambayo alimwandikia Katibu Mkuu wa chama hicho mkoani humo, alisema Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bw. Freeman Mbowe, anapaswa kutoa neno ili wanachama na wananchi waendelee kikielewa vizuri chama hicho badala ya kikigawa vipande.

"Msimamo mwingine ni kumtaka Bw. Mbowe na Katibu Mkuu,Dkt. Wilbrod Slaa, kuitisha mara moja mkutano wa Baraza Kuu la chama ili kutoa maamuzi ya suala hili kwani lilifanywa na watu wachache kwa masilahi yao," alisema.

Alishauri jambo hilo ni la msingi sana na maamuzi ambayo yatatolewa yame makini ili kudumisha hali ya utulivu ndani ya chama kiendeleze umarufu wake kwani ipo siku kinaweza kuongoza dola.Kitundu mbali ya kushika nafasi ya Mwenyekiti wa chama Mkoa, pia aliwahi kuwa muasisi na mlezi wa CHADEMA
(1992-2013), Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa (1992-2013) na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa (1992-2013).

Katika hatua nyingine, Katibu wa CHADEMA mkoani humo,Bw. Patric Msuta, amekiomba chama hicho kuitisha kikao cha Kamati Kuu kikae meza moja na viongozi wenye mgogoro na chama ili kumaliza tofauti zilizojitokeza.

Bw. Msuta aliyasema hayo hivi karibuni katika mkutano wake waandishi wa habari na kusisitiza kuwa, tangu mgogoro huo uanze, hakuna mwanachama aliyerudisha kadi."Hapa Singida, chama chetu hakina mpasuko wowote kwani wanaelewa vizuri msingi wa maamuzi wa Kamati Kuu kutokana na mgogoro uliyopo ndani ya chama chetu ambao naamini utamalizika kwa njia ya amani," alisema.
 

17 comments:

  1. Majira,
    Mbali na kutoa taarifa za baadhi ya viongozi wanaojiuzuru hebu kama mna divisheni ya utafiti itumieni ili ikusanye maoni juu ya matatizo ya hawa wanaharakati "Kama Joseph Khonyi" muone wangapi wanaunga mkono Zitto kuvuliwa nyadhifa, wangapi wanakataa Zitto kuvuliwa.

    Kisha ripoti hiyo watanzania waijue.

    KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

    ReplyDelete
  2. Usicheze na pesa. Zito sasa kwisha! Ashasahaulika. Wenzake wana pesa ya kutosha kuruka ncchi nzima. Ni zaidi ya serikali. Wanatembeza ubabe kama dola vile

    ReplyDelete
  3. Wenye akili mgando, wasiosoma, na matusi mengine mengi yameirudishia fadhila CHADEMA. Wamepewa kata tatu kati ya ishirini na saba. Tunawasubiri uchaguzi mkuu mtueleze vizuri kwanini mnatutukania wazee wetu kwamba wanadanganyika na kofia na kanga za CCM. Rusheni helkopta zenu sie tutatembea kwa miguu.

    ReplyDelete
  4. thanks for good sharing information

    ReplyDelete
  5. En el canto.

    Siento radiante
    un canto y
    una rima pasar
    donde el sueño
    describe la noche
    y una tierna
    poesía.

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete
  6. Le sourire et le conte du cœur.

    Quelquefois
    le murmure de
    la soirée m'invite
    à traduire le
    chant de la mort,
    et alors le sourire
    devient le manteau
    et un son délicat.

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete
  7. La clarté des sentiments.

    Dans le reste
    de la soirée
    je vois une
    lumière et le
    tendre cadeau
    d'une chanson
    très joyeuse.

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete
  8. En el canto.
    ( last version )

    Cuando viene
    una sombra
    invocando el
    candor de la noche
    estrellada siento
    un llanto y una
    rima avanzar
    suavemente en
    el sueño encantado
    de una tierna
    poesía: la emoción
    reaparece, un eterno
    sonido se difunde
    en el viento regalando
    la gracia de la nueva
    armonía.

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete
  9. Le souffle des sourires.

    Quand le chant
    de la neige
    revient tendrement
    où l'eau disparaît
    j'écoute, en silence,
    la route des
    sourires.

    Francesco Sinibaldi



    Quand le son disparaît...
    ( other version )

    En marchant sur
    le sentier qui traverse
    la douce campagne
    je médite sur le présent
    qui rappelle une
    sensation: c'est très
    agréable décrire
    la lumière qui
    couvre le passage
    de la brise qui
    retourne...

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete
  10. The martin's song.

    In the light
    of a white
    rose there's
    a delicate
    swallow, the
    sound of a
    stream and
    a gentle delight.

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete
  11. La frontière de mes mots.

    Je mentionne la
    vie qui brille,
    silencieuse, dans
    la première pensée
    d'une nouvelle
    émotion et ainsi
    cette mémoire,
    dans ton coeur,
    rappelle la lumière.

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete
  12. El claro sonido.
    ( other version )

    El amor reaparece
    trayendo un suspiro
    y la fuerza ilusoria
    de una imagen
    lejana: como un
    fulgor en la limpidez
    del cielo matutino,
    como un sueño
    luminoso que
    recuerda la pasión
    y una dulce cantilena...

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete
  13. Taciturn quietness.

    In the breath,
    in the sunshine,
    in a luminous
    singing walking
    alone near a
    delicate dream,
    in the tears
    of your care...

    Francesco Sinibaldi

    ReplyDelete

  14. Amazing post, I liked the article on this site. I love your way representation.
    Thank you too much and keep.


    Review my webpage - 부산오피
    (jk)

    ReplyDelete
  15. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  16. Reliable Dedicated Hosting

    Dedicated hosting servers can bring your online business to next level. If you are serious about your business you should opt for dedicated hosting servers only.


    to Learn more - https://www.dedicatedhosting4u.com/


    ReplyDelete