18 March 2013

Wakazi wa Majengo walalamika nyumba zao kujaa maji

Na  Patrick Mabula,
Kahama,


Wananchi wanaoishi eneo la mitaa  ya majengo  mjini Kahama wamelalamikia kero ya
mafuriko yanayotokana na mvua zinaponyesha  na kufanya mitaro kumwaga maji ambayo
huingia na kujaa ndani ya nyumba zao na kuwafanya wazikimbie na kulala nje huku
wengine wakilala kwa majirani.


Wakiongea na Majira mbele Ya nyumba zao zilizokuwa zimefurika maji kutokana na mvua
zinazoendelea kunyesha walisema wamekuwa wakilazimika kuzikimbia nyumba hizo
kutokana  na mafuriko hayo yanayosababishwa na mitaro iliyojengwa kupeleka maji kwa
kasi kweny makazi yao.

Bi.Roza Julius alisema nyumba zao zimekuwa zikifurika maji kila mvua zinaponyesha
katika msimu huu na kuwafanya walale nje  na wengine kwa  majirani  hadi asubuhi
wanapofanya  kazi   ya kumwaga kuyatoa nje .

Bw.Paulo Sambali alisema wamekuwa wakikumbwa na mafuriko kutokana na kasi ya maji
yanayotoka na mitalo iliyoimalishwa na Halmashauri ya mji wa kahama toka maeneo ya
mitaa ya boma , sokoni , nyamwezi , lumelezi , nyihogo  ambayo imekuwa ikasababisha
athari.

Bw.Felex Soko alisema kabla ya mitaro hiyo mikubwa iliyopo barabara kuu la lami
hajaimarishwa kupitisha maji walikuwa hawapati tatizo hilo  toka ilipopanuliwa mwezi
mmoja uliopita sasa hivi kila mvua ikinyesha nyumba zao zinapata mafuriko.

Bw.Juma Shagile katika malalamiko yake juu ya kero hiyo aliitaka Serikali iwanusuru
na kero hiyo kwa vile imekuwa ikiwasababishia vitu na mali zao kuharibika kutokana
na maji yanayofurika eneo lao na kujaa ndani ya nyumba zao.

Katibu wa Baraza la wazee wa wilaya ya Kahama  Bw.Paulo Ntelya aliyeshuhudia tatizo
hilo la alisema kero hiyo wataifikisha kwa viongozi husika wa Serikali kuhusu
wananchi wa mitaa ya majengo wanavyoteseka na mafurika hayo katika misimu huu wa
mvua.

Diwani wa kata ya Majengo Bw.Bobson Wambura alisema katika  mitaa hiyo inatokana na
udogo wa mitaro inayopokea maji toka barabara kuu ya rami  na kutokana na nyumba
hizo kuwa misingi yake ipo chini  husababisha maji kufurika ndani na aliwaahidi
kulifikisha  kwa  vyombo husika vya serikali  liweze kutatuliwa.

No comments:

Post a Comment