30 November 2011

Mafisadi CCM kung'oka rasmi

*Kamati ya Maadili sasa yapewa meno
*Mukama asema hakuna kurudi nyuma
*Viongozi waagizwa kuwachukulia hatua


Na Rehema Mohamed

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza rasmi hatua ya kuwashughulikia watuhumiwa wa ufisadi ndani ya chama hicho kwa

JK asaini Muswada Katiba Mpya

*Asema nafasi ya kuuboresha bado ipo wazi
*Wanaharakati wapinga, waishukia CHADEMA


Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete, jana amesaini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Mpya 2011, uliopitishwa na Bunge mjini
Magari mawili yenye namba T 361 AEW daladala Isuzu Journey (kulia) na lori Isuzu Canter T 602 AZY,(kushoto), yakiwa yamegongana na kuziba Barabara ya Msimbazi Kariakoo Dar es Salaam jana.

Mwenyekiti NCCR Mbeya wamkataa Mbatia

Na Esther Macha, Mbeya

WENYEVITI wa NCCR-Mageuzi katika wilaya zote mkoani Mbeya, wamemtaka Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Bw. James Mbatia, kujiuzulu wadhifa wake kwa
Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge na Huduma za Jamii, Dkt. William Mgimwa, akizungumza wakati wa mkutano wa majumuisho ya kutembelea, Mabaraza ya Watoto kwa wawakilishi wa kamati za kudumu za bunge, Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Mradi wa Shirika la Haki za Watoto Tanzania, Bw, Mussa Mgata.

TAMWA yaionya Serikali, wataka ithamini waandishi

Na Benjamin Masese

SERIKALI imehadharishwa kuimarisha ushirikiano na vyombo vya habari, kutoa taarifa mbalimbali kwa wakati kwani kitendo cha baadhi ya watendaji kushindwa

Wawekezaji siyo lazima watoke nje-Waziri Pinda

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu Bw. Mizengo Pinda, amesema suala la uwekezaji nchini haliwalengi watu wa nje tu, bali hata wa ndani wanaweza kuwekeza hata kwa kiwango
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bw, Abbas Kandoro, (wa pili kulia) akipita kwenye mabaki ya Soko la Tunduma, lililoungua hivi karibuni.
Baadhi ya wateja wakichagua na kununua nguo, zilizokuwa zikiuzwa kwenye baiskeli ya mfanyabiashara ndogondogo mwenye ulemavu Kariakoo Dar es Salaam jana.

Mwenge wa uhuru Temeke

Na Andrew Ignas

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni ambaye pia ni  kaimu Ukuu wa wilaya ya Temeke BW. Jordan Lugimbani amewataka viongozi wa serikali kuhakikisha wana simamia na kulinda  rasilimali mbali mbali ili ziweze kuwanufaisha vizazi vijazo.

Chipolopolo, Mbena kuzipiga Des. 2

Na Severin Blasio, Morogoro

MABONDIA wa ngumi za kulipwa mkoani Morogoro, Maneno William รข'Chipolopolo' na Albert Mbena wanatarajiwa kupigana Desemba 2 mwaka huu katika pambano lisilo la ubingwa.

Marsh awatetea akina Mkwassa

Na Shufaa Lyimo

KOCHA Msaidizi wa Taifa Stars Silvester Marsh, amewataka Watanzania kuacha kuwatupia lawama makocha wa timu ya Kilimanjaro Stars, Charles Boniface na Jamhuri Kihwelu 'Julio' baada ya kuanza vibaya mashindano ya Tusker Chalenji, yanayoendelea Dar es Salaam.

Simba Tishio yaipa tano Simba B

Na Omary Mngindo, Kibaha

UONGOZI wa tawi la Simba la Kibaha Kwamfipa (Simba Tishio), umeipongeza timu ya vijana ya chini ya miaka 20 ya klabu hiyo, kwa kutwaa ubingwa wa michuano Kombe la Uhai, iliyomalizika mwishoni mwa wiki.

Azam kukuza soka mikoa ya Kusini

Na Shufaa Lyimo

UONGOZI wa Klabu ya Azam FC, umesema utahakikisha unakuza na kuinua vipaji vya vijana wenye umri chini ya miaka 20, katika Mikoa ya Kusini.

Kesi ya Shabani Mintanga

Akina Mtagwa watakiwa nchini

Rehema Mohamed na Neema Malley

WASHTAKIWA wanaoshikiliwa nchini Mauritius kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya, Petro Mtagwa, Case Ramadhan na Nathalias Charles ambao ni mabondia waliokwenda nchini humo 2008, kushiriki michuano ya ngumi waletwe nchini kwa ajili ya kutoa ushahidi wa kesi hiyo, ambayo pia inamkabili Rais wa zamani wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), Shabani Mintanga.

Kili Stars yazindukia Djibouti

Yaichapa 3-0, mashabiki Simba, Yanga wajigawa kuisapoti
*Rwanda hiyo robo fainali

Na Zahoro Mlanzi

TIMU ya Taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars imefufua matumaini ya kutinga hatua ya robo fainali baada ya kuichapa Djibouti mabao 3-0 katika mchezo wa kuwania Kombe la Chalenji uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

29 November 2011

Maafa Mto wa Mbu

*Mafuriko yasababisha kifo, wananchi wakimbia makazi
*Mawasiliano Arusha, Karatu yakatika, eneo lageuka kisiwa
*Askari JWTZ wapelekwa eneo la tukio, vijana wapata ajira


Na Said Njuki, Monduli

WAKATI mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa mbalimbali nchini, zikisababisha
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Pugu Mwakanga, wakipita kwenye reli, wakati wakitoka shule Dar es Salaam jana, kitendo kinachoweza kuhatarisha maisha yao, elimu inapaswa kutolewa ili kudhibiti tabia hii kabla ya madhara kutokea.

Mtoto auawa akidaiwa kuiba sh. 10,000

*Akatwa mapanga mwili mzima
*Petroli yalipua nyumba, 2 wafa


Na John Gagarini, Kibaha

WATU sita wamekufa mkoani Pwani katika matukio tofauti likiwemo la mtoto Kelvin Mapundu (7), mwanafunzi wa
Mwendesha Baiskeli ya magurudumu matatu (Guta) ambayo hutumiwa kwa ajili ya kusafirisha mizigo, akisukuma baiskeli yake kando ya Barabara ya Mnyamani Buguruni, Dar es Salaam jana, akiwa amewapakia watoto wadogo bila kujali usalama wao.

Mawakili wataka kesi ya CHADEMA Arusha ufutwe

Queen lema, na Pamella Mollel, Arusha

UPANDE wa utetezi katika kesi inayowakabili viongozi waandamizi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umewasilisha

Chanzo cha ajali Kibaha,Chalinze chatajwa

Na Peter Mwenda

WAUMINI wa Kanisa Katoliki Tanzania wametaja chanzo cha ajali za mara kwa mara katika eneo la Chalinze na Kibaha Mkoa wa

Tunatarajia kiwanda cha sukari Songea-RC

Na Emmanuel Msigwa, Songea

MKOA wa Ruvuma upo kwenye mikakati ya kuwashawishi wawekezaji kujenga  kiwanda cha sukari mkoani humo pamoja na kufufua
Kocha mpya wa timu ya Simba, Milovan Cirkovic (mwenye miwani) akishuhudia mechi kati ya Malawi na Kenya ya kuwania Kombe la Chalenji, iliyopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana.Kocha huyo amesaini mkataba wa miezi sita kwa ajili ya kuinoa timu hiyo.
Beki wa timu ya Taifa ya Malawi, Steve Chagoma akimiliki mpira huku akizongwa na mshambuliaji wa Kenya 'Harambee Stars', Paul Were wakati wa mechi ya Kombe la Chalenji, iliyopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana.Malawi ilishinda mabao 2-0.

Kili Stars kibaruani tena leo

Na Zahoro Mlanzi

MABINGWA watetezi wa michuano ya Chalenji Kilimanjaro Stars, leo itakuwa na kibarua kingine ambapo itamenyana na Djibouti, katika

Bab atua Azam FC

Na Mwandishi Wetu

Baada ya mkataba wake kusitishwa na Klabu ya DT Long An ya Vietnam, kiungo Abdi Kassim 'Babi' jana amesajili kuichezea Azam FC ya

Kamati yasikitishwa na Z'bar Heroes

Na Mwajuma Juma, Zanzibar

KAMATI ya Mashindano ya Kombe la Mapinduzi Zanzibar (Mapinduzi Cup), imesikitishwa na timu ya taifa ya Zanzibar

28 November 2011

Mafisadi CCM sasa wakalia kuti kavu

*Mkakati wa kuwamaliza kidiplomasia yatajwa
*JK alikwepa mtafaruku,kupisha upepo mbaya


Na Mwandishi Wetu

SIKU tatu baada ya kumalizika kwa vikao vya juu vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma wiki iliyopita, upepo mbaya umeanza

JK ateta na CHADEMA Ikulu

Na Mwandishi Wetu
Rais Jakaya Kikwete (kulia), akiangalia ripoti ya mapendekezo ya katiba mpya iliyowasilishwa kwake na Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Freeman Mbowe Ikulu, Dar es Salaam jana.

HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bw. Freeman Mbowe, ameongoza ujumbe wa chama

Chakula cha sumu Sengerema

*Mama naye afariki Dunia

Na Mwandishi Wetu

SIKU moja baada ya Famili ya Bw. John Mashauri, wa Kijiji cha Mwabaluhi, wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza, kupoteza
Mbunge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA, Bw. John Mnyika (aliyesimama), akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu Maalumu wa Klabu ya waandishi wa habari Dar es Salaam (DCPC) uliofanyika juzi, wakati wa uchaguzi wa viongozi wa klabu hiyo.

Wanasiasa wanataka kumwaga damu -Mchungaji

*Ataka majadiliano si maandamano Katiba Mpya

Na Charles Mwakipesile, Mbeya

MWENYEKITI wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini, Mchungaji  Clement Mwaitebele, ameibuka na kukemea
Barabara ya Uhuru ambayo ilitumiwa na serikali kuingiza wageni wa kitaifa nchini, inawekwa viraka kila wakati na kupoteza uhalisia wa barabara hiyo, kama inavyoonekana mafundi wakiandaa mashimo kwa ajili ya kuweka viraka vipya Dar es Saalam jana.

NCCR wamwonya JK mchakato wa Katiba

Na Peter Mwenda

CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimetoa tamko rasmi kuhusu muswada wa sheria ya kuundwa kwa Tume ya kukusanya maoni ya wananchi

Wataka barabara ya lami kwenda hospitali

Na Eliasa Ally, Iringa

WANANCHI wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wameitaka serikali kuangalia uwezekano wa kuitengeneza kwa kiwango
Meya wa Manispaa ya Ilala, Bw. Jerry Silaa akipanda mti wa kivuli katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana, baada ya Lions Club kuikabidhi manispaa hiyo visima vya maji kwa ajili ya shule za msingi na sekondari vyenye thamani ya mil. 8.2.

Vijana tafakarini kabla ya kutenda -Manyanya

Na Bryceson Mathias Dodoma

MKUU wa Mkoa wa Rukwa na Mbunge wa viti Maalum (CCM) Mhandisi Stella Manyanya, ametaka vijana nchini kusaidia nchi yao

RC Mara akumbana na kilio cha maji Bunda

Na Raphael Okello, Bunda

SAKATA la kucheleweshwa kwa mradi mkubwa wa maji unaofadhiliwa na Benki ya Dunia (WB) mjini Bunda mkoani Mara tangu

Zanzibar Heroes yakaa pabaya

*Yatoka suluhu na Burundi, Zimbabwe yatakata

Na Zahoro Mlanzi

JAHAZI la timu ya Taifa ya Zanzibar 'Zanzibar Heroes', limezidi kwenda mrama baada ya kutoka suluhu na Burundi
Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes), Ali Badru Ali (kushoto), akimtoka beki wa timu ya Taifa ya Burundi, Ndayisaba Floribert wakati wa mechi ya kuwania Kombe la Chalenji, mchezo uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana.Timu hizo zilitoka suluhu.

Milovan kimeeleweka Simba

Zahoro Mlanzi na Amina Athumani

ALIYEKUWA Kocha Mkuu wa timu ya Simba, Milovan Cirkovic ametua nchini juzi usiku na muda wowote ndani ya wiki anatarajia

25 November 2011

Kashilila aichefua CHADEMA upya

 *Wamshangaa kauingilia mambo yao, kupotosha umma
*Wamtaka awataje wabunge wachanga wasiojua sheria
*Mnyika amshukia Makinda, asema alipuuza wabunge

Na Benjamin Masese

SIKU moja baada ya Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilila, kudai mazungumzo kati ya Rais Jakaya Kikwete na Kamati teule ya
Waziri wa Katiba na Sheria , Bi. Celina Kombani (katikati) akikata utepe kuzindua Maonesho ya Miaka 50 ya Ikulu, Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mama Maria Nyerere, Mjane wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Mkuu wa Sehemu ya Mipango Ikulu Bi. Ened Munthali.

ZUIO LA MAANDAMANO:

Jukwaa la Katiba lajibu mapigo

*Lasema maandamano ni Haki ya Watanzania

Na Rachel Balama

JUKWAA la Katiba Tanzania ambalo linajumuisha asasi za kiraia zaidi ya 180 vikiwemo vyama vya wafanyakazi, wanataaluma, waishio na VVU/UKIMWI, vyama vya
Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Konde Dkt. Israel Mwakyolile akimweleza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro (aliyeketi kulia) kuwawajibisha maofisa wa Jiji hilo waliosababisha vurugu wiki mbili zilizopita. Mkutano huo uliitishwa na viongozi wa dini kutathmini hali ya maendeleo ya mkoa kwa miaka 50 ya Uhuru.

NEC-CCM yamkaanga Ng'enda

Na pendo Mtibuche, Dodoma

HALMASHAURI Kuu ya Taifa (NEC), Chama Cha Mapinduzi (CCM), imeanza kuonesha makali yake baada ya Bw. Kilimbe Ng’enda kuvuliwa ukatibu wa chama hicho

Vyama vya Siasa vyatofautiana kukutana na Rais Kikwete

Na Rabia Bakari

USHAURI wa Kamati Kuu (CC), ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutaka Rais Jakaya Kikwete akutane na vyama vyote vya siasa vyenye uwakilishi bungeni ili
Katibu wa Kamati ya kutetea haki za Waislam Tanzania, Sheikh Issa Ponda (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, wakati akitoa onyo kwa serikali ya Tanzania isitumiwe na Marekani kukandamiza Uislamu.

Wanachama CHAWATE waitupia lawama ofisi ya Ushirika Temeke

Na  Salim Nyomolelo

BAADHI ya wanachama wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Walimu wilayani Temeke (CHAWATE SACCOS), wameilalamikia ofisi ya ushirika wilayani
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZ), Dkt. Adelhelm Meru (kulia), akisalimiana na Profesa Dorothy McCormick wa Chuo Kikuu cha Nairobi, wakati wa warsha ya wasomi, viongozi wa serikali na watu wenye uzoefu katika uzalishaji wa nguo iliyofanyika Dar es Salaam jana. Katikati ni Mkurugenzi wa Bisahara, Chuo Kikuu cha Mzumbe Profesa Andrew Mwambo.

Waislamu Dar waihadharisha serikali tishio la Al-Shaabab

Na David John

KAMATI ya Kutetea Haki za Waislamu nchini, imeihadharisha Serikali kutojihusisha na mambo ya kidini hasa yanayohusu kundi la Al-shaabab kwa shinikizo la mataifa

TBS yanasa mabati bandia, yapigwa mafuruku sokoni

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limepiga marufuku uzaaji wa mabati yanayouzwa na kampuni ya Kamaka CO LTD, iliyopo Barabara ya Mandela, jijini Dar es Salaam, baada ya
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni  Future Centery Helene Masanja, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu mechi ya kombaini ya Simba na Yanga, itakayocheza dhidi ya Asante Kotoko ya Ghana, katikati ni Mwenyekiti wa Yanga Loyd Nchunga na Mwenyekiti wa DRFA Amin Bakharesa.

Simba, Yanga zaungana

*Zaamua kuunda timu moja

Na Amina Athumani

WAPINZANI wa jadi nchini timu za Simba na Yanga, kwa mara ya kwanza katika historia ya soka zimeungana kuunda timu moja, ambayo itacheza na

Mwaikimba, Bocco watemwa Kili Stars

Na Amina Athumani

WACHEZAJI kumi kati ya 28, walioitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), wamechujwa katika kikosi hicho wakiwemo

Caravans yaandaa mashindano ya kriketi

Na Zahoro Mlanzi

KLABU ya kriketi ya Caravans, imeanzisha mashindano ya mchezo huo yakayoanza Novemba 27 mpaka Desemba 11, mwaka huu kwenye Viwanja vya

24 November 2011

Polisi wazuia maandamano

*Wahofia uvunjifu amani, yalipangwa kufanyika J'mosi 
*Wanaharakati kutafuta njia nyingine kufikisha ujumbe

*IGP Mwema asisitiza jeshi hilo halina nia mbaya

Na Benjamin Masese

SIKU moja baada ya wanaharakati kutoka asasi za kiraia zaidi ya 180, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) na Jukwaa la Katiba Tanzania kutangaza kufanya maandamano ya  amani nchi nzima Novemba 26 mwaka huu, Jeshi la Polisi nchini limeyazuia kutokana na hofu ya kuvunjika kwa amani.

Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Wilbroad Silaa akizungumza na Karani wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Bi. Anna Msofe jana, baada ya kesi yao  ya kufanya mkusanyiko kwenye viwanja vya NMC kinyume cha Sheria hivi karibuni kuhairishwa.

Ajali mbaya yaua wawili Dar

Salim Nyomolelo na Masau Bwire

Wakazi wa Jiji Dar es salaam wakiangalia gari dogo lililoharibiwa vibaya baada ya kugongwa nlori jana
Polisi akiangalia moja ya magari mawili yaliyopata ajali mbaya kwa kugongwa na lori la mafuta T 264 BUC Barabara ya Mandela, Dar es salaam jana.
Askari wa Usalama Barabarani akiwa amebeba Kichwa cha mtu aliyefariki baada ya kugongwa na lori jana maeneo ya Riverside Ubungo Jijini Dar es salaam.
WATU wawili wamekufa na wengine wanne kujeruhiwa vibaya baada ajali mbaya iliyotokea jana saa saba mchana katika eneo la

Serikali isitishe ombi la Tanesco

Na Rachel Balama

SERIKALI imetakiwa kusitisha ombi la dharura la kupandisha bei ya umeme kwa kiwango kikubwa ili kuepusha athari katika usalama na
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimsalimia Mbunge wa Monduli na Mjumbe wa NEC, Bw. Edward Lowassa. wakati wa kikao cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye Ukumbi wa White House mjini Dodoma jana. Kulia kwa Bw. Lowassa ni Waziri Mkuu Mstaafu Bw. Fredrick Sumaye na Bw. Kingunge Ngombale Mwiru (kulia)

Bush kutembelea Tanzania

Na Godfrey Ismaely

RAIS Mstaafu wa Marekani, Bw. George Bush anatarajiwa kufanya ziara yake ya kikazi nchi, ziara ambayo itakuwa ya siku tano
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Biashara Dar es Salaam (UDBS) wakizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Islamic Banking Bw. Amman Muhammad (kushoto) baada ya semina kuhusu taratibu za benki zinazofuata kanuni nza kiislamu (Shariah) Dar es Salaam juzi.
Beki wa timu ya vijana ya Simba,  Omari Kheri (kushoto) akiwania mpira wa juu na kiungo wa Toto Africa Severine Faustine, wakati wa mechi ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Uhai iliyochezwa Uwanja wa Karume Dar es Salaam jana. Simba ilishinda mabao 4-1.

Simba yawatoa kwa mkopo Kiemba, Kanoni

Na Amina Athumani

UONGOZI wa Simba, umewatoa kwa mkopo wachezaji wake beki Salum Kanoni aliyepelekwa Moro United na kiungo Amri Kiemba

Mchujo Kili Stars pasua kichwa

Na Amina Athumani

MAKOCHA wa kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), Boniface Mkwasa na Jamhuri Kihwelu 'Julio' jana

Munich, Inter, Benfica zafuzu 16 bora Ulaya

BERLIN, Ujerumani

BAYERN Munich, Inter Milan na Benfica zimefuzu hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, baada ya kucheza mechi

23 November 2011

Maandamano makubwa kumpinga JK Jumamosi

*Yatahusisha asasi 180,TUCTA, wenye VVU
*Ni kumshinikiza asisaini muswada wa katiba
*Kikwete afurahia kukutana na CHADEMA

Na Benjamin Masese

WANAHARAKATI wa asasi za kiraia zaidi ya 180, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) na Jukwaa la

Uvamizi viwanja:

Katibu Mkuu Ardhi apokea vitisho

Neema Malley na Jane Hamalosi

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka (wa pili kulia), akiangalia ramani halisi ya eneo la wazi lililoko Sinza Vatican, ambalo pamoja na kutengwa kwa ajili ya Michezo limevamiwa na kujengwa gereji, alipotembelea eneo hilo Dar es Salaam jana. Kulia ni Diwani wa Kata ya Sinza, Bw. Renatus Pamba, Mtendaji wa Kata Bw. David Mwakiposya (wa tatu kushoto) na Mwenyekiti wa serikali ya mtaa Sinza A Bw. Kassimu Kabulluh.

KATIBU  Mkuu wa  Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. Patrick Rutabanzibwa, amesema amekuwa
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM Januari Makamba (kulia), Kapteni Mstaafu John Chiligati (katikati) na Bi. Sofia Simba wakizungumza jambo, kabla ya kuanza kikao kwenye Ukumbi wa White House Makao Makuu ya Chama hicho mjini Dodoma jana.

Magamba CCM hayabanduki

*CC yachemsha, yaachia vikao vya juu

Na Pendo Mtibuche, Dodoma

KIKAO cha Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilichoanza kukutana juzi na jana mjini Dodoma, kimetawaliwa
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania, Bw. Sabasaba Moshingi, ( kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Bw. John  Mndeme baada ya  uzindunzi wa huduma ya TPB POPOTE  ulifanyika Dares jana.

Serikali yatakiwa kutoa habari kwa wananchi

Na Salim Nyomolelo

SERIKALI imetakiwa kujenga mazoea ya kutoa habari kwa wananchi ili kuwawezesha kutambua mabadiriko ya sheria, maendeleo

Serikali yatakiwa kuongeza uwekezaji sekta ya maji

Na Agnes Mwaijega

NAIBU Katibu Wizara ya Maji, Bw. Bashiri Mrindoko, amesema upo umuhimu mkubwa kwa serikali kuongeza uwekezaji katika sekta ya

Yanga kuingia kambini J'pili

Na Mwandishi Wetu

UONGOZI wa klabu ya Yanga umewataka wachezaji wa timu hiyo kuripoti kambini ifikapo Jumapili.Akizungumza Dar es Salaam jana
Vodacom Miss Tanzania 2011, Salha Israel akimkabidhi flana Mwenyekiti wa Kamati ya Tamasha la Utamaduni wa watu wa Mkoa wa Rukwa, Mwangaza Msongole. Katikati ni Meneja Mawasiliano wa Vodacom Salum Mwalim. Vodacom imekabidhi flana 1,000 zenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 14 kusaidia tamasha hilo.

TOC yaruka kimanga kozi ya ngumi

Na Amina Athumani

KAMATI ya Olimpiki Tanzania (TOC), imesema aihusiki na  kuvurugika kwa kozi ya kimataifa ya ngumi za ridhaa iliyoahirishwa.TOC imesema

Wanaokimbiza bendera waagwa Dar

Na waandishi maalumu

Wanariadha 30 wanaokimbiza bendera ya taifa, kupitia kampeni ya Kilimanjaro Jivunie uTanzania inayoenda sambamba na

22 November 2011

Moto wa Katiba Mpya CHADEMA kutinga Ikulu

*KAMATI Kuu yateua kamati ndogo ya muafaka
*Maandamano yawekwa kiporo kusubiri suluhu
*Mbowe: Hotuba ya rais imetusikitisha sana
*Wanaharakati Dar kutoa msimamo mzito leo


Na Benjamin Masese
Mwenyekiti wa Chadema Bw. Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu tamko la Chama hicho kutaka kuonana na Rais Jakaya Kikwete kumweleza msimamo wa kupinga rasimu ya katiba.

SIKU tatu baada ya Bunge la Tanzania kupitisha muswada wa Sheria ya kuundwa Tume ya Kukusanya maoni kuhusu
Wakazi wa Karakata Dar es Salaam, wakipita ndani ya maji juzi, wakati wakivuka kwenye njia iliyofurika maji kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

Polisi Moro yatangaza vita na waandishi

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

BAADHI ya askari wa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro, wametangaza vita na waandishi wa habari mkoani humo kwa madai kuwa, vyombo wanavyoandikia vinawatuhumu
Mjumbe wa Chama cha washereheshaji (SAA), Bw. Mackie Godwin (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu miaka 50 ya Uhuru kwa wenye ndoa walioishi pamoja kwa miaka 50. Wengine ni Elly Mgwala, Wiliam Chitanda na Steven Mwakajumba

Kamati Kuu CCM yawaka moto

*Taarifa ya Kamati ya maadili yaumiza kichwa wajumbe

Na Pendo Mtibuche, Dodoma

MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. Jakaya Kikwete, amefungua kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho cha siku mbili huku taarifa ya Kamati ya

CCM yaanza kujipanga kunyakua Ilemela, Nyamagana

Na Moses Matthew, Mwanza

KAMATI ya Habari na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza, imekamilisha kazi ya kupata maoni mbalimbali kutoka kwa

Utetezi kesi ya samaki wa Maguli yafungwa

Na Rehema Mohamed na Zena Mohamed

UPANDE wa utetezi katika kesi ya uvuvi haramu ndani ya Bahari ya Hindi kwenye kina kirefu cha Ukanda wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maarufu kesi ya ‘Samaki wa Magufuli'

Majambazi wateka mabasi matatu

Na Moses Mabula, Tabora

MAJAMBAZI sita wakiwa na bunduki pamoja na mapanga, wameteka mabasi matatu yaliyokuwa yakitokea Jijini Dar es Salaam kwenda Tabora na kupora mali pamoja na

Hakuna atakayewabugudhi wamachinga Mbeya-Kandoro

Na Charles Mwakipesile  Mbeya

MKUU Mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro, amewatangazia neema wafanyabiashara mdogondogo wa mitaani maarufu kama wamachinga kuwa hawatabugudhiwa na mtu yeyote
Beki wa timu ya vijana ya Simba Omari Kheri, akimkaba mshambuliaji wa JKT Oljoro Sannu Mwaseba wakati wa mechi ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Uhai, iliyochezwa Uwanja wa Karume Dar es Salaam jana. Simba ilishinda mabao 5-2.

Boban amchefua Julio

*SMG, Mgosi waitwa Kili Stars

Na Zahoro Mlanzi

PAMOJA na kupewa nafasi katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), mshambuliaji Haruna Moshi 'Boban' amemchefua Kocha Msaidizi wa

Wagombea ujumbe CECAFA waanikwa

Na Zahoro Mlanzi

JUMLA ya wagombea wanane kutoka nchi mbalimbali za Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ambao ni wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu vya ukanda
Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Sugu' katikati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), Dar es salaam jana kuhusu tamasha la burudani litakalofanyika, Novenba 26 katika viwanja vya Ustawi wa Jamii Kijitonyama (kushoto) ni msanii Fred Malik 'Mkoloni' na Zainabu Lipagile 'Zay B'.

Simba yainyuka Oljoro JKT

Na Shaban Mbegu

TIMU ya vijana ya Simba, jana imetinga nusu fainali ya michuano ya vijana ya Uhai Cup kwa kishindo, baada ya kuwafunga JKT Oljoro 5-3 katika mchezo wa robo fainali uliofanyika

Uchaguzi Mkuu FRAT sasa Aprili 24

Na Zahoro Mlanzi

KAMATI ya Uchaguzi ya Chama cha Waamuzi Tanzania (FRAT), imepanga kufanya Uchaguzi Mkuu Aprili 24, mwakani. Awali uchaguzi huo ulipangwa kufanyika mapema mwaka

21 November 2011

Mbunge aishukia CCM

 *Asema muswada waliopitisha unawagawa Watanzania
*Ahoji uhalali wa NEC kusimamia kura za maoni
*Askofu aonya wanaopotosha kuhusu mchakato huo


Na Mwandishi Wetu

SIKU chache baada ya Bunge kupitisha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba 2011, Mbunge wa Kigoma Kusini, Bw. David Kafulila (NCCR-Mageuzi), amesema
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete (kulia) akisalimiana na Mbunge wa Maswa Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bw. John Shibuda baada ya kuwasili mjini Dodoma juzi jioni kushiriki vikao vya Chama tawala. Wengine ni Makamu wake Bw. Pius Msekwa na katibu Mkuu Bw. Wilson Mukama.

Waumin wamkataa Askofu Anglikana

*Wamzuia kuingia kanisani kuongoza ibada

Na Jumbe Ismailly, Manyoni

SAKATA la waumini wa Kanisa la Anglikana Kilimatinde, Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida, kumkataa Askofu wa Dayosisi ya Rift Valley, John Lupaa, limechukua sura mpya

Vifo ajali ya basi Kagera vyaongezeka

Na Theonestina Juma, Bukoba

IDADI ya watu waliofariki katika ajali ya barabarani iliyohusisha basi la abiria na garila mizigo kwa kugongana uso kwa uso imeongezeka kutoka 16 hadi 18. Habari zilizopatikana
Nyumba zaidi ya 20 zilizoko eneo la Ukonga Mombasa zimebomoka na kusababisha baadhi ya wakazi wa eneo hilo kulala nje, baada ya mvua kubwa kunyesha Dar es Salaam juzi, kama inavyoonekana katika picha hii iliyopigwa jana.

Kamati Kuu CCM kuwang'oa vigogo leo?

Na Mwandishi Wetu

WAKATI vikao vya juu vya maamuzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), vikianza leo mjini Dodoma, chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete, hofu kubwa imetanda kuwa
Mtoto huyu alikutwa na kamera yetu akiosha vioo vya magari yaliyosimama kwenye foleni, eneo la Kamata, Barabara ya Nyerere, Dar es Salaam juzi.

Watimuliwa kufanya mitihani kwa kukosa ada

Na Salim Nyomolelo

ZAIDI ya wanafunzi 100 wa kidato cha kwanza na cha tatu katika Shule ya Sekondari Kwamkono wilayani Handeni mkoani Tanga wamezuiliwa kufanya mitihani yao ya mwisho wa mwaka kwa kushindwa kukamilisha michango mbalimbali ikiwemo ada.

Dkt. Kafumu awaonya watumishi wa Umma Igunga

Na Mwandishi Wetu, Igunga

MBUNGE wa Igunga Dkt. Peter Kafumu, (CCM), ametoa onyo kali kwa watumishi wa Halmashauli ya wilaya kuwajibika na kuwataka wenye tabia ya kula fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo kuacha mara moja kabla ya kufikiwa.

Mkazi wa nyanduga alilalamikia baraza la ardhi wilaya ya Tarime

 Na Timothy Itembe Tarime Mara

MKAZI wakijiji cha Nyanduga wilayani Rorya Mkoani Mara amelelemikia baraza la Ardhi na Nyumba la wilayani Tarime kuwa halikumtende haki katika shauri la kesi yake ya Ardhi No 117,2010 kuhusu kukaza rufaa

CCM yaanza kujipanga kunyakua Ilemela, Nyamagana

Na Moses Matthew, Mwanza

KAMATI ya Habari na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza, imekamilisha kazi ya kupata maoni mbalimbali kutoka kwa wananchi ngazi ya Kata kujua sababu zilizosababisha chama hicho kupoteza majimbo mawili ya Ilemela na Nyamagana katika uchaguzi Mkuu uliopita.

Wezi wa mifugo wadaiwa kuchoma nyumba ya Kamanda

Na Timothy Itembe Tarime Mara

MKAZI wa Kijiji cha Kwisarara wilayani Tarime, Mkoa wa Mara Bw. Machero Ghati, (33) amenusurika kufa baada ya mji wake kuteketezwa na mto na watu wanaoaminika kuwa ni wezi wa mifugo wanaokasirishwa na msimamo wake wa kupinga wizi huo.

Five Stars ziarani Kanda ya Kusini

Na Shufaa Lyimo

KUNDI la muziki wa taarabu la Five Stars, linatarajia kufanya ziara katika mikoa ya Kusini kuanzia Novemba 24 hadi 27, mwaka  huu kwa lengo la kutoa burudani kwa mashabiki wao.

Castle yatia mkono Ligi Kuu Uingereza

Na Victor Mkumbo

KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia yake ya Castle Lager, imedhamini kuonesha Ligi Kuu ya Uingereza (Barclays) kwenye vituo 48 vya televisheni barani Afrika.

Simba, JKT Oljoro hapatoshi robo fainali Uhai Cup

Na Zahoro Mlanzi

TIMU za JKT Oljoro na Simba, zitapambana leo asubuhi kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam katika robo fainali ya michuano ya Uhai Cup.

Wadau wataka Taifa Stars mpya

Na John Gagarini, Kibaha

WADAU wa soka nchini wameliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kuitumia michuano ya Chalenji kuchagua wachezaji wengine watakaounda kikosi cha timu ya taifa (Taifa Stars) ya baadaye.

18 November 2011

JK kuteta na wabunge wanachama wa TAPAC leo Dom

Na Godfrey Ismaely, Dodoma

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete, anatarajia kuwa
ngeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 10 ya Umoja wa
Wabunge wa Tanzania wa Kupambana na Ukimwi (TAPAC) utakaofanyika katika
ukumbi wa zamani wa bunge maarufu kama ukumbi wa Pius Msekwa leo.

Wafanyakazi mgodi wa Buzwagi walalamikia Polisi

Na Suleiman Abeid, Shinyanga

SAKATA la wafanyakazi wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani
Shinyanga kufungua jalada la kutukanwa na mmoja wa waajiri wa mgodi huo
polisi limechukua sura mpya baada walihusika kufungua jalada hilo kuanza kufukuzwa kazi.

Jaji Kiongozi ataja mafanikio sekta ya sheria

Na Salim Nyomolelo

WANANCHI wameombwa kujitokeza kwa wingi kupata huduma mbalimbali za kisheria na maelezo ya kina kuhusu maendeleo ya sekta hiyo katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam bila malipo.

Acheni kulinda makosa magari yanayomilikiwa na Polisi-DC

Na Esther Macha, Mbeya

MKUU wa Wilaya ya Mbeya Bw. Evance Balama, amemuagiza Kamanda wa Polisi na Mkuu wa usalama barabarani mkoani humo kuwathibiti na kuwachukulia hatua kali askari wanaodaiwa kuyalinda magari ya abiria yanayolalamikiwa na wananchi pindi yanapofanya makosa kwa maslahi yao binafisi.

Tumepiga hatua kubwa sekta ya afya- Wizara

Na Riziki lupatu

WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii imejitamba kuwa licha ya kuwepo kwa onhezeko kubwa la watu imepata mafanikio makubwa katika uboreshaji wa sekta ya afya nchini katika kipindicha miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara.

Yanga yapata ushindi wa kwanza

Na Shaban Mbegu

BAADA ya kuanza vibaya katika mashindano ya vijana ya Uhai Cup, timu vijana ya Yanga jana ilizinduka na kupata ushindi wa kwanza wa mabao 2-0 dhidi ya Polisi Dodoma.

Mabondia waachwa kwenye mataa

Na Amina Athumani

WASHIRIKI 30 wa kozi ya ukocha wa ngumi, ambayo ilipangwa kuanza jana mjini Kibaha wamejikuta wakiachwa kwenye mataa na kozi hiyo kuota mbawa, baada ya mkufunzi kutoka Aljeria kushindwa kutokea.

Papic aridhia Chuji kurudi Yanga

Na Mwandishi Wetu

KOCHA Mkuu wa Yanga, Kostadin Papic ameridhia kumrudisha kundini aliyekuwa kiungo wa timu hiyo, Athuman Idd 'Chuji' kwa ajili ya mashindano mbalimbali.

Boban, Mwaikimba waitwa Kili Stars

Na Zahoro Mlanzi

HATIMAYE yametimia! Ndivyo unavyoweza kusema kwa wachezaji Haruna Moshi 'Boban' na Gaudance Mwaikimba, baada ya kuitwa katika kikosi cha wachezaji 28 cha timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Chalenji itakayoanza kutimua vumbi Novemba 25, Dar es Salaam.

17 November 2011

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Sudan nchini Tanzania, Dkt. Yassir Mohamed Ali, alipofika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Muhidin Sufiani-OMR)

Al-shababab waitesa nchi

*Serikali yahadharisha wananchi
*Kenya wakamata Watanzania 10 
*Nahodha akerwa kauli za fujo

Na Reuben Kagaruki


SERIKALI imesema Tanzania inakabiliwa na tishio kubwa la kushambuliwa na kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab hivyo kuwataka wananchi kuchukua tahadhari pindi wanapoona watu wanaowatilia mashaka.

Tuko tayari kufa kutetea Watanzania-BAVICHA

Kamati Kuu CHADEMA yaota mbawa, sasa J.pili

Na Rehema Maigala

BARAZA la Vijana wa Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (BAVICHA) limesema lipo tayari kufa kwa kile wanachodai kwua ni kutetea haki ya mtanzania.
Mtuhumiwa wa wizi Bw. Saidi Dadi (18) mkazi wa Yombo kilakala, Manispaa ya Temeke aliyekamatwa akituhumiwa kuvamia Duka la dawa la Enol lililoko Mbande, Magengeni Dar es salaam na kuiba sh. 60,000 na kukimbia nzao, akiwa chini ya ulinzi wa polisi jana. (Picha na Mudhihir Mudhihir)

Waziri Kombani awaomba wananchi kupata huduma za sheria kuanzia leo

Na Godfrey Ismaely  Dodoma

WAZIRI wa Katiba na Sheria Bi. Celina Kombani, amewahimiza wananchi
kushiriki katika maadhimisho ya miaka 50 ya wizara hiyo yatakayoanza leo ili waweze kuwasilisha maoni yao na kero zinazowakabili kwa upande wa
sheria sambamba na huduma za usajili wa vizazi.

Wananchi walia na uzembe wa serikali mgomo wa daladala Dar

Na Benjamin Masese

MGOMO wa mabasi madogo ya abiria maarufu kama daladala yaendayo Kigogo Mburahati Kinondoni Dar es Salaam kushinikiza barabara hiyo kutengenezwa umeingia siku ya pili huku maelfu ya wananchi wa eneo hilo wakilaani vikali serikali kushindwa kuchukua hatua kurekebisha miundo mbinu hiyo.

Wana habari watatu wakadhidhiwa hundi za uchunguzi

Na Grace Ndossa

TAASISI ya utafiti ya utetezi wa haki za Aridhi imekabidhi hundi za sh. milioni tatu kwa waandishi wa habari watatu kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kina wa hali ya uwekezaji kwenye nishati mimea kwa lengo la kuibua masuala yaliyofichika na yanayoendelea kuathiri jamii.

Mkufunzi wa Algeria aikera BFT Na Amina Athumani

Na Amina Athumani
MKUFUNZI aliyeteuliwa kuendesha kozi ya ngumi nchini na Shirikisho la Ngumi la Ridhaa la Kimataifa (AIBA), Azzedin Aggoune kutoka Algeria amewakera viongozi wa Shirikisho la Ngumi za Ridha Tanzania (BFT), kutokana na kushindwa kufika kwa wakati.

Kaseja ampa tano nahodha Chad

Na Shufaa Lyimo

MLINDA mlango namba moja wa Simba na Taifa Stars, Juma Kaseja ameusifu uchezaji wa nahodha wa timu ya Chad, Mahamat Habib kutokana na jinsi anavyojua kupeleka mashambulizi langoni mwa wapinzani.

Timu ya taifa ya pool yaenda Malawi

Na Victor Mkumbo

KIKOSI cha timu ya taifa ya pool, kimeondoka jana kwenda nchini Malawi kushiriki katika mashindano ya All African Cup, yanayotarajiwa kuanza Novemba 22 hadi Novemba 26 mwaka huu.
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Dioniz Malinzi (kushoto) akikabidhi bendera ya taifa kwa timu ya taifa ya pool, ambayo imeondoka jana kwenda nchini Malawi kushiriki katika mashindano ya All Africa Cup, yanayotarajiwa kuanza Novemba 22 mwaka huu. (Picha na Victor Mkumbo)

Namba ya simu yatajwa kesi ya Mintanga

Rehema Mohamed

SHAHIDI wa tatu katika kesi kusafirisha dawa za kulevya Godfrey John, inayomkabili Rais wa zamani wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), Shaabani Mintanga ametaja namba ya simu ya mtu aliyekata tiketi za ndege za mabondia waliokwenda nchini Mauritius.

Kili Stars kufungua naRwanda chalenji

Na Zahoro Mlanzi

TIMU ya Taifa (Taifa Stars), imepangwa katika kundi linaloonekana kuwa gumu kuliko mengine kwa kukutanishwa na Ethiopia, Rwanda na Djbouti katika hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Chalenji, linalotarajiwa kuanza kutimua vumbi Novemba 25, mwaka huu, Dar es Salaam.

Tenga akiri Stars kucheza 'fyongo'

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amekiri timu ya taifa (Taifa Stars), kucheza chini ya kiwango katika mchezo dhidi ya Chad, licha ya kufuzu kucheza hatua ya awali ya makundi ya kuwania kucheza Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil.

16 November 2011

Chadema wateka Bunge

*Wabunge walia na Lissu, wahoji usomi wake
*Waionya serikali kutochukua hatua mapema
*Mnyika: Kikao cha Kamati Kuu kukutana kesho


Na Godfrey Ismaely, Dodoma

SIKU moja baada ya wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na NCCR-Mageuzi, kususia mjadala wa
Wanafunzi hawa ambao hawakufahamika madarasa na shule wanazosoma, walikutwa na kamera yetu wakigombea kunywa maji kwenye moja ya mabomba yaliyopo viwanja vya maonesho ya nane nane vilivyoko Msamala, Manispaa ya Songea jana.

Polisi Moro kashfa nzito

*Wadaiwa kuwalinda wauza mihadarati 

Na Lilian Justice, Morogoro

SIKU chache baada ya Kikosi Maalumu cha Kupambana na Ujambazi mkoani Morogoro 'Anti-Robery', kutuhumiwa kujihusisha
Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, wakisaidia kuliinua gari namba T 354 AGD Mitsubish Canter, lililogongwa na Daladala (halipo pichani) na kuanguka katikati ya Barabara ya Nyerere jana. Dereva wa gari hilo alijaeuhiwa vibaya.

Amuua mdogo wake kwa ahadi ya pikipiki

Na Esther Macha, Mbeya

MKAZI wa Kijiji cha Mpanda, Kata ya Nyimbili, Wilaya ya Mbozi, mkoani Mbeya, Bw. Iman Kalinga (22), anadaiwa kumuua mdogo wake
Muuzaji wa ndizi mbivu Bi. Georgista Mniuka, akiandaa ndizi zake kwa ajili ya kuuza kijiji cha Litola, wilayani Namtumbo jana. Biashara hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa mitaji na maeneo rasmi ya biashara.

Malindi yazidi kutupwa chini

Na Mwajuma Juma, Zanzibar

CHAMA cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), jana imetangaza kuishusha daraja la pili timu ya malindi kutokana na kupeleka masuala la

Kesi ya Prof. Mahalu kusikilizwa tena leo

Na Rehema Mohamed

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jana imeshindwa kuendelea kusikiliza kesi ya kuhujumu uchumi na kuipatia serikali hasara ya

Wasamaria jitokezeni kumsaidia Abdallay

Na Anneth Kagenda

Bw. Shaban Abdallay

KIJANA Shabani Abdallay (26) Mkazi wa Gongo la Mboto Mzambalauni amewaomba wafadhiri na viongozi mbalimbali kujitokeza

15 November 2011

Lema akubali dhamana

Imeandaliwa na  Pamela Malel,Quine Lema na Richard Konga

Asema wataandamana bila kibali cha polisi

HATIMAYE Mbunge wa Arusha mjini Bw. Godbless Lema, (CHADEMA) ameaga mahabusu baada ya kukaa kwa takriban siku 14 baada ya kukubali kuwekewa dhanama katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa mkoani huo jana.

Bungeni kwachafuka

CHADEMA wasusia muswada, watoka nje, Mbowe kutangaza msimamo wao leo, Makinda awajibu wanaharakati.

Wanafunzi waliokamatwa UDSM wafikishwa kortini

Rehema Maigala na Rehema Mohamed

WANAFUNZI 50 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliokatwa Ijumaa wiki iliyopita wakidaiwa kujihusisha na fujo mefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya ulinzi mkali kujibu mashitaka mawili yanayowakabili.

Tutabomoa nyumba zote maeneo yaliyovamiwa-CDA

Na Pendo Mtibuche, Dodoma

MAMLAKA ya Ustawishaji Makao Makuu Makao Makuu Dodoma (CDA) imesisitiza kuwa maeneo yote yameliyovamiwa na watu kinyume cha sheria hata kama ni kwa kushawishiwa na baadhi ya watu kuwadanganya kuwasaidia ni lazima yabomolewe.

Stars kazi moja leo

Na Zahoro Mlanzi

WAKATI timu ya taifa (Taifa Stars), ikishuka uwanjani leo kuumana na Chad katika mchezo wa kuwania kutinga hatua ya awali ya makundi ya kufuzu Kombe la Dunia, kocha wa timu hiyo, Jan Poulsen amesema lolote linaweza kutokea katika mchezo huo.

Esperance washangilia ubingwa wa Afrika TUNIS

Tunisia

MFUNGAJI wa bao la ushindi,  Harrison Afful ameimwagia sifa timu yake ya Esperance kwa kutwaa ubingwa wa Afrika, akisema kuwa, ndoto zake zimetimia.

14 November 2011

Moto wa Katiba Mpya kuwaka bungeni leo

 Na Salim Nyomolelo

*Wanaharakati: Kutachimbika kama utapitishwa
*Watishia kuhitisha maandamano nchi nzima
*Walemavu wauponda, wasema si rafiki
*Wabunge nao wajipanga kuonesha uzalendo

WAKATI Bunge la Tanzania linatarajia kupokea, kujadili na kupitisha muswada wa sheria ya jinsi ya kukusanya maoni ya Katiba Mpya, wanaharakati wanaojipambanua kama Jukwa la Katiba Jijini Dar es Salaam wamekuja juu na kutangaza kufanya maandamano ya nchi nzima iwapo itasomwa kwa mara ya pili kama ilivyopangwa na serikali.

Kamati ya Majadiliano imechangia kuharakisha maendeleo - Kombani

 na Godfrey Ismaely, Dodoma

SERIKALI imesema jitihada za kuishirikisha Kamati ya Majadiliano kabla ya kuweka saini mikataba mbalimbali ikiwemo ile inayohusu huduma za kijamii, zimechangia kuharakisha maendeleo.

MAONI YA KAFULILA KUHUSU MAMLAKA YA RAIS MCHAKATO WA KATIBA MPYA.

Jana wakati nachangia kwenye mjadala wa wabunge wote kuhusu namna ya kuenenda katika mjadala wa katiba nilijaribu kuweka msimamo wangu wa ujumla kuhusu misingi ya kufanya mjadala huu ufike salama na kufikia matokeo tunayotaka kama Taifa.

Taasisi za fedha zashauriwa kusaidia elimu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

TAASISI  za fedha nchini zimeshauriwa  kusaidia sekta ya elimu nchini kama njia ya kufikia maendeleo ya kweli.

Ushauri huo ulitolewa na Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam alipokua akipokea hundi kwa ajili ya upanuzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) mkoani Kagera.

Mchakato wa katiba mpya

Na Rachel Balama

MCHAKATO  wa uundaji wa katika mpya ni kiini macho kilichowekwa na serikali kwa nia ya kuwahadaa wananchi wakati serikali haina nia ya kufanya hivyo.

Kadharika serikali imetakiwa kuweka wazi kama kweli ina lengo la kuundwa kwa katiba mpya au kuifanyia marekebisho katiba ya sasa.

Nape atamba kuyavua magamba yaliyokwama

Na Rachel Balama

KATIBU wa Uenezi na Itikadi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Bw. Nape Nnauye, amesema kuwa viongozi wote wanaojitapa  kwamba magamba yao yapo kiunoni na hayawezi kuondolewa wanajidanganya,  yataondolewa kwa shoka kwenye kikao kijacho cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.

Ni vita mbeya

JWTZ, Polisi, wapambana na Machinga
*Wafunga mitaa, wachoma moto magari
*Chanzo Kandoro na sera ya safisha jiji 
 






 Na Esther Macha, Mbeya
JESHI la Polisi mkoani Mbeya jana lililazimika kutumia mabomu ya machozi  ili kuwatawanya  wafanyabishara ndogo ndogo maarufu kama (Machinga) kutokana  na kukaidi amri iliyotolewa na uongozi wa Jiji wa kuwataka kuondoka katika maeneo wasiyoruhusiwa kufanya biashara.