05 April 2013

Nape afichua siri za CHADEMA *Akanusha tuhuma dhidi ya CCM, Mwakyembe *Adai chama hicho sasa kinatumiwa na mafisadi



Na Gladness Mboma

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema tuhuma zinazotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), dhidi ya chama tawala ni matokeo ya chama hicho kulishwa uongo na
mafisadi wanaotaka kushika dola kwa gharama yoyote.

...waapa kumtoa Lwakatare *Ni maamuzi ya Halmashauri Kuu, Lissu 'afunguka'


Na Goodluck Hongo

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeapa kuhakikisha Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa chama hicho, Bw. Wilfred Lwakatare, ambaye anakabiliwa na kesi ya ugaidi,
anaachiwa huru wakidai kuwa, mashtaka dhidi yake hayana ukweli.

Mchungaji, Diwani wajisalimisha polisi vurugu za Tunduma



Na Rashid Mkwinda, Mbeya

DIWANI wa Kata ya Tunduma Bw. Frank Mwakajoka (CHADEMA), na Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), mjini Tunduma, mkoani Mbeya, Gidioni Mwamafupa, wamejisalimisha kwa Jeshi la Polisi mkoani humo
kutokana na vurugu kubwa zilizotokea jana mjini humo.

Askofu Lukosi mbaroni, akutwa K'njaro akihubiri


Na Florah Temba, Moshi

JESHI la Polisi mkoani Kilimanjaro, limemkamata Askofgu Romanus Lukosi wa Kanisa la Evangelist Assemblies Of God, lililiko Makambako, mkoani Njombe ambaye aliondoka nyumbani kwake Machi 22 mwaka huu, katika mazingira ya kutatanisha.

Jambazi akutwa na risasi 1,276 za SMG


Na Mwajabu Kigaza, Kigoma

JESHI la Polisi mkoani Kigoma, limemkamata mkazi wa Kijiji
cha Kitambuka, Kata ya Mnanila, Wilaya ya Buhingwe, mkoani
Kigoma Bw. Mwanzo Wilson (45), ambaye inadaiwa ni jambazi
sugu akiwa na risasi 1,276 za bunduki aina ya SMG alizozihifadhi katika dumu lenye mafuta ya Mawese akitaka kuzisafirisha.

Waziri Membe 'kupasua jipu' la mgogoro Ziwa Nyasa



Na Rose Itono

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Benard Membe, leo atazungumzia sababu za nchi ya Malawi kujiondoa katika mazungumzo ya mgogoro wa mpaka wa
Ziwa Nyasa na Tanzania.

M/kiti CCM kizimbani Dar kwa kujipatia milioni 500/-



Na Rehema Mohamed

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam, Bw. Ayub Chamshama (68), jana alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka matano likiwemo la kujipatia fedha sh. milioni 500 kwa njia ya udanganyifu.

Mbatia ahofia vita ya udini nchini *Shekhe ataka Wakristo, Waislamu kujadili mgogoro wa kuchinja


Darlin Said na Kassim Mahege

MWENYEKITI wa Kituo cha Demokrasia nchini (TCD), Bw.
James Mbatia, amesema Tanzania ipo hatarini kuingia kwenye
vita ya kidini kama hatua za haraka kudhibiti mifarakano ya
kiimani, inayotokea hazijachukuliwa.

Z'bar yatunga sheria kupinga ndoa ya jinsia moja


Na Mwajuma Juma, Zanzibar

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, tayari imeshatunga sheria
ya kukataza ndoa za jinsia moja na kuendelea kuitumia sheria ya adhabu ili kushughulikia masuala yote ya aina hiyo.

Stanbic yadaiwa fidia bil. 3/- kwa kufunga duka Kariakoo



Na Rehema Mohamed

BENKI ya Stanbic Dar es Salaam, imefunguliwa kesi ya madai na Kampuni ya Star Digital Technology & Pritways Limited na Oliver's Investment & Co (1993) Limited, katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ikidaiwa fidia ya sh. bilioni 3, baada ya kufunga duka la kampuni hiyo lililopo Mtaa wa Pemba na Sikukuu, Kariakoo.

VIBALI UKAAZI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano, Bi. Samia Suluhu Hassan (kulia), akipewa maelezo ya Vibali vya Ukaazi Zanzibar na Mkuu wa Kitengo cha kuzalishia hati za kusafiria
na Ukaazi, Bw. Haji Hamza (aliyekaa). Bi. Hassan jana alifanya  ziara ya kutembelea taasisi za Muungano ziliopo Zanzibar.
(Picha na Ali Meja)

Viongozi Fikisheni ushauri wa Dkt. Bilal kwa wananchi


MAKAMU wa Rais, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, juzi alifungua mkutano wa mwaka wa Utafiti ulioandaliwa na Taasisi ya Utafiti
wa Kuondoa Umaskini nchini (REPOA).

04 April 2013

TUCTA waibana serikali kima cha mshahara


Na Gladness Theonest

SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), kupitia Baraza Kuu la shirikisho hilo, limeitaka Serikali kuhakikisha ndani ya mwaka mmoja, wafanyakazi katika sekta zote wanalipwa kima cha mshahara kinachokidhi mahitaji yao na kama itashindwa, watashinikiza mgomo.

Lori lapinduka na kuua watatu Mto Wami


Na Masau Bwire, Bagamoyo

WATU watatu wamefariki dunia baada ya roli walilokuwa wakisafiria aina ya Nissan Dizel, lenye namba T 885 ACC,
kutoka Pangani, mkoani Tanga kwenda Dar es Salaam,
kupinduka na kutumbukia kwenye korongo lililopo
eneo la Mto Wami, Bagamoyo, mkoani Pwani.

Ujenzi wa vyoo shule ya Mengi waanza


Na Chrisina Mokimirya

UJENZI wa vyoo katika Shule ya Msingi Reginald Mengi, iliyopo Sinza, Dar es Salaam, umeaanza baada ya shule hiyo kukabiliwa na tatizo hilo kwa muda mrefu.

UVCCM: hatupo tayari kuandamana



Na Heckton Chuwa, Moshi

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), mkoani Kilimanjaro, umesema hautashiriki wala kufanya maandamano yoyote yasiyo na tija badala yake wataweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazowakabili ikiwemo ya ukosefu wa ajira.

Polisi wazima vurugu za CCM, CHADEMA



Na Bryceson Mathias, Mvomero

JESHI la Polisi Wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro, limefanikiwa kutuliza vurugu za uchaguzi wa kuwapata wajumbe
wa Mabaraza ya Katiba ngazi ya Wilaya, uliokuwa ukiratibiwa
na baadhi ya viongozi wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Serikali isikilize kilio cha Nkamia jimboni kwake


APRILI 2 mwaka huu, Mbunge wa Kondoa Kusini, mkoani Dodoma, Bw. Juma Nkamia (CCM), alizungumza na waandishi
wa habari ili kufikisha kilio chake serikalini juu ya tatizo la njaa ambalo linawakabili wapiga kura wake.

Wanaofanya ibada mbaya kwa JK waonywa


Na Mwandishi Wetu, Mbeya

VIONGOZI wa dizi zote nchini, wametakiwa kuacha mara moja kutoa matamko ya laana na kufanya ibada za kumuombea mabaya kiongozi wa nchi Rais Jakaya Kikwete, kwani kufanya hivyo ni kusababisha Taifa na Watanzania wote kupata laana na ndio
sababu ya kutokea majanga mengi siku hadi siku.

Uchunguzi kuporomoka ghorofa Dar, vifo 13 mgodini waendelea


Na Stella Aron

JESHI la Polisi nchini, linaendelea kufanya uchunguzi wa matukio ya kuanguka kwa ghorofa 16 katikati ya Jiji la Dar es Salaam na kuanguka kwa kifusi katika machimbo ya Moshono, mkoani
Arusha ili wahusika wahusika waweze kuchukuliwa hatua.

Afariki dunia kwa shoti ya umeme Dar



Na Miriam Sarakikya

MKAZI wa Mbagala Sabasaba, Dar es Salaam, Saidi Madafu (33) amefariki dunia baada ya kunaswa na umeme akiwa kazini.

Auawa kwa kisu akiwa muziki



Na John Gagarini, Kibaha

MFANYAKAZI wa baa ya Shimbikati, iliyopo Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, Hamis Kilongani (30), ameuawa
kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali (kisu), tumboni.

KATUNI


02 April 2013

Kikwete awataka Waislamu, Wakristo wabadilike


Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete amesema, kama viongozi na waumini wa dini ya Kikristo na Kiislamu hawatakubali kubadili muelekeo wao, nchi itaelekea kubaya na kupoteza sifa ya kuwa kisiwa chama amani.

Wafukuaji vifusi Dar waokota vichwa *Waliokufa sasa wafikia 34, wahusika wote mbaroni


Na Goodluck Hongo

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Meck Sadiki, amesema idadi ya watu waliokufa katika tukio la kuanguka kwa ghorofa 16 katikati ya jiji hilo, imefikia 34 pamoja na vichwa viwili ambavyo vimefukuliwa kwenye kifusi lakini havina viwiliwili.

Taarifa ya CCM yamliza Mkapa


Cornel Anthony na Hamisi Nasiri, Masasi

RAIS mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa, juzi alishindwa kujizuia na kutoa machozi baada ya kupokea ripoti
ya uharibifu uliofanywe katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Masasi, mkoani Mtwara.

Wanafunzi Bagamoyo walalamika kubakwa



Na John Gagarini, Bagamoyo

WATU wasiofahamika katika Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani, wanadaiwa kuanzisha mtandao wa kuwakamata wanafunzi wa kike, kuwabaka wanapokwenda shuleni au kurudi nyumbani.

NCCR-Mageuzi waandamana kutaka amani


Na  Patrick Mabula, Kahama

CHAMA cha NCCR-Mageuzi, Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, kimewataka viongozi wa madhehebu ya dini nchini, vyama vya siasa na Serikali kutumia hekima na madaraka yao
vizuri ili kuhakikisha amani na utulivu unaendelea kudumu.

MAANDAMANO


Katibu Habari na Uenezi Taifa wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Kitengo cha Vijana, Bw. Deogratias Kisandu (kushoto), akiongoza maadamano ya kusisitiza amani yaliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Kahama, mkoani Shinyanga na baadaye kufanya mkutano wa hadhara kwenye Viwanja vya CDT, uliokuwa na lengo la kuhubiri amani, upendo na mshikamano. Kulia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa chama hicho, Bw. Hemed Msabaha. (Picha na Patrick Mabula)

Padri asoma waraka wa onyo kwa serikali


Na Steven Augustino, Tunduru

JUKWAAA la Wakristo nchini (TCF), limesema kama Serikali itashindwa kuchukua hatua za kuwalinda wananchi wake, kanisa litachukua hatua ya kuwaeleza waumini wake kwa uwazi kuwa Serikali iliyopo madarakani inaibeba dini moja.

Kuanguka ghorofa neema kwa madereva


Na Mwandishi Wetu

KIFUSI cha ghorofa 16 ambalo lilidondoka mwishoni mwa wiki katika Mtaa wa Indira Ghandi, Barabara ya Bagamoyo, Dar es Salaam, kimekuwa biashara nzuri katika baadhi ya maeneo ya jiji hilo ambapo baadhi ya watu hukununua sh. 40,000 hadi 70,000 kwa roli
moja kutokana na ujazo wake.

KATUNI


Tukipuuza ya Lowassa, majengo mengi yataua na kuundwa tume



TUKIO la kuporomoka kwa jengo la ghorofa 16 jijini Dar es Salaam na kusababisha vifo vya watu 36, majeruhi 17, limeibua maswali mengi kwa wananchi wa kada mbalimbali.

Baadhi ya viongozi wa dini, nao hawakusita kuelezea hisia zao
juu ya uzembe wa baadhi ya watendaji waliopewa dhamana ya kukagua ubora wa majengo yaliyo kwenye ujenzi.

Askofu: Viongozi hawana uzalendo *Malasusa aibana serikali kuanguka kwa ghorofa Dar *Waumini watakiwa kudumisha amani, mshikamano



Na Waandishi Wetu

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt. Alex Malasusa, amesema tukio la kuporomoka ghorofa 16 mwishoni mwa wiki
Dar es Salaam ni matokeo ya usimamizi mbovu wa majengo.

JK atembelea wajeruhi wa kifusi


Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete, jana aliwatembelea majeruhi ambao waliangukiwa na kifusi cha ghorofa 16 ambalo liliporomoka
asubuhi ya Machi 26 mwaka huu, katiika Mtaa wa Indira
Ghandi, Dar es Salaam na kusababisha vifo vya watu 22.

Watoto 197 wazaliwa mkesha wa Pasaka Dar



Na Waandishi Wetu

WATOTO 197 wamezaliwa katika mkesha wa Sikukuu ya Pasaka, kwenye Hospitali ya Amana, Wilaya ya Ilala, Mnanyamala, Wilaya
ya Kinondoni pamoja na Temeke zote za Dar es Salaam.

Walimu,wanafunzi waishi kinyumba

Na John Gagarini, Bagamoyo

MWALIMU wa Shule ya Msingi Msoga, iliyopo Wilaya ya Bagmoyo, mkoani Pwani, Bw. Joel Mjema, anatuhumiwa
kumpa mimba mwanafunzi wa darasa la sita shuleni hapo
(jina tunalihifadhi) hivyo kushindwa kuendelea na
masomo baada ya kumaliza darasa la saba.

Wamaliza kufukua kifusi cha ghorofa 16


Na Peter Mwenda

KAZI ya ukoaji watu waliofunikwa na kifusi cha ghorofa 16, ambalo limeanguka mwishoni mwa wiki kwenye Mtaa wa Indira Ghandi, Barabara ya Morogoro, Dar es Salaam, imemalizika jana ambapo miili mitatu ilipatikana na kufikisha idadi ya watu 26 ambao wamepoteza maisha katika tukio hilo.

KATUNI


Ngawaiya kuwaburuza Diwani, Ofisa mtendaji mahakamani


Na Gladness Mboma

MDHAMINI wa Taasisi ya Maendeleo Tarafa ya Kibosho (KIDEFU)mkoani Kilimanjaro,Bw.Thomas Ngawaiya ametishia kuwafikisha mahakamani Diwani wa Kata ya Kirima,Bw.Paul Kileo na Ofisa Mtendaji Kata ya Kibosho, Bw.Gilbart Nyamsha kwa kutangaza kuuza mapipa ya lami yenye thamani ya shilingi bilioni 2.

Watu wawili wanaosadikiwa majambazi wauawa Lushotoa a

Na Yusuph Mussa, Lushoto

WATU wawili wanaosadikiwa ni majambazi wameuawa na wananchi wenye hasira kali baada
ya kuwatuhumu kufanya vitendo vya ujambazi na uporaji wa mali za wananchi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana (Mach.30) Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Tanga Bw. Constantine Masawe alisema tukio hilo limetokea juzi saa 12 asubuhi kwenye
kijiji cha Ubiri kata ya Ubiri wilayani Lushoto.

Bw. Masawe aliwataja marehemu hao kuwa ni Bw. Simon Mswaki (32) mkazi wa Kitongoji
cha Vuli, Kijiji cha Ubiri wilayani Lushoto na Bw. Godfrey Changoma (35) mkazi wa
Kijiji cha Mshangai, Kata ya Mazinde wilayani Korogwe.

"Watu hao inaaminika ni majambazi, na walikutwa na vitu vya wizi kama deki na vitu
vya kuvunjia nyumba. Wananchi waliamua kuchukua sheria mikononi na kuwaua papo
 hapo kwa kuwakatakata miili yao" alisema Bw. Masawe.

Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wa habari hizi mmoja wa mashuhuda Bw.
Henry Lazaro alisema watu hao wamekuwa wakiiba mali za watu kama vile mbuzi na
wakati mwingine kuvamia majumbani na kuwajeruhi watu kisha kuchukua luninga na vitu
vingine.

"Hawa watu waliouawa hivi karibuni wamemjeruhi kwa kumkata vidole Mwenyekiti wa CCM
Kata ya Ubiri Bw. Rajab Shehoza, ambapo ilibidi apelekwe KCMC Moshi, lakini wanapita
wakiiba mifugo na vitu vingine.

"Kwenye hilo tukio la kuuawa walikuwa watatu, lakini mmoja akakimbia na kumjeruhi
mtu mmoja, wenzake miili yao imekatwa vipande vipande hadi walipotaja mtandao wao wa
ujambazi, ndipo walipopasuliwa vichwa vipande vinne kwa shoka" alisema Bw. Lazaro.

Bw. Lazaro amewashauri polisi kama wanataka kufanikiwa kuwakamata majambazi
wasitumie ubabe kwa wananchi, na wanatakiwa kuwauliza kwa upole, kwani hasira za
wananchi wa maeneo hayo zimekuja
 baada ya ndugu zao kutiwa kashikashi wakati walikuwa hawahusiki na ujambazi.

Mamba aliyeua watu wawili auawa


Na. Jovither Kaijage,
Ukerewe  

MAMBA mmoja anayesadakiwa kuua watu wawili katika nyakati tofauti katika wilaya ya Ukerewe,Mwanza  ameuawa.

Kwamujibu wa taarifa toka eneo la tukio katika kijiji cha Muluseni kata ya Ngoma zinasema Mamba huyo mwenye uzito wa kilo 300 na urefu wa futi 18 aliuawa juzi baada ya kunashwa na mtego wa ndoano.

Jk atoa zawadi ya pasaka kwa yatima Dar



Na Darlin Said

RAIS Jakaya Kikwete ametoa zawadi ya Sikukuu ya Pasaka yenye thamani ya zaidi ya shilingi mil.5 kwa vikundi tisa vya kulea watoto yatima na waishio katika mazingira magumu jijini Dar es Salaam.

Zawadi hizo alizikabidhi Kamishna wa Idara ya Ustawi wa Jamii, Bw.Dunford Makala kwa niaba ya Rais Kikwete katika hafla fupi ya kukabidhi zawadi hizo iliyofanyika Dar es Salaam jana katika mahabusu ya watoto iliyopo Kisutu.

Wanafunzi 888 hawajaripoti shuleni



Na Suleiman Abeid,
Simiyu

ASILIMIA 48.4 ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza katika shule za sekondari wilayani Meatu mkoani Simiyu hawajaripoti katika shule hizo hadi kufikia katikati ya mwezi Machi mwaka huu.

Kaya 4,092 kujengewa vyoo vya kisasa


Na Mercy James,Njombe

HALMASHAURI ya Wilaya ya Njombe inatarajia kuendesha mpango wa kujenga vyoo bora
katika kaya zaidi ya 4,092 kwa kipindi cha miaka minne ikiwa ni kampeni ya kitaifa
ya kuzifikia kaya 100,000 ifikapo mw2aka 2015.

Akutwa chooni akiwa amejinyonga



Leah Daudi na Neema Malley

MWANAUME mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Baraka Iddi anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka (25-30) mkazi wa Mbweni amekutwa chooni amejinyonga kwa kutumia kamba.

Askari ajeruhiwa kwa panga


Na Prosper Mgimwa,
Sumbawanga

ASKARI wa Jeshi la Polisi mkoani Rukwa amelazwa katika hospital ya mkoa baada ya kujeruhiwa kwa panga wakati akimkamata mtuhumiwa.

Wananchi watumia mitishamba kujitibu


Na Joseph Mwambije,
Songea

KUTOKUWEPO kwa Zahanati na miundombinu mizuri ya barabara katika kijiji cha Magwamila ambacho kiko mpakani na nchi ya Msumbiji katika kata ya Muhukuru Songea vijijini mkoani Ruvuma kumewalazimisha wananchi kujitibu kwa kutumia mitishamba.

Watendaji wa serikali lawamani kwa rushwa


Na Florah Temba,
Moshi.

TATIZO la uharibifu wa mazingira katika Mkoa wa Kilimanjaro, limeelezewa kuendelea kushika kasi kutokana na baadhi ya watendaji wa serikali kujiingiza kwenye vitendo vya Rushwa na kuvifumbia macho vitendo vya uvunaji miti na upasuaji wa mbao.

Wananchi wamtimua mwe nyekiti wao wa kijiji


Na Thomas Kiani 
Singida

WANANCHI 3,700 WA Kijiji cha Mpugizi Kata ya Mwaru Wilayani Ikungi mkoani Singida kwa pamoja wamemtimua Mwenyekiti wa Kijiji na Mtendaji wake na kugoma kuendelea kutoa michango ya ujenzi wa Zahanati na choo cha shule ya msingi wakidai
viongozi hao kula fedha za michango vyanzo vya mapato. 

KIKOSI CHA YANGA

Kikosi cha Yanga kikiwa katika picha ya pamoja katika moja ya mechi za Ligi Kuu. Picha ya Maktaba

Polisi Moro waibania Yanga *Azam FC yainyuka Ruvu Shooting



Na Eliza Mayemba, Morogoro

VINARA wa Ligi Kuu ya Vodacom, Yanga jana walibanwa mbavu na Polisi Morogoro baada ya kulazimishwa suluhu katika mechi ya ligi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Simba, Toto Africans hakuna mbabe



Na Daud Magesa, Mwanza

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacm Simba, jana walitoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Toto Africans katika mechi ya ligi hiyo iliyochezwa Uwanjwa CCM Kirumba jijini hapa

Kikwete aongoza waombolzaji kumuaga Mbunge

Na Goodluck Hongo

RAIS Jakaya Kikwete jana aliwaongoza viongozi mbalimbali wa Serikali na Wabunge katika kuuwaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Chambani Pemba visiwani Zanzibar aliyefariki juzi katika hospitali ya Taifa Muhimbili.

Adaiwa kumbaka mjukuu wake hadi kumpa ujauzito



Na Abdallah Amiri,
Nzega

JESHI la Polisi wilayani Nzega mkoani Tabora Linamshikilia mkazi mmoja wa kijiji cha Mwamala
Haji Onjaonja (65) kwa tuhuma za kumbaka mjukuu wake
hadi kumsababishia ujauzito.

Mwanamke abakwa na kisha kunyongwa

Na  Prosper Mgimwa

Sumbawanga

MWANAMKE  mmoja  amefariki dunia baada  ya kubakwa na kunyongwa kisha mwili wake kuutelekeza njiani katika kijiji cha Kipabonde Ziwa Rukwa Wilayani
Sumbawanga mkoani Rukwa.

Malecela awarushia kombora CHADEMA



Na Mwandishi wetu,Singida

MJUMBE wa Baraza Kuu la Jumuia ya Wazazi Taifa, William Malecela amekionya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuwa kisitegemee ushindi wa “chee” katika uchaguzi mkuu ujao.

Wanaigeria wakuhukumiwa miaka mitatu


Na Rehema Mohamed

RAIA watatu wa Nigeria wamehukumia kifungo cha miaka mitatu jera na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu au kulipa faini ya sh.100,000 baada ya kupatikana na hatia ya kuingia nchini bila kibali.

Wawili wafariki dunia Dar


Na Leah Daudi

WATU wawili wamefariki dunia baada ya kugongwa na gari lenye namba T 855 ATB aina ya Scania ambalo lilikuwa likiendeshwa na dereva ambaye bado hajafahamika akitokea Ubungo kuelekea Buguruni Jijini Dar es salaam.

Watembea kilometa 10 kufuata matibabu


Na Martha Fataely,
Same

WAKAZI wa kata ya Mpinji wilayani Same, hulazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 10 huku wakiwa wamewabeba wagonjwa kwa kutumia machela na vitanda kuwapeleka hospitali ya jirani ya kata hiyo, kufuatia kata hiyo kukosa zahanati.

Waachieni watoto urithi wa elimu siyo mali-Bulembo


Na Mwandishi Wetu,Singida

WANANCHI wameaswa kuwaachia watoto wao urithi wa elimu badala ya mali ili waweze kukabiliana na changamoto za sasa za sayansi na teknolojia.

Nimefuraishwa na mshi kamano wa CCM,Serikali'

'
Na Mwandishi Wetu, Shinyanga

MWENYEKITI wa Jumuia ya Wazazi Taifa Abdallah Bulembo ameeleza kuridhishwa kwake na umoja, mshikamano uliopo baina ya CCM na serikali yake katika mikoa ya Shinyanga na Geita.

Kesi inayomkabili Mhasibu TRA kusikilizwa Aprili 2 mwaka huu


Na Rehema Mohamed

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Aprili 2 mwaka huu inatarajiwa kuanza kusikiliza utetezi wa kesi ya kutakatisha fedha inayomkabli aliyekuwa mhasimbu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Bw.Justice Katiti.

Madeva 5000 ukosa ajira kila mwaka kwa ukosefu wa viwango



Na Veronica Ikonga

MUUNGANO wa madereva wa malori na mabasi Tanzania (TDACCT) wamesema zaidi ya madeva 5000 wanakosa ajira kutokana na kukosa viwango vinavyostahili.

Walimu wadaiwa kuacha kukimbilia biashara zaidi




Na Timothy Itembe Tarime.

SERIKALI imetakiwa kukemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya walimu kutoa ajira juu ya ajira kwa kuwapa rushwa walimu wenzao ili kuwasaidia vipindi vyao darasani na wao kusafiri kwenda kufanya shughuli zao za kibiashara.

Madereva pikipiki 85 wapatiwa semina elekezi



Na Abdallah Amiri,
Igunga.

JESHI la Polisi wilaya ya Igunga mkoani Tabora limewapatia semina elekezi madereva pikipiki na bajaji zaidi ya 85 juu ya taratibu na matumizi ya vyombo vya usafiri.

Serikali imeombwa kuwanusuru Wabarabaig

Na Martha Fataely,Moshi.

SERIKALI imeombwa kutafakari vyema mpango wake wa kuwahamisha wafugaji
wa asili ya Kibarabaig wanaoishi msitu wa pongwe wilayani Pangani
mkoani Tanga kwa kuwatengea maeneo maalum ya kuishi kabla ya kuwaondoa
maeneo hayo.

Milioni 30 kutumika kuje nga mazalia ya samaki


Na Mwajuma Juma,
Zanzibar

JUMLA ya shilingi milioni 30 zinatarajiwa kutumika kwa ajili ya kutengeneza Matumbawe (mazalia ya samaki ya kienyeji) katika ghuba ya chwaka huko kijiji cha Marumbi wilaya ya kati Unguja.

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi, Bw. Mussa Aboud Jumbe amesema kuwa wameamua kutengeneza Matumbawe hayo na kuyatupa katika bahari hiyo kutokana na kuwepo kwa uharibifu mkubwa unaosababishwa na uvuvi haramu ambao umesababisha kupungua kwa samaki katika vijiji hivyo.

Hata hivyo alisema kuwa mpango huo utawezesha kupunguza mgogoro uliopo baina ya vijiji viwili hiyvo kati ya Chwaka na Marumbi katika suala zima la
upatikanaji wa samaki,kutokana na kuwa kutakuwa na samaki wa kutosha ndani ya eneo hilo.

“Eneo la marumbi ni sehemu moja wapo lililoharibiwa na wavuvi wanaotumia uvuvi haramu ,hali iliosababisha ukame wa upatikanaji samaki katika kijiji hicho na hata vijiji jirani, hivyo hatua hii itaweza kusaidia kuondosha
upungufu huo”, alisema.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa kuwa kutoka na  athari kubwa iliojitokeza wameamua kuendesha mrdi huo kwa majaribio ambao unalengo la kuengeza nyumba za samaki pamoja na kuongeza kiwango cha uzalishaji wa samaki katika eneo
hilo.

Alisema kuwa mbali na malengo hayo pia faida yake kubwa ni kuweza kudhibiti uvuvi haramu katika maeneo hayo.Sambamba na hilo amesema kuwa kuna haja ya Serikali kuangalia uwezekano wa kuongeza fedha zaidi ili kuweza kuwanusuru wavuvi wa Zanzibar.

Kwa upande wao wenyeviti wa kamati za uvuvi kutoka vijiji vya uroa,pongwe na Chwaka walisema kuwa wakati zoezi hilo likiendelea tayari mafanikio
yameanza kujitokeza baada ya kuona samaki wageni wakiingia katika matumbawe
hayo.




Wakristo waondolewe hofu la usalama wao kanisani kwa vitendo


LEO Wakristo wote duniani, wanaadhimisha kifo cha
Yesu Kristo aliyeteswa msalabani mjini Yerusalemu.

Siku ya leo ni mwanzo wa Sikukuu ya Pasaka ambayo Yesu
Kristo alifufuka maada ya mateso yaliyosababisha kifo chake msalabani ambapo Wakristo huitumia siku hiyo kushangilia
ushindi wa kufufuka kwake na ukombozi wao.

Katibu aliyefukuzwa CCM arudishwa kundini


Na Suleiman Abeid, Shinyanga

HATIMAYE Katibu wa Siasa na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Shinyanga Mjini, Bw. Charles Shigino, aliyekuwa amesimamishwa uongozi, amerejeshwa katika nafasi yake.

Mhasibu OUT kortini kwa kutakatisha mil. 578/-


Na Rehema Mohamed

MHASIBU wa Chuo Kikuu Huria nchini (OUT), Bw. Engels Mrikaria (42), jana alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, akikabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kutakatisha fedha zaidi ya sh. milioni 578.

Jukwaa la afya EAC lazinduliwa mjini Kigali



Na James Gashumba, EANA

JUKWAA la Afya Afrika Mashariki (EAHP), limezinduliwa juzi mjini Kigali, nchini Rwanda ambapo Serikali za nchi wanachama, zimetakiwa kushirikiana na jukwaa hilo kwa manufaa ya jamii.

Darala Mto Kirurumu lakatika, abiria wakwama



Na Sophia Fundi, Karatu

IDADI kubwa ya abiria waliokuwa wakitokea Serengeti na Ngorongoro wengi wao wakiwa watalii, jana walishindwa
kuendelea na safari baada ya Daraja la Mto Kirurumu kukatika.