Na Prosper Mgimwa
Sumbawanga
MWANAMKE mmoja amefariki dunia baada ya kubakwa na kunyongwa kisha mwili wake kuutelekeza njiani katika kijiji cha Kipabonde Ziwa Rukwa Wilayani
Sumbawanga mkoani Rukwa.
Tukio hilo lilitokea usiku wa Machi 24 mwaka huu, ambapo Kamanda wa polisi Jacob Mwaruanda alisema watu waliofanya tukio hilo walimbaka kwanza kisha kumnyonga shingo .
Mwaruanda alisema kuwa bado Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi na pindi utakapokamilika na kuwakamata watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili za mauaji.
Na katika tukio jingine watoto wawili wamenusurika kifo baada ya nyumba waliyokuwa wamelala kushika moto ulioshababishwa na kibatari katika kijiji
cha Singiwe kata ya Matai Wilayani kalambo Mkoani Rukwa.
Kamanda wa polisi Mkoani Rukwa Jacob Mwaruanda alisema kuwa watoto hao
walijeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao na kufikishwa kwenye kituo cha
afya kwa matibabu.
Aliwataja watoto hao kuwa ni Gabinus Nkanga(12) na Maria Nkanga(8) wote ni
familia moja ambapo hasara iliyopatikana ni zaidi ya milioni tano
inadaiwa kuwa nyumba hiyo ilikuwa na chumba cha duka.
Hata hivyo kamanda wa polisi mkoani Rukwa amewataka wananchi kuwa
makini nyakati
za usiki na vibatari hasa kwa watoto ili kuondokana na suala la janga moto.
No comments:
Post a Comment