31 May 2013

Dereva wa pikipiki ya kubeba abiria 'Bodaboda' 'akiuchapa' usingizi baada ya kukosa abiria kwa muda mrefu, kama alivyokutwa Mtaa wa Samora Posta Dar es Salaam jana. Kuendesha vyombo vya moto bila kupumzika husababisha uchomvi ambao huchangia kutokea kwa ajali. (Picha na Charles Lucas)
Baadhi ya wakazi wa jiji wakimuangalia mtu ambaye hakufahamika jina aliyekuwa akitafuta kiatu kilichotumbukia katika mfereji wa majitaka, kama alivyokutwa Ubungo, Dar es Salaam juzi. (Picha na Prona Mumwi)

Meneja wa Vodacom Tanzania Mkoa wa Kigoma, Bw. Kasinde Umella, akisalimiana
na Baba wa mshindi wa sh. Milioni 100, katika 'Promosheni ya Vodacom
Mahela', Bw. Nicodemus Nalisis (kushoto), alipofika uwanja wa ndege kumlaki mtoto wake
Bw. Valerian Kamugisha (katikati) alipowasili Kigoma kutoka Dar es Salaam alikokabidhiwa 'kitita' hicho juzi. (Na Mpigapicha Wetu)



Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo Pichani) Dar es Salaam jana, wakati akitangaza matokeo mapya ya mtihani wa Kidato cha Nne (CSSEE) uliofanyika Oktoba mwaka jana. Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) Profesa Rwekaza Mkandara. (Picha na Prona Mumwi)

Minazi, karafuu yahamia Wizara ya Kilimo

Na Mwajuma Juma,  
 MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali amesema kuwa kuanzia sasa mashamba yote ya karafuu na minazi yaliyokuwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Ardhi, Makazi, Maji na Nishati yatakuwa yakishughulikiwa na Wizara ya Kilimo na Maliasili, ili kuondoa mvutano wa kiutendaji baina ya wizara hizo mbili.
Balozi Seif alitoa uamuzi huo katika Chuo cha Amali vitongoji Chake Chake Pemba wakati akizungumza na masheha wa mikoa miwili ya kisiwani Pemba.
Alisema udhibiti wa mapato yanayotokana na mazao yaliyomo kwenye baadhi ya mashamba ya Serikali yalikuwa yakileta mgongano kutokana na mashamba hayo kushughulikiwa na Wizara mbili tofauti.
Hivyo aliwaomba Masheha ambao maeneo yao yamo mashamba ya

Wazazi Masasi wahimizwa kupeleka watoto shule

Na Said Hauni, Lindi


 WA Z A Z I Wi l a y a y a Masasi mkoani Mtwara wamesisitizwa kuwapeleka watoto wao shule ili waweze kupata haki zao za msingi katika kupata elimu itakayoweza kuwasaidia kuendesha maisha yao ya sasa na ya baadaye
Rai hiyo ilitolewa na Kaimu Ofisa Elimu shule za msingi wilayani humo, Said Nanjayo, alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Walemavu wa ugonjwa wa Ukoma katika kijiji cha Mkaseka, Jimbo la Lulindi, wakati wa uzinduzi wa jengo la darasa moja la awali lenye thamani ya sh.milioni 9.
Akizungumza baada ya ufunguzi wa darasa hilo, Nanjoyo alisema ni vema wazazi walio na watoto walio na umri wa kuanza masomo ya awali kuwapeleka mara moja kwenye shule hiyo ili waweze kuanza kupata elimu itakayowawezesha kuingia darasa la kwanza kwenye shule ya

Waziri ataja mbinu za kumaliza migogoro


Na Mwa j uma J uma ,
Zanzibar


 WAZIRI wa Katiba na Sheria, Abubakar Khamis Bakar, amesema kuwa katika kutafuta amani na utulivu ni lazima pawepo na msimamo wa pamoja ili kuweza kufanikiwa kumaliza tofauti.
Waziri huyo aliyaeleza hayo katika uzinduzi wa kitabu cha Mizozo na namna ya kuitambua na kuitatua kisha kuichambua mizozo ya Zanzibar hafla iliyofanyika mjini Unguja.
Alisema kuwa katika kufikisha suala hilo pamoja na kuwepo na msimamo lakini hekima na busara itumike ili kufikia lengo la kupatikana kwake.
Hata hivyo alisema kuwa si njia sahihi ya kufikiria kuwa njia pekee ya kumaliza tofauti baina ya pande mbili ni kumshinda unaepambana nae bali ni kumshawishi ili akubaliane na mtazamo pamoja na unayoyasema.
Aidha, alisema kuwa kwa vyovyote vile kiini cha migogoro huwa ni

'Majambazi' wasomewa mashtaka hospitalini

Na Said Hauni, Lindi


 WAKAZI wawili katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi,wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na shtaka la kujihusisha na masuala ya ujambazi kwa kutumia silaha mbalimbali ikiwemo bunduki ya kienyeji na kufanikiwa kupora bidhaa na fedha taslimu jumla ya sh milioni 1.2.
Washtakiwa hao ambao kesi yao ipo kwa Hakimu Aluu Nzowa wa Mahakama ya wilaya hiyo ni, Hamisi Athumani Mbuhi na Rajabu Juma Ndete wote ni wakazi wa mtaa wa Kongo mjini Lindi na wamelazwa hospitali ya mkoa huo Sokoine.
Akiwasomea shtaka lao katika wodi namba sita walikokuwa wamelazwa Mwanasheria wa
 Serikali, Juma Maige alidai Mei 20 mwaka huu usiku washtakiwa wote kwa pamoja walifika dukani kwa Hamisi Hassani Bakari lililopo Kijiji cha Mkwajuni Wilaya ya Lindi na

Mtatiro kuzindua kampeni udiwani Muheza

Na Mwandishi Wetu, Muheza


 NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF),Julius Mtatiro anatarajiwa kuzindua kampeni za udiwani katika Kata za Genge na Tingeni zilizoko wilayani Muheza Mkoa wa Tanga.
Mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi CUF Taifa, Nuru Awadh Bafadhili alisema jana kuwa uzinduzi huo utafanyika siku mbili ambapo katika Kata ya Genge utafanyika kesho na Kata ya Tingeni itakuwa Juni 2.
Alisema mapokezi ya Naibu Katibu Mkuu huyo yatafanyika katika Kijiji cha Kerenge Kata ya Tingeni na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kumlaki kiongozi huyo.
Wakati huo huo,Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Muheza mkoani

Viongozi Newala wafurahishwa na vikundi vya wakulima



 USHIRIKIANO na mwamko wa wakulima walioungana katika vikundi kutekeleza mradi wa Mpango wa Maendeleo vijijini; katika mwambao wa Pwani ya Tanzania (CRSPT); unaotekelezwa na Aga Khan Foundation, katika Wilaya ya Newala, umewafurahisha, viongozi katika kata ya Mcholi ya kwanza, walioshiriki siku ya wakulima kijijini, Chiunjila, anaripoti Godwin Msalichuma, Newala.
Hayo yalijitokeza kijijini hapo hivi karibuni, ambapo diwani Selemani Kaisi, alipopewa fursa ya kuzungumza na vikundi vya wakulima takribani 87, wanaume 61 na wanawake 26, walikusanyika katika siku yao, ili kujifunza pamoja mambo muhimu na changamoto zinazowakumba katika mradi huo wa kilimo cha mpunga na ufuta.
“Nimeridhishwa sana na utekelezaji wenu wa mradi huu kwa ushirikiano na kwa kweli unanitia moyo kuona haya yakifanyika kwa umoja na nguvu ya pamoja, niseme kuwa mmeshakuwa wataalamu sasa, ninaimani mnaweza kuendelea hata bila ya wafadhili kuwepo” alisema Kaisi na

Kigoma watakiwa kuchangamkia promosheni Vodacom

Na Mwandishi Wetu, Kigoma


 MZAZI wa kija naaliy eshindash.milio ni10 0katika promosheniya VodacomMahela, Bw .Nicodemus Nalisis am etoawit okwawa kaziw a Mkoaw aKigo mak ujen gatabia yakushiriki mash in danomba lim bali yanayotolewanakamp unizasimuza mkononi hapanchini.
Bw.Nicodemus alisemahayo juzi mkoaniKi gomaw akat ialipowasili kumpok eakijana wakeB w.ValerianKamugish aaliyewasilimkoani hapa marab aada ya kuka bidhiwakiasi chash .mi lioni10 0m wanzoni mwawik ihiibaad ay akuibukamshindiwashindanoh ilo .
Alisem a k uwa hatua yakushiriki ma shindanoha yoyatatoa fursayaushindi k wawa nanchiwengi mkoani Kigoma hivyo kuongeza uwezekano wa mkoa wa Kigoma kutoa washindi wengi katika mashindano yanayoendeshwa na Vodacom na kubadilisha maisha yao ya kiuchumi na

Wanaoita wenzao mafisadi wamkera Pinda

Na Elizabeth Joseph, Dodoma




WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amewatahadharisha watu wanaopenda kuwaita wenzao mafisadi pindi wanapowaona wamepata mafanikio kwa kuwa na yeye anatarajia kunufaika na ufugaji wa nyuki.
Alisema hivi karibuni anatarajia kuvuna asali karibu tani moja na mara akianza kuiuza lazima apate faida kutokana na asali hiyo, hivyo Watanzania wenye dhana ya ufisadi kwa wanaopata faida au maendeleo katika shughuli za kujiinua kiuchumi waache tabia hiyo.
Pinda alibainisha hayo juzi mjini hapa wakati akifungua semina ya wakuu wa mikoa na wilaya nchini iliyohusu utoaji wa pembejeo za ruzuku kwa wakulima.
Aliwataka wakuu hao kutafuta njia ya kuwasaidia wafugaji nchini kwa

Dawa bandia kugundulika kwa kutumia simu

Na Rachel Balama


 KAMPUNIzakuten genezadawa za b ina damunchini zimetak i wakutumia teknolojiampya ijulikanayo“hakikisha d awa156 29 ”iliyoanzishwan akampu ni yadawa yaG laxoSmithKline ili kudhibiti da w abandia.
Mwit ohu ou litolew a Dar es Salaamja nan aNaibuWaziriwaAfyanaUstawiwaJamii , Dkt.Seif Rashi d, wakati a kiz induaprogramuyamtanda owah a kikisha dawahal isi kwaku tum aujumbemfupi wamaneno kwen da1 5629 .
A lisemak uwanjia hiyoitasaidia kudhibitida waba ndiakw ak uwa changamo tokub wailiyo pokw asasaniuwepo wadaw a band iapamoja na watukuu zadawazi sizofaakutibumago njwa.
Alis emaSerikali itajitahidi kufanyauhakik iilikuhakikisha

Mtoaji taarifa za uwongo kwa IGP, Waziri ahukumiwa

Na Rehema Mohamed


 Mohamed (25), amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela au faini ya sh. milioni tatu baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka matatu.
Mashtaka hayo ni kutoa taarifa za uongo katika mitandao ya simu za mkononi na kutuma ujumbe wa maudhi kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Said Mwema.
Mshtakiwa huyo alisomewa hukumu hiyo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam na Hakimu Hellen Liwa ambapo upande wa mashtaka uliwakilishwa na wakili Bw. Ladslaus Komanya.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Liwa alisema hayo ni makosa mapya yaliyo katika Sheria Mpya ya Mawasiliano na Mitandao.
“Kwa kitendo ulichokifanya kuwatumia ujumbe viongozi wa juu wa

Ufaulu IV-2012 waongezeka

Grace Ndossa na Goodluck Hongo


 KIWANGO cha ufaulu kwa wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka 2012, kimeongezeka kwa asilimia 43.8 tofauti na yale yaliyotangazwa awali ambayo ni asilimia 34.5.
Matokeo hayo yametangazwa Dar es Salaam jana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa ambaye alisema kuwa, kati ya wanafunzi 397,138, waliofaulu ni 159,609.
Kati ya wanafunzi hao, wavulana 98,858, wasichana ni 60,751, sawa na asilimia 43.8 tofauti na matokeo ya awali.
Alisema waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni 35,349 ambapo kati yao, wavulana ni 24,425, wasichana ni 10,924, sawa na asilimia 9.55. Waliopata daraja la

Uandishi umechangia mateso ya Kibanda-Kamati


Mashaka Mhando na Rachel
Balama


 TUKIO la kuteswa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), ambaye anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini, limechangiwa na kazi yake ya uandishi wa habari likihusisha vyombo vya dola na vyama vya siasa.
Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya uchunguzi wa tukio hilo, Bw. Deodatus Balile, aliyasema hayo mjini Tanga jana wakati akiwasilisha ripoti ya uchunguzi uliofanywa na watu watano.
Alisema kamati hiyo imebaini halina uhusiano wowote na masuala ya rushwa au mapenzi bali ni mpango maalumu ambao uliandaliwa na baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola wasio waaminifu ili kutekeleza matakwa ya kisiasa.
“Kamati imebaini kuna kutupiana mpira kati ya vyombo vya dola na vyama vya siasa katika kuandaa mpango wa kuteswa kwa Bw. Kibanda hatua ambayo uchunguzi huo umebaini kuwepo kwa sababu ya kutokea tukio hili,” alisema Bw. Balile.
Katika taarifa hiyo yenye kurasa 10 ambayo aliwasilishwa kwenye

Wenje, CUF ngoma nzito


*HOTUBA YAKE YALETA UTATA KWA WABUNGE CUF
*AKATAA KUOMBA RADHI, ASEMA KADHALILISHWA
*KAMATI KUMJADILI, NDUGAI AAHIRISHA BUNGE
Na Waandishi Wetu


 KWA mara nyingine, Naibu Spika wa Bunge, Bw. Job Ndugai, jana amelazimika kuahirisha kikao baada ya wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), kupinga baadhi ya maneno yaliyopo katika hotuba ya Kambi ya Upinzani.
Hotuba hiyo ilisomwa bungeni mjini Dodoma na Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Ezekiel Wenje, ambaye ni Mbunge wa Nyamagana, Mwanza.
Wakati Bw. Wenje akiendelea kusoma hotuba hiyo, mbunge wa Jimbo la Mtambile, Bw. Masoud Salim (CUF), Zanzibar, alisimama na kuomba mwongozo wa spika na kutaka hotuba hiyo isitishwe akidai imejaa uzushi, uwongo na ushenzi.
Katika hotuba yake, Bw. Wenje alisema Chama cha CUF itikadi zake ni

Filikunjombe: Nina imani na uongozi CCM

Na Mwandishi Wetu, Ludewa


 MBUNGE waLu dewa, mkoaniNjombe, Bw. D eoFilikunjombe, ameipo nge za safumpyawaChamaChaMapindu zi (CC M), kwakazi kub wa wanayo endeleakuif anyailikukijengachama hichokuanzia ngazi ya shina hadi T aifa.
Bw .Filikunjomb eali yasemahayom jini humoja nawakati akihutub iawananc hikwenyemkutanowa hadharauli ofanyika katikaKatayaLupinguna kuonge za kuw a, y eyote mwe nyendotoyakushi ndanana CCM anapot eza mudawake.
“KatibuMkuu wa chamach etu, Bw. Abdu lrahmanKinan a,pianinai manik ub wanaKatibu wa NEC ,Itikad inaUen ez i, Bw. NapeNnauye,k azi wanayoifanyayakupigani awanyonge inaone sha kiwan gocha uzalendo walichnachohiv yot uwaungem kono.
 “Kasi ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010/2015, kusimamia

Kova, Kamuhanda wapanda vyeo

Na Mosi Mrisho


 RAIS Jakaya Kikwete, amewapandisha vyeo baadhi ya maofisa wa polisi akiwemo Kamanda wa Polisi mkoani Iringa, Michael Kamuhanda, kuwa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, uteuzi ambao unaanza mara moja.
Katika uteuzi huo, Kamanda Kova na Isaya Mngulu, wote wamekuwa Makamishna wa Polisi (CP).
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Wizara ya Mambo ya Ndani ya

30 May 2013


Baadhi ya wakazi wa jiji wakiangalia pikipiki zilizohifadhiwa nje ya Kituo cha Polisi Buguruni, Dar es Salaam jana. Pikipiki hizo zilikamatwa kwa makosa mbalimbali katika msako unaofanywa na jeshi hilo. (Picha na Charles Lucas)

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (HLRC), Bw. Harold Sungusia (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam jana, wakati akitoa tamko kwa vyombo vya habari kuhusu vurugu zilizotokea mkoani Mtwara hivi karibuni. Katikati ni Mkurugenzi wa Uwezeshaji na Uwajibikaji, Bi. Imelda Urio na Ofisa Usalama Mtandao wa Watetezi Bw. Benedict Ishabakaki. (Picha na Prona Mumwi)

PPF yatumia mil. 680/- kusomesha wanafunzi

Na Mashaka Mhando, Tanga


 MFUKO wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF) unaoshiriki kwa mara ya kwanza Maonesho ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika Jijini Tanga, hadi kufikia Desemba mwaka jana, umetumia kiasi cha shilingi milioni 682.9 kusomesha wanafunzi wapatao 1,333 nchini.
Akizungumza na gazeti hili, katika mahojiano maalumu Ofisa Uhusiano wa mfuko huo, Janet Ezekiel, alisema kuwa fedha hizo wamezitumia kusomesha wanafunzi hao kupitia fao la elimu ambalo wanasaidia kuboresha na kusaidia suala la elimu kwa wanachama wake.
Ofisa Uhusiano huyo, alisema mbali ya fao hilo la elimu pia mfuko huo hadi kufikia Machi 31 mwaka huu tayari walikuwa na jumla ya wanachama wapatao 219,000 uliosababisha mfuko huo

Balozi Seif awafunda wakulima wa karafuu


Na Mwajuma Juma,
Zanzibar


 WAKUL IMA wa mashamba ya karafuu w ame s h a u r i w a kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalamu wa kilimo hicho ili kujenga nguvu za uzalishaji wa uhakika wa zao la karafuu nchini.
Ushauri huo ulitolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi wakati wa ziara yake ya kukagua baadhi ya mashamba ya Serikali ya miti ya mikarafuu ambayo yako chini ya usimamizi wa baadhi ya wakulima ndani ya Mkoa wa Kusini Pemba.
Alisema kumejengeka dhana kwa baadhi ya wakulima wa mikarafuu kujilimbikizia miti mingi ya zao hilo wakiwa na fikra za kupata uzalishaji mkubwa zaidi jambo ambalo ni

Baadhi ya wapitanjia wakiangalia gari lenye namba T 201 BEQ, lililopata ajali eneo la Ubungo, Dar es Salaam jana. Dereva gari hilo alishindwa kulidhibiti wakati akikimbia baada ya kugonga pikipiki kwenye makutano ya Barabara za Sam Nujoma na Barabara ya Morogoro. (Picha na Prona Mumwi)

Serikali iangalie upya mfumo ukopeshaji wakulima’

Na Elizabeth Joseph, Dodoma


 WADAU wa kilimo nchini wameitaka Serikali kuuangalia upya mfumo w a k u w a k o p e s h a wakulima pembejeo za kilimo.
Pia wameitaka kuangalia mfumo wa kuwakopesha wakulima kwa kupitia taasisi za kifedha ili ulete manufaa kwa wakulima wadogo nchini.
Hayo yalibainishwa juzi mjini Dodoma na wadau hao katika semina kwa wakuu wa mikoa na wilaya nchini iliyolenga kuutambulisha mfumo mpya wa kuwakopesha wakulima ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa kupitia benki na kuongeza kuwa mfumo huo unaweza kumfanya mkulima mdogo ambaye ndiye mlengwa akashindwa kukopeshwa kutokana na urasimu uliopo katika taasisi hizo za kifedha.
Pia walisema kuwa wakulima wakubwa ndio mara zote wamekuwa wakitumia taasisi hizo kukopa fedha kwa ajili ya kilimo chao hivyo wasije wakajinufaisha wao binafsi kupitia mfumo

Lissu awafunda wanawake CHADEMA

Na Elizabeth Joseph, Dodoma


 WANAWAKE nchini wametakiwa kutobweteka na kuchangamkia fursa mbalimbali katika kuwania nafasi za uongozi ili kuingia kwa vitendo katika ngazi mbalimbali za maamuzi.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA) uliofanyika mkoani humo.
Alisema kuwa wanawake katika chama hicho hawatakiwi kubweteka kwa lengo la kusubiri kupewa nafasi za upendeleo za uongozi na hivyo wanapaswa kuzigombania kama wanavyofanya wanaume.
Mafunzo hayo ambayo yanawashirikisha viongozi wa Bawacha kutoka katika

Maambukizi ya Ukimwi yaongezeka maradufu


Na Florah Temba, Same


 WANACHAMA w a Vikundi vya Kuweka na Kukopa (VICOBA) wamekabidhiwa simu za mkononi bure,ili waweze kuweka fedha zao kwa njia ya kisasa na kuachana na mtindo wa utunzaji fedha kwa njia ya masanduku.
Hatua hiyo ya kuwakabidhi simu hizo ilizinduliwa Dar es Salaam jana na Makamu wa kwanza wa Rais wa Vicoba Taifa Scholastica Kevela.
Akizindua kampeni hiyo kwa wana Vicoba, Bi. Kevela alisema hatua hiyo itasaidia kupunguza taarifa za upotevu wa fedha na kuwarahisishia uwekaji wa fedha katika mazingira mazuri.
“Hata kama simu ya mkononi itaibiwa lakini fedha zilizokuwepo hazitaweza
Mamalishe akimpimia mteja wa chai ambaye alikuwa ndani ya daladala kwenye Kituo cha Shule ya Uhuru Kariakoo, Dar es Salaam jana. Kutokana na ushindani wa biashara hiyo wanalazimika kuwafuata wateja popote. (Picha na Charles Lucas)

VICOBA yakabidhi simu bure kwa wanachama

Na Heri Shaaban


 WANACHAMA w a Vikundi vya Kuweka na Kukopa (VICOBA) wamekabidhiwa simu za mkononi bure,ili waweze kuweka fedha zao kwa njia ya kisasa na kuachana na mtindo wa utunzaji fedha kwa njia ya masanduku.
Hatua hiyo ya kuwakabidhi simu hizo ilizinduliwa Dar es Salaam jana na Makamu wa kwanza wa Rais wa Vicoba Taifa Scholastica Kevela.
Akizindua kampeni hiyo kwa wana Vicoba, Bi. Kevela alisema hatua hiyo itasaidia kupunguza taarifa za upotevu wa fedha na kuwarahisishia uwekaji wa fedha katika mazingira mazuri.
“Hata kama simu ya mkononi itaibiwa lakini fedha zilizokuwepo hazitaweza kuchukuliwa labda muhusika awe anafahamu namba ya siri na hivyo leo nitakabidhi kwa vikundi vya

Musai chafaidika na mradi wa samaki

Na Mercy James, Mbarali


 KIKUNDI cha Muungano wa Ufugaji Samaki Igomelo (MUSAI) kilichopo kijiji cha Igawa wilayani Mbarali mkoani wa Mbeya, kimeanza kunufaika na mradi wa ufugaji samaki katika mabwawa yaliyopo katika eneo la umwagiliaji la Igomelo na kujipatia zaidi ya sh. milioni 2.3.
Kikundi hicho ambacho kilianza mwaka 2009 kikiwa na wanachama 30 na sasa wamebaki 19, kimetumia nguvu zao kwa asilimia 20 na serikali kupitia mfuko wa DADPS kuchangia asilimia 80 ya mradi huo, ambapo wafugaji hao wamevuna jumla ya kg 170, katika awamu ya kwanza na awamu ya pili wamevuna kg 200 na kupata jumla ya kg 370.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Musai, Abdallah Jumma alisema licha ya

Serikali yawatoa hofu waandishi wa habari

Na Mwandishi Wetu, Tanga

SERI K A L I i m e a h i d i kuendelea kuhakikisha mazingira ya kazi ya waandishi yanaboreshwa na pale ambapo maisha yao yanakuwa hatarini, haitasita kuchunguza na kuchukua hatua stahiki bila uoga wala upendeleo. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Mashauriano Kati ya Baraza la Habari na Wahariri wa Vyombo vya Habari,mjini Tanga jana. a ihdiremii lakireSa mesilaa iPmpango wa kuendesha shughuli za serikali kwa uwazi (OGP ) ambao unasimamiwa na wizara yake na wamedhamiria kuhakikisha kuwa Sheria ya

Wakulima Bumbuli wang'oa chai, wapanda mahindi

Na Yusuph Mussa, Lushoto

MGOGORO wa wakulima wa chai, Chama cha Wakulima wa Chai Usambar a (UTEGA) na mwekezajiShadadMullah umeingia sura mpya baada ya wakulima hao kuamua kung’oa zao la chai na kupanda mahindi. Wakulima hao wanadai kilimo cha chai kimekuwa ni sawa na biashara haramu kwao. Hayo waliyabainisha kwa nyakati tofauti juzi nje ya uzio wa Kiwanda cha Chai Mponde kilichopo Halmashauri ya Bumbuli wilayani Lushoto wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hizi. Walisema, wao kulima chai na kuiuza kwenye kiwanda bila kulipwa vizuri wakati ni wabia ni sawa na kero. “Mwandishi angalia upande ule tumeamua kung’oa chai na kupanda mahindi, tumeona kwetu hii ni biashara haramu, kwani hatufaidiki nayo pamoja na kwamba sisi ni wabia kupitia Chama wa

‘Mgonjwa wa akili’ aua watoto, ajeruhi


Livinus Feruzi, Bukoba
na Thomas Kiani, Singida


 MTU anayedhaniwa kuwa na matatizo ya akili amewaua watoto wawili kwa kuwakatakata mapanga na kumjeruhi mama yake mzazi pamoja na mtoto mwingine wa darasa la saba, wote wakiwa ni wa familia moja.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Bw. Philip Kalangi, alisema tukio hilo lilitokea Kata ya Kamachumu wilayani Muleba. Kamanda Kalangi alimtaja mtuhumiwa wa mauaji hayo kuwa ni Salvatory Sylivester (30), mkazi wa Kikomero.
Waliouawa katika tukio hilo kwa mujibu wa Kamanda Kalangi ni Kevin Antidius (3) na Julieth Julius (5). Waliojeruhiwa ni mama yake mzazi, Valentine Sylvester (69) na Kabyemera Sylvester (7), ambaye anasoma darasa la kwanza.
Kamanda Kalangi alisema mtuhumiwa huyo anashikiliwa na polisi. Alisema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa mtuhumiwa alikuwa na matatizo ya akili. Alisema polisi wanaendelea na

Sitta awasha moto CCM



*NI KUTOKANA NA KAULI YAKE KUHUSU URAIS 2015
*MANGULA ASEMA NEC HAIJATANGAZA MCHAKATO KUANZA
*ASISITIZA WATAKAOJITANGAZA WATAKATWA 

 WAKATI Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akijipambanua wazi kuwa yeye na mawaziri wenzake watatu wanaoendana kimawazo watakaa na kuangalia mmoja wao awanie urais mwaka 2015 , Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula, amesema wanaofanya hivyo wanakiuka katiba ya CCM hivyo wakati ukifika watakatwa majina yao.
Mangula alitoa kauli hiyo juzi wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari mara baada ya kuzindua kampeni za mgombea udiwani wa CCM katika Kata ya Iyela, jijini Mbeya.
Alisema Katiba ya chama hicho iko wazi na inataka wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi kupitia CCM kusubiri wakati nafasi husika zitakapotangazwa.
Alisema kufanya hivyo kabla ya kutangazwa ni kutomtendea haki kiongozi

LHRC yaja na mapya sakata la gesi

Na Waandishi Wetu


 SAKATA la kupinga ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, bado ni tete baada ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kubaini kuwepo kwa vijana wanaoapishwa viapo na wazee wa kimila kuhakikisha gesi hiyo haitoki.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Harold Sungusia, alisema utafiti wao umebaini jinsi kiapo hicho kinavyofanyika.
Alisema wananchi hao w amemw a g a d amu y a mbuzi wawili ili kukamilisha matambiko na imani za viapo hivyo kimila.
“Kutokana na utafiti, tumeona umuhimu wa kutoa tamko kwenu ili mtusaidie kueleza jamii, Serikali na wananchi wa Mtwara kuwa kuendelea kuamini kuwa hali ya Mtwara ni shwari sawa na kufunika moto kwa blanketi, kwani vijana wetu wanaendelea kula viapo vya kuhakikisha gesi haitiki,”alisema
Aliongeza kuwa katika utafiti huo wameweza kuongea na wazee hao

Mbunge amkingia kifua JK bungeni

Na Waandishi Wetu


 MBUNGE wa Peramiho kwa tiketi ya CCM, Jenista Mhagama , amemkingia kifua, Rais Jakaya Kikwete, akitaka Bunge lisimfanyie tathmini kuhusiana na kauli yake kuwa hali ya kifedha kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini ni nzuri, kauli ambayo kambi rasmi ya upinzani bungeni, imedai inapingana na ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambayo imeonesha hali ya mifuko hiyo kuwa ni mbaya
 Mbunge huyo alitoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma jana, wakati akichangia makadirio ya bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa mwaka wa fedha 2013/14.
Alisema kuwa kitendo cha kumpakazia maneno Rais Kikwete, si jambo la

28 May 2013

Maofisa wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO), Mkoa wa Kinondoni Kaskazini, wakijiaandaa kukata umeme katika nyumba namba 604, Mtaa wa Msisiri Mwananyamala baada ya kubaini wizi wa umeme katika nyumba hiyo, ambapo pia ilikutwa mita ilitoka eneo jingine bila idhini ya shirika. (Picha na Charles Lucas)

Baadhi ya wafanyabiashara wa nazi kwa jumla katika Soko la Ilala, wakichagua bidhaa hiyo, Dar es Salaam hivi karibuni, ambapo bei ya nazi moja iliuzwa sh. 350. nazi hizo nyingi zinatoka mkoani Tanga. (Picha na Heri Shaaban)
Mtuhumiwa wa kesi ya kula njama za kutenda kosa ambaye ni Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bw. Wilfred  Lwakatale akiwa chini ya ulinzi wa askari Magereza, wakati akitoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam jana, mara baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo hadi Juni 10 mwaka huu. Wa pili kulia ni mshitakiwa wa pili, BW. Ludovick Joseph. (Picha na Heri Shaaban)

27 May 2013

Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali Dkt.Mohamed Mohamed aliye simama kulia akizungumza na wajumbe wa baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala Dar es Salaam juzi,katika Mdahalo wa kujadili Maendeleo ya Tiba Asili nchini.(Picha na Prona Mumwi)
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Saruji ya Twiga (TPCC), Pascal Lesoinne (kushoto),wakishirikiana kukata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Wazo Misikiti na PK Tegeta itakayojengwa na kampuni hiyo.(katikati) Diwani wa Kata ya Wazo Bw John Moro uzinduzi huo ulifanyia Dar es Salaam mwishoni mwawiki,watatu kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Wazo, Mtuzya Mtuzya. Kulia ni Meneja Huduma za Jamii wa TPCC, Natasha D’Souza, na (wa pili kulia) Mkuu wa Rasilimali Watu wa kampuni hiyo, Jayne Nyimbo.Ujenzi huo utagharimu sh milioni 175.(Na Mpigapicha wetu)
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (MNEC) Taifa, Wilaya ya Korogwe Vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Tanga, Dkt. Edmund Mndolwa, akimtambulisha kwa wajumbe wa Baraza Kuu la Wanawake wa wilaya hiyo (hawapo pichani), Diwani wa Kata ya Kwadelo wilayani Kondoa mkoani Dodoma juzi, Alhaji Omari Kariati (kushoto), wakati wa semina ya uelewa wa kilimo cha alizeti. Diwani huyo alialikwa kutoa elimu iliyofanikisha kilimo cha zao hilo kwenye kata yake. (Na Mpigapicha Wetu)

Wafanyabiashara waandamana kupinga ushuru

Na Patrick Mabula, Kahama


 WAFANYABIASHARA wa mazao ya nafaka na wasafirishaji wenye magari malori, wilayani Kahama wameandamana hadi ofisi za Halmashauri ya wilaya wakipinga ushuru wanaotozwa kuwa ni mkubwa.
Wafanyabiashara hao waliandamana juzi na kuvamia ofisi za halmashauri hiyo baada ya malori yaliyokuwa yamebeba nafaka kukamatwa na askari mgambo kutokana na mgogoro huo wakipinga kutozwa ushuru mara mbili.
Kundi hilo la wafanyabiashara wakiwa katika ofisi za Halmashauri hiyo, askari mgambo aliyekuwa akilinda alilazamika kupambana nao bila mafanikio huku akitishia kuwalipua kwa bunduki hali iliyowatia hasira na kusababisha vurugu kubwa.
Wakiongea na waandishi katika ofisi hizo wafanyabishara hao walikuwa

Mndolwa awataka wananchi kujikita katika kilimo cha alizeti

Na Mwandishi Wetu, Korogwe


 MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (MNEC) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Tanga, Dkt. Edmund Mndolwa amewataka wananchi wakazi wa Wilaya ya Korogwe Vijijini kujikita katika kilimo cha alizeti ili kiweze kuwakomboa kiuchumi.
Dkt. Mndolwa alieleza kuwa mazingira ya wilaya hiyo na Mkoa wa Tanga kwa ujumla yanahimili kilimo cha alizeti hivyo kama wananchi watakithamini na kulifanya zao hilo kuwa la biashara watanufaika haraka kwa kuondokana na umaskini na utegemezi.
Kiongozi huyo aliyasema hayo wakati akiwahamasisha wananchi kutoka vijiji vya kata na tarafa za wilaya hiyo juzi na kuwahakikishia wananchi hao kwamba kilimo cha alizeti hakitawaacha maskini kutokana na utafiti wa kisayansi kuthibitisha ubora na manufaa ya zao hilo ikiwa ni

Dkt. Salim ahimiza maadili kwa viongozi, Watanzania


Na Mwandishi Wetu,
Zanzibar


 WA Z I R I Mk u u Ms t a a f u , Dk t . S a l im A hme d Salimu, amewataka viongozi na Watanzania kwa ujumla kuzingatia maadili kwani taifa limefika hapa lilipo kutokana na ukosefu wa maadili kwa viongozi na wananchi kwa ujumla.
Kutokana na hali hiyo, alitoa mwito kwa viongozi na Watanzania kwa ujumla, kuzingatia maadili ya uongozi na kwa Watanzania kuzingatia maadili ya utaifa alioacha mwasisi wa Taifa hili, hayati Mwalimu Julius Nyerere.
Dkt. Salim, aliyasema hayo, katika mahojiano maalum mara baada ya uzinduzi wa Tawi jipya la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein, eneo la Bububu, nje kidogo ya mji wa Zanzibar, mwishoni mwa wiki.
Alisema hatua hiyo itasaidia kulinda misingi mikuu ya taifa letu ambayo ni

Viongozi CCM Tabora wazomewa mkutanoni

Na Mwandishi Wetu, Tabora


 BAADHI ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kukumbwa na izomeazomea kutoka kwa wananchi wakati wa mkutano wa hadhara.
Tukio hilo lilitokea kwenye mkutano huo ambao ulifanyika kwenye viwanja vya stendi ya mabasi ya zamani ambapo CCM ilikuwa ikifanya mkutano wake.
Mkutano huo wa hadhara ulifanyika baada ya viongozi wa CHADEMA wakiongozwa Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, kufanya mkutano eneo hilo na kusema wabunge wa CCM Tabora hawawatendei haki wapiga kura wao.
Alisema viongozi wa CHADEMA watapiga kambi mkoani Tabora kuwatetea wananchi kuhusiana na haki zao.
Hatua hiyo iliwafanya CCM nao kujibu mapigo kwa baadhi ya viongozi wake akiwemo Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, Aden Rage, kujibu mapigo.
Dalili za zomeazomea zilianza mapema kwani baadhi ya wananchi walianza

Walimu ‘vinara’ wa mapenzi watajwa


Na Suleiman Abeid,
Kahama


 KATIKA hali isiyo ya kawaida, wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyasubi, iliyopo Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, wamepiga kura za siri ili kuwafichua walimu wenye tabia ya kufanya mapenzi na wanafunzi wao shuleni hapo.
Uamuzi wa kupigwa kura hizo ulifikiwa hivi karibuni kwenye Kikao cha Baraza la Shule la Watoto ambacho kiliitishwa kwa lengo la kujadili vurugu zilizokuwa zikijitokeza shuleni hapo na kusababisha baadhi ya walimu kupigwa.
Kikao hicho kiliitishwa na Mratibu wa Mradi wa Haki Yangu Sauti Yangu, mkoani humo, Bw. Gerald Ng’ong’a na kubaini kuwa, sababu moja wapo iliyochangia vurugu hizo ni baadhi ya walimu kufanya mapenzi na wanafunzi wao.
Inadaiwa hali hiyo pia imechangia wanafunzi wengi waliomaliza kidato cha

CCM, CWT Bunda wavutana kiutendaji

Na Raphael Okello, Bunda


 KATIBU Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Bunda, mkoani Mara Jonas Sariro, ametoa onyo kwa viongozi wa Chama cha Walimu nchini (CWT), wilayani humo na kudai kuwa, CCM ina jukumu la kuwasimamia watumishi wa Serikali ili waweze kutekeleza sera na ilani ya chama.
Sariro ametoa onyo hilo kutokana na madai ya CWT wilayani humo kuilalamikia CCM wakidai viongozi wake wanafanya kazi za Serikali kwa kukagua utendaji wa walimu shuleni, kuwafokea na kutishia kuwafukuza kazi au kuwahamisha.
CWT walidai kuwa, hoja ya viongozi wa CCM ni juu ya chama ambacho ndicho kinachoongoza dola kuwajibika kuwalipa mishshara walimu.
Alisema CCM ipo tayari kuwachukulia hatua walimu wote ambao

CHADEMA wapata pigo Sengerema


 Na Mwandi shi We tu, Sengerema

 ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( BAVI CHA) , mk o a n i Mwanza, Bw. Slavatory Magafu, amekihama chama hicho na kujiunga Chama cha NCCR-Mageuzi.
Bw. Magafu alijiunga na chama hicho juzi wakati wa kampeni za kumnadi mgombea udiwani katika Kata ya Nyampulukano, wilayani Sengerema, Bw. Dotto Nungwa.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa kadi ya NCCR-Mageuzi,Bw. Magafu alisema ame b a i n i CHADEMA hakiwezi kuifikisha nchi katika mikono salama.“Mwaka 2010 niliwania ubunge wa jimbo hili kwa tiketi ya CHADEMA, hivi sasa nimejiunga rasmi NCCR-Mageuzi chama ambacho hakina udini, ukabila wala ukanda,” alisema.
Kwa upande wake, Bw. Nungwa aliahidi kuwasaidia wananchikwa kumaliza kero zao na kuhakikisha wanashiriki mikutano yakata na vijiji pamoja na kusomewa

Polisi wanusurika kufa wakikimbiza pikipiki

Na Said Hauni, Lindi


 ASKARI wawili wa Jeshi la Polisi akiwemo mmoja wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Wilaya ya Nachingwea, mkoani Lindi, wamelazwa katika Hospitali ya Nyangao, baada ya pikipiki waliyokuwa wakiitumia kugongana na gari ndogo.
Ajali hiyo ilitokea wakati askari hao wakimkimbiza mwendesha pikipiki aliyekuwa amekiuka Sheria za Usalama Barabarani. Kamanda wa Polisi mkoani humo, George Mwakajinga, alisema ajali hiyo imetokea wilayani humo Mei 20 mwaka huu.
Aliwataja askari hao kuwa ni F 6986 PC Living aliyevunjika miguu yote miwili na mkono wa kushoto na G 2116 PC Edwin, ambaye amepata maumivu ya ndani kwa ndani.
“Hawa askari walikuwa kazini wakiwa wamepakiana kwenye pikipiki aina ya