30 May 2013

LHRC yaja na mapya sakata la gesi

Na Waandishi Wetu


 SAKATA la kupinga ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, bado ni tete baada ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kubaini kuwepo kwa vijana wanaoapishwa viapo na wazee wa kimila kuhakikisha gesi hiyo haitoki.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Harold Sungusia, alisema utafiti wao umebaini jinsi kiapo hicho kinavyofanyika.
Alisema wananchi hao w amemw a g a d amu y a mbuzi wawili ili kukamilisha matambiko na imani za viapo hivyo kimila.
“Kutokana na utafiti, tumeona umuhimu wa kutoa tamko kwenu ili mtusaidie kueleza jamii, Serikali na wananchi wa Mtwara kuwa kuendelea kuamini kuwa hali ya Mtwara ni shwari sawa na kufunika moto kwa blanketi, kwani vijana wetu wanaendelea kula viapo vya kuhakikisha gesi haitiki,”alisema
Aliongeza kuwa katika utafiti huo wameweza kuongea na wazee hao
wa kimila na kuwahakikishia kuwa kati ya mbuzi hao, ambao mmoja alichinjwa eneo la Msimbati ambapo kutajengwa bomba la gesi, ikiwa ni ishara ya kuhakikisha gesi, haitoki ,” alisema.
Alisema mgogoro huo ambao umeleta madhara kutokana na vurugu za Mei 22, mwaka huu umesababisha vifo na mauaji, uharibifu wa mali, kukosekana kwa amani kati ya wananchi na vyombo vya usalama.
Sungusia aliitaka Serikali kuboresha vyombo vyake vya usalama na kufanya mabadiliko ili kurejesha uhusiano mzuri na wananchi.
Pia wameshauri kamati teule iliyoundwa na Bunge kufika Mtwara na kufanya mazungumzo na wananchi ili kupata taarifa sahihi na kutafuta mbinu mbadala za kurejesha amani ya kudumu.
K w a u p a n d e w a k e Mwanasheria wa LHRC, Bi Grace Mwangamila, alisema kutokana na tafiti hiyo wamegundua kuwa wananchi wa Mtwara bado wana roho ya kinyongo.
CUF yaandaa kongamano
Kwa upande wake Chama cha Wananchi (CUF), kinaandaa kongamano maalum kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Mtwara na Lindi wanaoishi jijini Dar es Salaam, ili kuwaelimisha kuhusiana na hasara na faida zinazotokana na gesi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro, alisema mkutano huo utafanyika Juni 2, mwaka huu katika ofisi za chama hicho kutokana na maombi ya wananchi hao.
Alisema wameamua kufanya mkutano huo jijini Dar es Salaam baada ya Serikali kupiga marufuku mikutano ya wanasiasa na asasi za kiraia mkoani.
“Tumeamua kufanya mkutano huu kwa ajili ya kuwaelimisha Watanzania wenzetu ambao hawajui hadi sasa gesi ina faida gani na hasara zipi, hivyo tutawaeleza suala zima la uwekezaji katika sekta hii,”alisema Itatiro.
A l i o n g e z a k w a m b a inawezekana fujo zao zinatokana na kutoelewa lolote juu ya suala la gesi . Pia alisema katika kongamano hilo wananchi wataandika maoni mbalimbali ambayo yatakusanywa na kupelekwa katika Ofisi ya Rais, Ofisi ya Wazuri Mkuu, na Spika wa Bunge.
CEGODETA
Nayo Taasisi ya Utawala Bora na Maendeleo Tanzania (CEGODETA) imeitaka Serikali kuhakikisha inafanya uchunguzi wa kina na kuwachukulia hatua wanasiasa wote watakaobainika kuhusika na vurugu za Mtwara na kusababisha watu kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa bila kujali nyadhifa zao.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na kusainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa CEGODETA, Thomas Ngawaiya, ililaani vikali vurugu hizo na kuitaka serikali kuwachukulia hatua wahusika wote.
N g a w a i y a a l i s e m a kutokufanya hivyo kutaifanya Tanzania kuonekana ni nchi isiyotawalika kama baadhi ya nchi za Kiafrika zilivyo.
“CEGODETA inaamini kwamba vurugu za Mtwara zina mkono wa kisiasa, hivyo serikali ifanye uchunguzi wa kina na kuwachukulia hatua wanasiasa wote watakaobainika kuhusika na vurugu hizo bila kujali ni vyama gani au wana wadhifa gani ndani ya vyama vyao, vinginevyo Tanzania itakuwa ni nchi isiyotawalika,” alisema.
Alionya wanasiasa wanaotaka kutumia vurugu ili kuingia madarakani kuacha mara moja kwani wanapaswa kuelewa kuwa amani ya nchi itakapovurugika hata wao watadhurika.
Aliitaka Serikali ichukue hatua zinazofaa kuhakikisha matukio kama hayo hayajirudii tena mkoani Mtwara na nchi nzima.
Ime a n d i k w a Ma r i a m Mziwanda, Rehema Maigla na Rose Itono

No comments:

Post a Comment