30 May 2013

Balozi Seif awafunda wakulima wa karafuu


Na Mwajuma Juma,
Zanzibar


 WAKUL IMA wa mashamba ya karafuu w ame s h a u r i w a kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalamu wa kilimo hicho ili kujenga nguvu za uzalishaji wa uhakika wa zao la karafuu nchini.
Ushauri huo ulitolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi wakati wa ziara yake ya kukagua baadhi ya mashamba ya Serikali ya miti ya mikarafuu ambayo yako chini ya usimamizi wa baadhi ya wakulima ndani ya Mkoa wa Kusini Pemba.
Alisema kumejengeka dhana kwa baadhi ya wakulima wa mikarafuu kujilimbikizia miti mingi ya zao hilo wakiwa na fikra za kupata uzalishaji mkubwa zaidi jambo ambalo ni
ndoto kitaalamu.
Aidha, alisema kuwa Serikali inaendelea na mikakati ya kuimarisha zao hilo na kuwasihi wananchi pamoja na wakulima wa kilimo hicho kuunga mkono juhudi hizo, ambazo zimeleta faraja kwa Serikali.
"Hivi sasa tunapaswa kuwa makini katika uzalishaji wa zao la karafuu kitaalamu kwani wakati wa kuvuna karafuu mpeta umepitwa na wakati kulingana na mazingira yaliyopo ya soko la dunia," alisisitiza Balozi Seif.
Kwa upande wao wakulima hao walieleza kuwa ufinyu wa taaluma ya kilimo hicho ndio uliokuwa ukiwapa ukaidi na kupelekea kuleta mgongano kati yao na wataalamu wa kilimo hicho.
Mapema Ofisa Mdhamini wa Wizara ya Ardhi, Makazi, Maji na Nishati Pemba, Hemed Salum alisema kasi ya wakulima wa mikarafuu k u j i t o k e z a k u f y e k e a mashamba yanayomilikiwa na Serikali hivi sasa imeongezeka zaidi.

No comments:

Post a Comment