31 May 2013

Mtoaji taarifa za uwongo kwa IGP, Waziri ahukumiwa

Na Rehema Mohamed


 Mohamed (25), amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela au faini ya sh. milioni tatu baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka matatu.
Mashtaka hayo ni kutoa taarifa za uongo katika mitandao ya simu za mkononi na kutuma ujumbe wa maudhi kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Said Mwema.
Mshtakiwa huyo alisomewa hukumu hiyo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam na Hakimu Hellen Liwa ambapo upande wa mashtaka uliwakilishwa na wakili Bw. Ladslaus Komanya.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Liwa alisema hayo ni makosa mapya yaliyo katika Sheria Mpya ya Mawasiliano na Mitandao.
“Kwa kitendo ulichokifanya kuwatumia ujumbe viongozi wa juu wa
serikali unahukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela au kutoa faini ya sh. milioni tatu iwe fundisho kwa wengine, kama hujaridhika na adhabu unaweza kukata rufaa,” alisema.
Katika maelezo ya awali, ilidaiwa Mei 20 mwaka huu katika Makao Makuu ya jeshi hilo, zilipelekwa taarifa za kiintelejentsia kwa maofisa wa ngazi za juu kuwa kuna mtu ambaye namba yake ya simu imesajiliwa kwa mitandao tofauti.
Namba hizo ni 0687 521947 na 0687 521948 za Airtel na 0759 799956 ya Vodacom zilizokuwa zikitumika kutoa ujumbe kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na IGP.
Baada ya upelelezi kufanyika, ilibainika namba hizo zilisajiliwa kwa majina tofauti ambayo ni Fadhili Issah, Fadhili Issa na Godfrey Joseph ambazo alikuwa akizitumia mshtakiwa.
Baada ya mshtakiwa kukamatwa Mei 25 mwaka huu na kuhojiwa polisi, alikiri kutumia namba hizo na kuzisajili kwa majina tofauti kwa lengo la kufanya uhalifu na kuficha utambulisho wake.
Mei 27 mwaka huu, mshtakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashtaka yanayomkabili na kukiri kutenda makosa hayo

No comments:

Post a Comment