Na Mwandishi Wetu,
Zanzibar
WA Z I R I Mk u
u Ms t a a f u , Dk t . S a l im A hme d Salimu, amewataka viongozi na
Watanzania kwa ujumla kuzingatia maadili kwani taifa limefika hapa lilipo
kutokana na ukosefu wa maadili kwa viongozi na wananchi kwa ujumla.
Kutokana na hali hiyo, alitoa mwito
kwa viongozi na Watanzania kwa ujumla, kuzingatia maadili ya uongozi na kwa
Watanzania kuzingatia maadili ya utaifa alioacha mwasisi wa Taifa hili, hayati
Mwalimu Julius Nyerere.
Dkt. Salim, aliyasema hayo, katika
mahojiano maalum mara baada ya uzinduzi wa Tawi jipya la Chuo cha Kumbukumbu ya
Mwalimu Nyerere uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein, eneo la Bububu, nje kidogo ya mji wa
Zanzibar, mwishoni mwa wiki.
Alisema hatua hiyo itasaidia kulinda
misingi mikuu ya taifa letu ambayo ni
umoja, usawa, amani na utulivu ambayo
sasa imeanza kumomonyoka.
Alikuwa akijibu swali kuhusu hali ya
Taifa letu katika kuzienzi tunu za taifa letu za umoja, usawa, amani na utulivu
alizoacha Mwalimu Nyerere.
Akichangia suala hilo, Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi
(CUF), Maalim Seif Shariff Hamad, alisema viongozi wengi kwa sasa hawafuati
misingi ya uongozi aliotuachia Mwalimu Nyerere.
Alitolea mfano malumbano ya kidini
yanayotokea hivi sasa, kuwa ni uthibitisho wa kuanza kupotea kwa misingi ya
umoja aliyoacha Mwalimu Nyerere.
Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha
Mwalimu Nyerere, Dkt. Chinuno Magoti, amesema, kwa kutambua umuhimu wa falsafa
ya Mwalimu Nyerere kuhusu usawa, umoja, amani na utulivu, chuo hicho cha
Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, kinatoa mafunzo kwa vitendo.
Alisema kamwe hauwezi kusikia migomo
yoyote katika chuo hicho kutokana na kufundisha utii na nidhamu ya hali ya juu.
Tawi jipya la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,
lilizinduliwa rasmi eneo la Bububu mjini Zanzibar na Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein, mwishoni mwa wiki.
No comments:
Post a Comment