31 May 2013

Filikunjombe: Nina imani na uongozi CCM

Na Mwandishi Wetu, Ludewa


 MBUNGE waLu dewa, mkoaniNjombe, Bw. D eoFilikunjombe, ameipo nge za safumpyawaChamaChaMapindu zi (CC M), kwakazi kub wa wanayo endeleakuif anyailikukijengachama hichokuanzia ngazi ya shina hadi T aifa.
Bw .Filikunjomb eali yasemahayom jini humoja nawakati akihutub iawananc hikwenyemkutanowa hadharauli ofanyika katikaKatayaLupinguna kuonge za kuw a, y eyote mwe nyendotoyakushi ndanana CCM anapot eza mudawake.
“KatibuMkuu wa chamach etu, Bw. Abdu lrahmanKinan a,pianinai manik ub wanaKatibu wa NEC ,Itikad inaUen ez i, Bw. NapeNnauye,k azi wanayoifanyayakupigani awanyonge inaone sha kiwan gocha uzalendo walichnachohiv yot uwaungem kono.
 “Kasi ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010/2015, kusimamia
shughuli za maendeleo nchini ni dhahiri umasikini utaondoshwa katika nchi yetu kwa kasi kubwa,” alisema.
Alisema ahadi zote zilizotolewa 2010, atahakikisha zinatekelezwa kwa kiwango cha juu ili kuwajengea imani wananchi hao na kudai kuwa, atahakikisha anafanikisha ujenzi kwa Barabara Kuu ya Njombe- Ludewa kwa kiwango cha lami.
Pia aliahidi kuanzisha mchakato wa ujenzi wa barabara itokayo Ludewa Mjini kwenda Mwambao wa Ziwa Nyasa ikiwemo Kata ya Lupingu.
Akizungumzia maboresho ya mawasiliano ya simu, mbunge huyo alisema tayari maombi yake ya minara mitano yameanza kutekelezwa ambapo hivi sasa amepata minara mitatu ambayo itapanua huduma ya mawasiliano ya simu za mkononi katika maeneo mbalimbali wilayani humo na Kata hiyo ya Lupingu.
Kwa upande wake, Bw. Kinana alipongeza jitihada zinazofanywa na Bw. Filikunjombe katika kutetea na kusimamia utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya wananchi wa jimbo hilo.

No comments:

Post a Comment