30 May 2013

Sitta awasha moto CCM



*NI KUTOKANA NA KAULI YAKE KUHUSU URAIS 2015
*MANGULA ASEMA NEC HAIJATANGAZA MCHAKATO KUANZA
*ASISITIZA WATAKAOJITANGAZA WATAKATWA 

 WAKATI Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akijipambanua wazi kuwa yeye na mawaziri wenzake watatu wanaoendana kimawazo watakaa na kuangalia mmoja wao awanie urais mwaka 2015 , Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula, amesema wanaofanya hivyo wanakiuka katiba ya CCM hivyo wakati ukifika watakatwa majina yao.
Mangula alitoa kauli hiyo juzi wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari mara baada ya kuzindua kampeni za mgombea udiwani wa CCM katika Kata ya Iyela, jijini Mbeya.
Alisema Katiba ya chama hicho iko wazi na inataka wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi kupitia CCM kusubiri wakati nafasi husika zitakapotangazwa.
Alisema kufanya hivyo kabla ya kutangazwa ni kutomtendea haki kiongozi
aliyeko madarakani ambaye ndiye anayetekeleza ilani ya chama.
Mangula alisisitiza kuwa n i ma k o s a ma k u bwa kwa mwanachama yeyote kuzunguka wakati huu na kujitangaza kuwa atawania urais mwaka 2015, kutokana na ukweli kuwa tayari nchi inaongozwa na Rais anayetoka CCM ambaye ni Rais Jakaya Kikwete.
“Hivyo kutangaza nia kabla ya wakati ni makosa makubwa,” alisisitiza. Alisema kuwa kama chama hicho kitakuwa na ushahidi wa kutosha kuwa kuna wanachama walijitangaza mapema kabla ya wakati kutangazwa ni wazi kuwa vikao vya mchujo vitawachuja na kuwaondoa katika orodha ya wanaowania nafasi hiyo na kubaki na wagombea waliofuata kanuni na katiba ya chama hicho.
Alisema watakaobainika tutawakata majina yao kwa kuwa ni NEC tu yenye mamlaka ya kutangaza wakati wa kujitangaza.
Kwa upande wa nafasi za ubunge na udiwani katika maeneo ambayo yanaongozwa na upinzani mwanachama wa CCM, anaruhusiwa kupitapita kwa ajili ya kuangalia hali ya hewa na kuwafanya wanachama kumfahamu ili wakati ukifika aweze kujitosa rasmi katika kinyang’anyiro ili kukomboa nafasi hiyo.
Hivi karibuni waziri Sitta akiwa anaongoza harambee katika Kanisa Katoliki la Mt. Josephine alidaiwa kutamka wazi kuwa yeye na rafiki zake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Ujenzi, Dkt.John Magufuli na Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, kwa kuwa ndio anaoendana nao kimawazo na kimsimamo wa kutopenda kuwaonea wanyonge, watakaa na kuona mmoja wao agombee urais.
 YA
O

1 comment:

  1. Hao ni chui waliovaa ngozi ya kondoo katika chama chetu hatutaki wanafiki na wasaliti wa chama kwa kujitafutia umaarufu usio na tija na sisi Watanzania hatuwezi kamwe kumchagua raisi mnafiki kama kafanya hivyo leo itakuwaje wakiwa maraisi si watatusaliti watanzania.

    ReplyDelete