Livinus Feruzi, Bukoba
na Thomas Kiani, Singida
MTU anayedhaniwa kuwa na matatizo ya akili amewaua
watoto wawili kwa kuwakatakata mapanga na kumjeruhi mama yake mzazi pamoja na
mtoto mwingine wa darasa la saba, wote wakiwa ni wa familia moja.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kagera, Bw. Philip Kalangi, alisema tukio hilo lilitokea Kata
ya Kamachumu wilayani Muleba. Kamanda Kalangi alimtaja mtuhumiwa wa mauaji hayo
kuwa ni Salvatory Sylivester (30), mkazi wa Kikomero.
Waliouawa
katika tukio hilo kwa mujibu wa Kamanda Kalangi ni Kevin Antidius (3) na
Julieth Julius (5). Waliojeruhiwa ni mama yake mzazi, Valentine Sylvester (69)
na Kabyemera Sylvester (7), ambaye anasoma darasa la kwanza.
Kamanda Kalangi
alisema mtuhumiwa huyo anashikiliwa na polisi. Alisema uchunguzi wa awali
unaonesha kuwa mtuhumiwa alikuwa na matatizo ya akili. Alisema polisi
wanaendelea na
uchunguzi na kuwa mara baada ya kukamilika mtuhumiwa atafikishwa
mahakamani.
Katika
tukio la pili, mwanafunzi wa
kidato cha pili Shule ya Sekondari ya Kagemu, Umud Buruan (17) amefariki baada
ya kuchomwa jichoni na mwamvuli na mwenzake.
Akielezea tukio
hilo, Bw. Kalangi alisema jana saa 10:30 wakati wanafunzi wakitoka shuleni
kwenda nyumbani walianza kutaniani, ambapo, Machel Omugisha (16) alikasirika na
kumchoma mwezake sehemu ya jicho kwa kutumia mwamvuli aliokuwa nao.
Mwanafunzi huyo
alifariki baada ya kufikishwa katika hospitali ya Mkoa wa Kagera wakati
akipatiwa matibabu na kuwa tayari mtuhumiwa anashikiliwa na polisi.
Wakatu huo
huo, Jeshi la Polisi mkoani Singida
limemtia mbaroni mkazi mmoja wa Kijiji cha Musimi Kata ya Sepuka Wilayani
Ikungi, Swalehe Mohamed (42) maarufu kwa jina la ‘Kipara’ kwa tuhuma za kumuua
mama yake wa kufikia kwa kumkata kata kwa panga mikono yote miwili na kwenye
makwapa yote mawili.
Katika
taarifa yake kwa waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi mkoani
Singida, Jofrey Kamwela, alisema tukio hilo lilitokea jana
No comments:
Post a Comment