WANAWAKE
nchini wametakiwa kutobweteka na kuchangamkia fursa mbalimbali katika kuwania
nafasi za uongozi ili kuingia kwa vitendo katika ngazi mbalimbali za maamuzi.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mbunge wa
Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya
Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA) uliofanyika mkoani humo.
Alisema kuwa wanawake katika chama
hicho hawatakiwi kubweteka kwa lengo la kusubiri kupewa nafasi za upendeleo za
uongozi na hivyo wanapaswa kuzigombania kama wanavyofanya wanaume.
Mafunzo hayo ambayo yanawashirikisha
viongozi wa Bawacha kutoka katika
kanda zote za chama hicho nchini,
yamefadhiliwa na chama rafiki kutoka nchini Denmark.
"Msisubiri kuwezeshwa kwani cha
kupewa si kitamu na ni hatari kusema kuwa tukiwezeshwa tunaweza maana mtabaki
kupewa na mtakuwa nyuma siku zote kwa wanaume".
"Ha k i k i s h e n i wa n awa k e
we n g i wanajitokeza katika shughuli za chama chetu hasa katika chaguzi"
alisema Lissu.
Naye Kaimu Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa,
Suzan Lyimo alisema kuwa miongoni mwa malengo ya mafunzo hayo ni pamoja na
kuwawezesha wakufunzi wa kanda na kukiandaa chama kikanda kwa ajili ya chaguzi
za serikali.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa
Bawacha Tanzania Visiwani, Mariam Msabaha aliwataka wanawake kutoogopa
kugombania nafasi mbalimbali za uongozi kwa kuhofia kuwa nafasi hizo
zimeshikiliwa na wenzao.
Pia
aliwataka viongozi wanawake kutokuwa na choyo pindi watakapoona wanawake wenzao
wanagombea nafasi zinazojitokeza.
No comments:
Post a Comment