KIKUNDI cha Muungano wa Ufugaji Samaki Igomelo (MUSAI) kilichopo kijiji
cha Igawa wilayani Mbarali mkoani wa Mbeya, kimeanza kunufaika na mradi wa
ufugaji samaki katika mabwawa yaliyopo katika eneo la umwagiliaji la Igomelo na
kujipatia zaidi ya sh. milioni 2.3.
Kikundi hicho
ambacho kilianza mwaka 2009 kikiwa na wanachama 30 na sasa wamebaki 19,
kimetumia nguvu zao kwa asilimia 20 na serikali kupitia mfuko wa DADPS
kuchangia asilimia 80 ya mradi huo, ambapo wafugaji hao wamevuna jumla ya kg
170, katika awamu ya kwanza na awamu ya pili wamevuna kg 200 na kupata jumla ya
kg 370.
Mwenyekiti wa
Kikundi cha Musai, Abdallah Jumma alisema licha ya
kuvuna samaki hao
wanategemea kupandikiza vifaranga 9,600 katika mawawa hayo na ameeleza baadhi
ya changamoto zinazowakabiri na mtazamo wao wa baadaye kuwa ni kuzalisha samaki
kwa wingi ili kukuza kipato katika kaya za wanakikundi.
Kaimu Ofisa Idara ya Uvuvi wilaya
alisema, pamoja na kutoa elimu ya ufugaji pia idara hiyo inasimamia
upandikizaji, utunzaji hadi kufikia wakati wa kuvuna na mipango ambayo
wameiweka katika kuhakikisha mabwawa 300 yaliyopo wilayani humo yanakuwa na
mazao ya samaki ili kukuza uchumi wa kaya za wanavikundi waliopata mafunzo.
Augustine
Lawi, Mkuu wa Idara ya Uvuvi na Mifugo amesema, awali mafunzo hayo yalitolewa
na wakufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) ambapo wananchi
walielimishwa kuhusu ufugaji na utunzaji wa samaki bwawani katika kuongeza
uzalishaji wa vifaranga.
No comments:
Post a Comment