BAADHI
ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamejikuta kwenye wakati mgumu baada
ya kukumbwa na izomeazomea kutoka kwa wananchi wakati wa mkutano wa hadhara.
Tukio
hilo lilitokea kwenye mkutano huo ambao ulifanyika kwenye viwanja vya stendi ya
mabasi ya zamani ambapo CCM ilikuwa ikifanya mkutano wake.
Mkutano
huo wa hadhara ulifanyika baada ya viongozi wa CHADEMA wakiongozwa Naibu Katibu
Mkuu, Zitto Kabwe, kufanya mkutano eneo hilo na kusema wabunge wa CCM Tabora
hawawatendei haki wapiga kura wao.
Alisema
viongozi wa CHADEMA watapiga kambi mkoani Tabora kuwatetea wananchi kuhusiana
na haki zao.
Hatua
hiyo iliwafanya CCM nao kujibu mapigo kwa baadhi ya viongozi wake akiwemo
Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, Aden Rage, kujibu mapigo.
Dalili
za zomeazomea zilianza mapema kwani baadhi ya wananchi walianza
vicheko na
kejeli kwa viongozi wa CCM, huku wengine wakisikika wakisema hawataki
majigambo, matusi bali wanataka barabara za lami
Tabora-Nzega,
Tabora-Urambo na ile ya Itigi-Tabora, huku wengine wakisema Peoples Power’.
Wakati
katibu wa CCM Mkoa wa Tabora Idd Ame,akimwaga sera zake,wananchi wachache
waliokusanyika kwenye mkutano huo walianza kuzomea kila katibu huyo alipokuwa
akitoa kauli kuhusu CHADEMA.
"Ndugu
zangu wananchi hebu angalieni mnavyodanganywa, hivi hawa CHADEMA wanajigamba
kujenga barabara wakati wao sio watoaji wa fedha na fedha zinatolewa na
Serikali ya CCM sio hao CHADEMA, wanafiki waongo," alisema.
Alisema
Zitto anaacha jimbo lake Kigoma kwenda Tabora kuwafundisha siasa.
Baada
ya katibu huyo kutamka maneno hayo, ndipo wananchi walipoanza kuzomea kwa nguvu
na kudai wanataka sera na si matusi, huku wengine wakisema CCM waongo siku zote
walikuwa wapi kuja kufanya mikutano hadi CHADEMA waende.
Zomeazomea
ilizidi ambapo Katibu wa CCM Mkoa wa Tabora,alipoendelea kutamka kuwa endeleeni
na huo ujinga wenu hapa tutaumizana hapa, alizidisha hasira za wananchi huku
nao wakijibu mapigo kuwa; “Sawa tu tuumizane tumechoka na ahadi zenu za uongo.”
"Hapa
tuko kamili endeleeni kuzomea tu, tutaumizana kweli kweli hapa msifikiri
hatuwezi na tutawashtaki viongozi wa CHADEMA Tabora kwa kutufanyia fujo kwenye
mkutano wetu,” alisema kada huyo wa CCM.
Wakati katibu huyo akitamka hayo,mjumbe wa NEC, John Mchele,
alitoka jukwaani na kwenda kumnong`oneza katibu huyo.
Nyie chadema kwanini muwanyime haki wenzenu kuendesha mkutano wao! Hao sio wananchi ila ni chadema, chama cha zomeazomea. Muandishi wa habari hii kawapamba tu.
ReplyDeleteWananchi hao wamechoka kudanganywa, kwani lazima waambiwe na CHADEMA ? yaani mnawafanya watu wajinga hawawezi kutofautisha mchele na pumba. Zile siku za zidumu fikra za sijui nani zimepita !!!!!!!!! hivi hamjaamka usingizi wa chama kimoja ?
ReplyDeleteNa zama za chadema M4c za kuuza mbuzi kwenye gunia?
DeleteMtazungumza lugha zote mwaka huu na mwakani. M4C imewashika pabaya. Aluta continua. Wananchi Tabora amkeni kutoka usingizi huo wa chama kimoja. Miaka 50 bado tunaahidiana barabara zisizoisha!.
ReplyDeletemimi mzanzibibari si riziki mpaka ni-ione ccm imeshindwa vibaya sana katika mikoa yote ya tanganyika na zanzibar....
ReplyDeleteccm hawana ila jazba, chuki, ufisadi, mausi na uharibifu wa mali za umma... wameona hawana njia yakushinda uchaguzi wa 2015øøøsasa wanapita wakidanganya watu, kwakutumia pesa za mfuko wa hifadhi za taifa... mabanda hawana wala hoja hawazijui...
Watanzania ni wavivu wa kufikiria kwakweli,hivi kweli mtu anakuaminisha kana kwamba yeye ni mtakatifu, nasi bila kufikiria kitakacho
ReplyDeletetokea tunashangilia tu!!
hakuna mkweli kwny kusaka ulaji watanzania 2metawaliwa na siasa mbov hao viongoz wanawateka 2 muwape kura wajenge makwao hakuna mzalendo wa nchi kutoka chama chochote walaghai 2ukweli ni kuwa uchumi 2nao lakini 2meukalia hzo sera makelele 2 kwa vyama vyote
ReplyDelete"Heee et viongozi wanatudanganya ili tuwape kura wajenge makwao"Mbona unaongea kama mwenda wazimu?wewe huoni mahali nchi ilipofikia wala huoni nchi yetu inaelekea wapi, nchi imejaa dhuluma kila kona watu wanajitoa mhanga kutetea halafu we unabeza? Ok fyne onyesha wewe uzalendo wako ili wote tutoke hapa tulipo. Kama umekata tamaa ya maisha ni wewe sio sisi. Jamani tuwapuuuze watzu wa aina hii inawezekana hata familia ao wamezitelekeza kwani hawana uelewa wa kufikiria na kutatua matatizo wanategemea kupewa kanga zenye picha a watu fulani, tshirts n.k
DeleteHapana bwana chadema itawapa kazi, itawajengea barabara za lami mpaka mlangoni, itawasomesha bureeeee, itawaruhusu wachimbe madini yao wenyewe wauzeee wapate fedha!. Nchi nzu ina rasilimal za kutosha. pipozi pawaaaa!
ReplyDeletesisiem kuweni na busara za kuwasoma wananchi, sio kila jambo waonekane wametumwa na chadema. tutuashindwa kujijenga wenyewe nw kuwapa shavu wapinzani. mfano kuna haja gani ya kutosikiliza hoja za mbatia? mwigulu kuwa makini maana kile ukiingia singida lazima kuwe na fujo kila siku kampeni za kata ya iseke zinafanyika na hakuna fujo lakini jana ulipoingia ukashauri ccm wabebe mapanga na virungu.
ReplyDeleteKumbe Mwigulu ana fujo. Kumbe kila mtu anachukia fujo. Kama unachukia fujo nanwewe usifanye fujo!
ReplyDeleteHawa ccm wako kama vidama vya kondoo,Hawawezi kufikiri nini kilicho na ukweli na ni nini ni uongo . Hivi miaka hamsini ya ccm bado mnadanganyika tu ?hamuwezi kujua kama hawa ni wezi wahuni na matapeli no1, nchini ni wao. Eti pesa ziko Serikalini iko wapi hiyo Serikali ?Wakija tena waambieni siku zao ZINAHESABIKAA
ReplyDeleteZiikisha za hayo yataingia majizi mengine. Kama wewe utabahatika itakua vyema. Ningependa nikufahamu nipendekeze upewe utakatifu!!!!!!! Serikali lazima iwepo hata kama ukilia itakuawapo. Hakuna dola nzuri yoyote duniani. Bora yetu
DeleteNYANI WANAFUKUZA NGEDERE ILI WAO NDO WATUNZE SHAMBA LA MAHINDI
DeleteJamani watanzania tuepuke hao wahuni wa chadema kama ukoma. Ni wadanganyifu wa kutupwa! Hawasemi huko nyuma hali ilikuaje. Hakuna hata kijiji kilichokua na huduma ya umeme. Mikoa mingi ili remote, haifikiki. Watu walikua hawawezi kununua hata dawa ya meno. Sasa hivi angalau kuna kamiddle class kanakoingilika kirahisi. Shida zetu ni kubwa sana na umasikini unatisha. Lakini turuhusu hawa wahuni waharibu na kunyang'anya hat hiki kidogo? Ndivyo wanavyotamba mitaani!Hata kama umejinyima ukajenga kibanda chako ukapaka rangi vizuri eti wanakuita fisadi
ReplyDelete