31 May 2013

Kova, Kamuhanda wapanda vyeo

Na Mosi Mrisho


 RAIS Jakaya Kikwete, amewapandisha vyeo baadhi ya maofisa wa polisi akiwemo Kamanda wa Polisi mkoani Iringa, Michael Kamuhanda, kuwa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, uteuzi ambao unaanza mara moja.
Katika uteuzi huo, Kamanda Kova na Isaya Mngulu, wote wamekuwa Makamishna wa Polisi (CP).
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi, ilisema maofisa wengine waliopandishwa vyeo katika ngazi hiyo ni Thobias Andengenye na Simon Sirro.
Msemaji wa Wizara hiyo, Bw. Isaac Namtanga, aliwataja maofisa wengine kuwa ni Elice Mapunda, Brown Lekey, Hamdani Omar Makame, Kenneth Kasseke, Abulrahman Kaniki, Adrian Magayane, Sospeter Kondela na Ernest Mangu. Wengine ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, Hussein Laisseri, Anthony Mwami, Adolfina Chialo, Mpinga Gyumi, Ally Mlege, Hezron Gyimbi na Jonas Mugenzi ambao kabla ya uteuzi huo walikuwa Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi.

No comments:

Post a Comment