30 May 2013

Serikali yawatoa hofu waandishi wa habari

Na Mwandishi Wetu, Tanga

SERI K A L I i m e a h i d i kuendelea kuhakikisha mazingira ya kazi ya waandishi yanaboreshwa na pale ambapo maisha yao yanakuwa hatarini, haitasita kuchunguza na kuchukua hatua stahiki bila uoga wala upendeleo. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Mashauriano Kati ya Baraza la Habari na Wahariri wa Vyombo vya Habari,mjini Tanga jana. a ihdiremii lakireSa mesilaa iPmpango wa kuendesha shughuli za serikali kwa uwazi (OGP ) ambao unasimamiwa na wizara yake na wamedhamiria kuhakikisha kuwa Sheria ya
Haki ya Kupata Habari inatungwa kwa kuwashirikisha wadau wote ili kuwapa wananchi haki ya kutafuta habari na kuzitumia kwa maendeleo yao. Alichukua nafasi hiyo kuwapa pole wanahabari na wanandugu wa waand i s h i w a l i o p a t a madhara mbalimbali. “Napenda kuwahakikishia kuwa Serikali iko pamoja nao na inatambua mchango mkubwa ambao waandishi mnatoa katika kuleta maendeleo ya nchi yetu,” alisema na kuongeza; “Mnayo haki na kwa hakika ni wajibu wenu kudai kwa sauti kubwa wale walioshiriki katika kuwadhuru wanahabari watiwe nguvuni na kufikishwa katika vyombo vya sheria.” Alisema waandishi wa habari wajiepushe na ushabiki wa aina yeyote ile uwe wa kidini, kisiasa au kikabila kwa kutumia vyombo vya habari. Alitoa pongezi kwa Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwa kuona umuhimu na kuunda Baraza . irabaHa ya insaTa la bitaKa lAlifafanua kuwa ni matumaini yake umoja wao katika Baraza hilo utafanikisha masuala ya wanahabari kuingizwa katika Katiba ijayo. “Naamini baadhi ya masuala hayo ni pamoja na lile la Uhuru wa kupata habari, Uhuru wa vyombo vya habari na Uhuru wa uhariri pamoja na Uhuru wa kujieleza na kutoa maoni,” alisema Waziri Chikawe. Alisema iwapo masuala hayo yatasimamiwa kwa dhati yatapata nafasi katika Katiba mpya. “Na kama ikitokea kwamba katika rasimu ya kwanza ya Katiba itakayotolewa hayatakuwepo nyinyi, wenyewe kupitia Baraza lenu muyawakilishe mapendekezo hayo kwenye tume ya mabadiliko ya katiba ili yaingizwe katika Katiba mpya,” alisisitiza.

No comments:

Post a Comment