09 September 2013

RAIS KABILA ATOA TAMKO ZITO DRC



 KINSHASA, DRC
RAIS Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), amesema hayupo tayari kuruhusu mapigano kati ya jeshi la nchi hiyo na waasi, eneo la Afrika ya Kati.Alisema mapigano hayo yanaweza kuligawa Taifa hilo ambapo jeshi la nchi hiyo litaendelea kulinda amani na kuchukua hatua kwa yeyote anayejaribu kuivuruga.

Kwa mujibu wa Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani (DW), Rais Kabila aliyasema hayo katika hotuba yake aliyoitoa mwishoni mwa wiki mjini Kinshasa wakati akifungua mkutano wa maridhiano ya kitaifa nchini humo.
Hata hivyo, mkutano huo ulisusiwa na baadhi ya vyama vya siasa kutoka upinzani ambapo mazungumzo ya amani kati ya Serikali ya Congo na waasi wa M23 yanatarajiwa kuanza leo.Hali hiyo inatokana na ongezeko la vurugu karibu na eneo la mpaka wa Congo na nchi jirani ya Rwanda ambapo kundi la M23, lilianzisha uasi Mashariki mwa Kongo na kufanikiwa kuudhibiti Mji wa Goma kwa muda mfupi

1 comment:

  1. Siri ya waasi imefichuka. Rais Kabila kaza boot. Utashinda!

    ReplyDelete