09 September 2013

WANAHABARI WASHAURIWA KUJIENDELEZA KITAALUMA


Na Grace Ndossa

WAZIRI wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, F e n e l l a Mu k a n g a r a , amewataka waandishi wa habari kujiendeleza kielimu ili sheria itakapopitishwa waweze kuwa na vigezo vinavyotakiwa.Hayo alibainisha mwishoni mwa wiki mjini Dodoma alipokuwa anazungumza na kikundi cha waandishi wa habari (Habari Group) na kueleza kuwa sheria itakuwa inawabana kama watakuwa hawajafikia vigezo.

A l i s e m a k u w a n i vyema waandishi wa habari wakaongeza elimu waliyonayo kwani walio wengi hawajafikia kiwango kitakachowekwa katika sheria ya habari."Nasisitiza mjiendeleze kielimu ili kufikia vigezo vitavyopitishwa na sheria ya habari kwani elimu ni muhimu na mjitahidi kuandika habari kwa umakini na usahihi," alisema Mukangara.

Pia alisema katika Wizara ya Habari yangu ina fursa nyingi za vijana,hivyo mnatakiwa kujitokeza na kutumia fursa zilizopo katika kujikwamua kiuchumi.Alisema vijana wanaweza kujiunga kwenye vikundi na kufika katika wizara hiyo kuelezea kitu wanachotaka k u f a n y a i l i wawe z e kusaidiwa na mikopo, kwani ipo ambayo mtu atarudisha kwa riba nafuu.Hata hivyo, alisema kuwa vijana wengi wana fursa nyingi hivyo ni muhimu wajiunge kwenye vikundi kwani fursa za kilimo kwanza zipo.

No comments:

Post a Comment