09 September 2013

MBEYA YATAJA CHANZO CHA MAPATO YAKE



 Na Rashid Mkwinda, Mbeya
AS ILIMIA 4 0 y a mapato ya Mkoa wa Mbeya yanatokana n a s h u g h u l i z a kiuchumi katika sekta za viwanda,biashara na kilimo huku asilimia 80 ya wakazi wake wakijishughulisha na kilimo cha mazao ya chakula na biashara.

Akizungumza na timu ya waandishi wa habari waliokuwa katika mafunzo ya habari za Biashara na Uchumi, Mkoa wa Mbeya, Mchumi wa Mkoa, Rukia Manduta, alisema asilimia 40 ya mapato hayo yanatokana n a uwe k e z a j i k a t i k a viwanda, madini, biashara na usafirishaji.
Alisema kuwa serikali inaendelea kuimarisha miundo mbinu katika barabara ambapo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe umeongeza chachu kwa wakulima kupata fursa ya kusafirisha mazao ya kilimo kama vile maua mboga mboga na matunda.
Alisema uwekezaji katika sekta ya utalii umeendelea kuimarika kwa Bonde la Ihefu lililopo wilayani Mbarali kuingizwa katika Hifadhi ya Taifa ilhali Ziwa Rukwa lililopo wilayani Mbozi na Chunya na Ziwa Nyasa lililopo katika wilaya ya Kyela yanasaidia pato la mkoa katika sekta ya usafirishaji na uvuvi.
Kwa upande wake Ofisa Biashara wa Mkoa wa Mbeya, Joseph Semu alizitaja baadhi ya changamoto zinazochangia kukosekana kwa wawekezaji wakubwa kuwa ni pamoja na uhaba wa maeneo na kwamba kufuatia hali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro ameunda timu ya watu sita ili kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo.
Semu alisema kuwa timu iliyoundwa na mkuu wa mkoa imechukua wataalamu kutoka Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo mkoa wa Mbeya(SIDO),TCCIA,TIC, Mhadhiri wa chuo kikuu Mzumbe, na wataalamu wawili kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa.
Awali, akizungumza na Katibu Tawala msaidizi wa Mkoa wa Mbeya, Leonard Magacha, mkufunzi wa mafunzo ya habari za Biashara na Uchumi kwa waandishi wa habari Mkoa wa Mbeya, Mnaku Mbani alisema kuwa lengo la mafunzo hayo kwa wanahabari ni kuwajengea uwezo wanahabari kuandika habari za biashara na uchumi.
Alisema fursa hiyo kwa wanahabari imelenga kuibua changamoto za kiuchumi kwa Mkoa wa Mbeya kwa nia ya kupatiwa ufumbuzi na kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo mkoani humo.

No comments:

Post a Comment