29 August 2013

MWIGULU AMVAA MBOWE,DKT. SLAA



 Goodluck Hongo na Hytham Mushi
SIKU mbili tangu kuanza kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania, Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba, ameanza kuwasha 'moto' bungeni kwa kuhoji sababu za Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Katibu wake, Dkt. Willbrod Slaa, kuendelea kuwa huru, wakati wanastahili kuwa jela kwa kusababisha mauaji ya raia.

Nchemba alitoa kauli hiyo mjini Dodoma jana wakati akiuliza swali la nyongeza. Katika swali hili mbunge huyo alihoji ni kwa nini Serikali imeshindwa kuwachukulia hatua viongzi wa vyama vya siasa wanaosababisha vurugu na mauaji ya raia.
"Ni lini Serikali itachukua hatua kwa viongozi wa vyama vya kisiasa wanaosababisha maafa ikiwemo mauaji ya Ndago, Arusha, Morogoro na Iringa, kwani kama kweli hatua zingechukuliwa basi Mbowe na Slaa sasa hivi wangekuwa tayari wako jela," alisema Mwigulu.
Kauli hiyo ilisababisha Bunge kuzizima kwa kelele kutokana na kutajwa kwa Mbowe na Dkt.Slaa. Swali hilo lilijibiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika, ambapo alisema kuwa nchi hii inaongoza kwa kufuata utawala bora.
"Katika hili kuna mihimili mitatu ya Bunge,Mahakama na Serikali Kuu, hivyo kwa hali hiyo kuna kesi ambazo zipo mahakamani, hivyo wanaiachia mahakama katika suala hilo," alisema Mkuchika.
Baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu ndipo baadhi ya wabunge walipoomba miongozo juu ya kauli mbalimbali zilizotolewa bungeni juzi na jana.
Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje (CHADEMA) aliomba mwongozo kwa Naibu Spika, Job Ndugai, akitumia kanuni ya 68 (7) ibara ya 61 na 64 kuwa inakataza kwa mbunge kutoa maneno ambayo yanamchafua mtu mwingine hivyo alimtaka Mwigulu Nchemba afute kauli yake.
"Naomba mwongozo wako kupitia ibara ya 68 (7) kanuni ya 61 na 64 ya Bunge inamzuia mbunge kutoa maneno ya kumchafua mtu mwingine kwani kuna mauaji ya aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA wilayani Arumeru kuuawa kwa kuchinjwa na mashine ya kukatia miti/magogo na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), licha ya kukamatwa watu hao, lakini pia walitoroka wakiwa na pingu mikononi hadi leo hawajulikani walipo; hivyo kwa suala hilo naomba Mwigulu Nchemba afute kauli yake," alisema Wenje.
Kufuatia hali hiyo Naibu Spika Bw.Job Ndugai alisema atalitolea ufafanuzi yeye mwenyewe baadaye kidogo.

5 comments:

  1. Mie nadhani mwigulu ni mbwia unga- muonekano wake, mwenendo wake na hata apimwapo mental scan anaonekana ameathirika sana na vitu fulani. May be huenda tatizo likawa linasababishwa na jinsi alivyowhi kuugua mwaka 2003 - 2007

    ReplyDelete
  2. Mwigulu Mchemba is good for nothing MP.

    ReplyDelete
  3. Nchemba anaficha makosa kwa kuwakosoa wasio na makosa . C CM inashindwa kupata viongozi wenye busara. Ni aibu kuongozwa kitaifa na mtu asoye na uwezo.

    ReplyDelete
  4. Kuna masuala muhimu zaidi kushughulikiwa kama migogoro na nchi jirani nilitegemea kumuona mwigulu mstari wa mbele kumshauri rais namna ya kupambana lakini mind set ya wanaccm wengi wameiweka kupambana na chadema kwa kuwa ni mafisadi hawako tayari kupoteza dola

    ReplyDelete
  5. Huyu jammaa anataka uwaziri amesahau ccm imebakiza mwaka mmoja tuizike na yeye akiwa ndani

    ReplyDelete