29 August 2013

TIMUATIMUA YAKWAMA TAZARA



 Anneth Kagenda na Salma Mzee

TARATIBU za kuanza kuwakabidhi barua za kuwaachisha kazi wafanyakazi wa Idara ya Karakana na Ujenzi katika Shirika la Reli Tanzania na Zambia (TAZARA), uliokuwa uanze jana, umekwama kwa sababu ambazo hazikujulikana mara moja
.B a r u a z a wa f a n y a k a z i walioachishwa kazi zilikuwa zianze kukabidhiwa jana mchana, lakini muda huo ulipofika ilitolewa taarifa kuwa utaratibu huo umeahirishwa kwa kile kilichoelezwa kuwa mhusika alipigiwa simu ili asitishe hatua.

Hali hiyo ilijitokeza makao makuu ya TAZARA, Dar es Salaam jana, hatua iliyosababisha wafanyakazi hao kuanza kuimba nyimbo za kejeli zenye ujumbe kuwa menejimenti inawaogopa kuwapa barua za kuwaachisha kazi.

Uamuzi wa kuwaachisha wafanyakazi 1,067 ulifikiwa juzi ukihusisha wafanyakazi mbalimbali kutoka vitengo sita katika shirika hilo, lakini waliotangazwa kwenye awamu ya kwanza ya kukabidhiwa barua walikuwa wafanyakazi wa vitengo vya karakana na ujenzi.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli Tanzania ( T R AW U ) , Ya s i n M l e k e , aliwaambia waandishi wa habari kuwa wafanyakazi wa vitengo vinne, kati ya sita walikuwa hawajatangaziwa uamuzi wa kupewa barua

No comments:

Post a Comment