- WENGINE 11 HOI,WAVUNJIKA MIKONO,NYONGA
Suleiman Abeid, Shinyanga na Faida Muyumba, Geita
WATU 13 wamekufa na wengine 11
kujeruhiwa vibaya katika ajali iliyotokea saa 2.30 usiku wa kuamkia jana baada
ya gari dogo aina ya Hiace kugonga kwa nyuma gari aina ya Scania lililokuwa
limeharibika na kuegeshwa pembeni mwa barabara.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kihenya Kihenya,
alisema ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Ngogwa wilayani Kahama wakati
gari hilo dogo
la abiria namba T. 756 CHX likitokea mjini Kahama kwenda katika mji wa
Ushirombo wilayani Bukombe mkoa wa Geita.Alisema lilipofika eneo hilo ndipo lilipogonga kwa nyuma lori hilo namba T. 999 AMS.
Kihenya alisema kuwa katika ajali hiyo
jumla ya watu 11 walifariki eneo la ajali akiwemo mtoto mchanga wa miezi saba.
Aliongeza kuwa wengine wawili walifariki wakati wakipatiwa matibabu katika
Hospitali ya Serikali wilayani Kahama.Kamanda huyo alisema mpaka jana mchana
maiti saba zilikuwa zimetambuliwa ambao ni pamoja na mtoto mwenye umri wa miaka
saba aliyetambuliwa kwa jina la Kasandu Jumanne mkazi wa Mwanza, Masanja
Matogolo (Kahama) na David Charles (Masumbwe, Bukombe).
Wengine waliotambuliwa jana ni Regina
John (Rorya), Ezekiel Mnyiko, ambaye alikuwa dereva wa Hiace na Peter Daud
(wote wakazi wa Ushirombo) na Mlekwa Mguhati (Masumbwe).Kihenya alisema polisi wanaendelea na
uchunguzi ili kubaini chanzo cha ajali hiyo. Hata hivyo alisema huenda
ilisababishwa na mwendo kasi na uzembe wa dereva kutokuwa makini barabarani.
Alisema hali za majeruhi ni mbaya na
taratibu zilikuwa zinafanyika ili kuwahamishia Hospitali ya RufaaBugando
mkoani Mwanza, huku majeruhi 9 hali zao zikiendelea vizuri. Al i s ema ma j e r
u h i we n g i wamevunjika mikono na nyonga.Kwa upande mwingine Kaimu Kamanda huyo aliwashukuru wakazi wa Kijiji cha
Ngongwa kutokana na ushirikiano wao waliouonesha kwa jeshi hilo mara baada ya kutokea ajali hiyo na
kutoa mwito kwa wananchi kufika katika hospitali ya serikali mjini Kahama ili
kuweza kutambua maiti zilizohifadhiwa katika hospitali hiyo.
No comments:
Post a Comment