07 November 2013

WADAU WATAKIWA KUIPA SAPOTI THE TANZANITE



 Na Fatuma Rashid
  Wadau wa michezo nchini, wametakiwa kujitokeza kuisaidia timu ya taifa ya vijana ya mpira wa miguu ya wanawake (The Tanzanite), ili iweze kufika mbali zaidi.

  Timu hiyo inakabiliwa na mechi ya marudiano ya kusaka tiketi kucheza Kombe la Dunia la vijana kwa wanawake, dhidi ya Msumbiji wikiendi ambapo katika mechi ya awali iliyochezwa wiki mbili zilizopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ilishinda mabao 10-0.
  Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wachezaji wa The Tanzanite, wakati wa kuiaga timu hiyo iliyoondoka jana kwenda Msumbiji Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo, Juliana Yasoda alisema timu hiyo inahitaji nguvu za ziada kutoka kwa wadau mbalimbali, ambao wataisaidia kufika mbali zaidi.
Yasoda alisema timu hiyo itazidi kusonga mbele kama wadau hao, watajitokeza kuipa sapoti katika michuano mbalimbali.
  Kwa upande wake Kocha Mkuu wa timu hiyo, Rogasian Kaijage alisema kikosi chake kipo imara kwa ajili ya mpambano na watajitahidi kufanya vizuri zaidi ya mechi iliyopita.Kaijage alisema Watanzania wanatakiwa kuiangalia timu hiyo kwa mtazamo tofauti, kwani hivi sasa anaiandaa ili kukuza soka la wanawake nchini.
  “Hii ni timu ambayo inatakiwa kutazamwa kwa mbali zaidi, kwani lengo hasa si kwa miaka ya sasa bali ni kuunda soka la wanawake ambalo litaitangaza Tanzania katika ramani ya Dunia hapo baadaye,” alisema.
   Alisema kuchelewa kwa wachezaji wanne watakaoungana na wenzao kesho mara baada ya kumaliza mitihani ya kidato cha nne, haitaathiri kitu kwani watafika ikiwa bado muda wa michuano na pia kama itatokea dharura ambayo itawalazimu kuchelewa zaidi basi kuna wachezaji wengine ambao pia wanauwezo

No comments:

Post a Comment