07 November 2013

LIEWIG AIKAMUA SIMBA



Na Mwandishi Wetu
  Kocha raia wa Ufaransa aliyefurushwa Simba msimu uliopita, Patrick Liewig hatimaye jana amelipwa nusu ya fedha anazoidai klabu hiyo.

  Simba imemlipa kocha huyo dola 10,000 za Marekani kati ya dola18,000 alizokuwa anaidai ambazo imeahidi kuzilipa wakati mwingine. Kocha huyo anaidai Simba fedha hizo kwa ajili ya kuifundisha timu hiyo kuanzia Januari hadi Mei mwaka huu, ambapo nafasi yake imezibwa na Mzalendo Abdallah ‘King’ Kibadeni.
  Akizungumza mara baada ya kumkabidhi fedha hizo Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang are Kinesi alisema kocha huyo atalipwa fedha nyingine leo kiasi cha dola 3,000 na nyingine atalipwa mwakani ambazo ni dola 5,000.
   Kocha huyo ambaye alikuwa akiidai Simba dola 26,000 tayari alishalipwa dola 10,000 Juni mwaka huu. Liewig alikuwa anadai dola 12,000 za mshahara wake na dola 12,000 kwa ajili ya kuvunjiwa mkataba wake na dola 2,000 za tiketi za kwenda kwao Ufaransa.Liewig aliiongoza Simba katika mechi 25 ambapo kati ya hizo ishinda tisa, sare nane na kufungwa saba.

No comments:

Post a Comment