11 September 2013

Z'BAR TUSILAUMIWE

  • ZMA YATOA TAMKO ZITO,YAKIRI KUISAJILI


 Na Mwajuma Juma, Zanzibar
MKURUGENZI wa Mamlaka ya Usafiri wa Baharini Zanzibar (ZMA), Bw. Abeid Omar Maalim, amesema Zanzibar haipaswi kulaumiwa kutokana na tukio la kukamatwa kwa meli ambayo ilibeba shehena ya bangi nchini Italia.

Bw. Maalim aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari Zanzibar katika kumbukumbu ya kutimiza miaka miwili tangu kuzama kwa meli ya Mv Spice Islander.
Alisema meli hiyo ambayo inamilikiwa na Kampuni ya Gold
Star, iliyopo kwenye Visiwa vya Marshal, Amerika ya Kusini ilisajiliwa Zanzibar mwaka 2011 ambapo usajili huo hauna maana kuwa Zanzibar inahusika na tukio hilo.
"Kweli meli hii ilisajiliwa Zanzibar, jambo la msingi ni kuangalia bangi iliyokamatwa ilipakiwa wapi na nani anahusika na biashara hiyo," alisema Bw. Maalim.
Aliongeza kuwa, kama itabainika mmiliki wa meli hiyo anahusika moja kwa moja na usafirishaji huo, ZMA haitasita kuchukua hatua za kufuta usajili na kuangalia sheria nyingine.
"Kwa mujibu wa sheria za usajili wa meli, kuna kipengele ambacho mmiliki anajifunga kwa kusema meli yake haitasafirisha biashara haramu ikiwemo ya dawa za kulevya, ikibainika kafanya hivyo meli yake itafutiwa usajili," alisema.

2 comments:

  1. NI KWELI NI KUKURUPUKA KUILAUMU ZENJI KWA KUKAMATWA KWA MELI HIYO, MELI NYINGI ZA NCHI MBALI MBALI HUKAMATWA NA MIZIGO HARAMU LAKINI MUHIMU NI MZIGO WA NANI SI MELI IMESAJILIWA WAPI

    ReplyDelete
  2. Tatizo hapa ni kwamba katika usajili huu;si kwamba jina la Zanzibar ndiyo lilotumika ila ni jina la Tanzania na hivyo kimataifa jina lote la Tanzania limechafuka.

    Kwa mantiki hiyo inamaana sisi Tanzania bara nasi tumechafuka wakati sisi hata huo usajili hatukuufanya ila Ulifanywa na Zanzibar.

    Hizi ndiyo kasoro za Muungano; ifike wakati kila mtu abebe mzigo wake;kama ni kusajili meli za madawa ya kulevya basi kila mtu asajili kwa jina lake mfano Tanganyika au Zanzibar ili ile adha ya kuchafuka jina kama inatokea iwe yako wewe peke yako pasipo kuwachafua na watu wengine wasio husika.Hii ndiyo hoja ya msingi hapa.

    Shabani Hamis/mzee wa kugegeda

    ReplyDelete