09 September 2013

EPZA YAAHIDI KUVUTIA UWEKEZAJI



 Na Mwandishi Wetu
UO N G O Z I w a Mamlaka ya Ukanda M a a l u m u w a Uwekezaji (EPZA) ume s ema u t a e n d e l e a kutekeleza mpango wa Serikali wa maendeleo wa miaka mitano kwa kuhakikisha inaendelea kuweka mazingira ya kuvutia wawekezaji katika sekta ya viwanda ili kuharakisha shughuli za maendeleo nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa EPZA, Dkt. Adelhelm Meru, alibainisha hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam hivi karibuni, ambapo alifafanua maendeleo ya miradi na uwekezaji katika ukanda huo kwa miaka sita iliyopita.Alisema EPZA inaweka nguvu kubwa kwenye maendeleo ya viwanda kwa kuwa sekta hiyo ni msingi mkubwa wa maendeleo ya nchi yoyote duniani na kwamba Tanzania haiwezi kuachwa nyuma kwa hilo kama kweli inataka kupata maendeleo endelevu.
"Historia ni shahidi kuwa viwanda ndiyo moja ya misingi muhimu ya maendeleo," alisema na kuongeza kuwa ndiyo maana taasisi yake inafanya kila linalowezekana kuhakikisha sekta hiyo inakua hapa nchini.
"Taasisi hii inatekeleza kwa vitendo mpango huo wa maendeleo na tumedhamiria kuongeza nguvu zaidi," alisema.A l i s e m a m o j a y a vipaumbele vya mpango wa maendeleo wa miaka mitano ni maendeleo ya viwanda na kuwa EPZA inataka kuhakikisha kuwa hilo linafanikiwa kwa faida ya nchi nzima.
"Tunaunga mkono mpango wa maendeleo wa miaka mitano, tumedhamiria kufanikiwa katika hili," alisema. Alisema kuwa kuimarika kwa sekta ya viwanda nchini kutasaidia kuzalisha ajira mpya, upatikanaji wa teknolojia mpya na kuongeza kipato cha nchi hivyo kukuza uchumi na ustawi wa jamii.
Alisema kwa kutambua umuhimu wa sekta ya viwanda katika kuzalisha ajira na kukuza uchumi wa nchi, taasisi yake imejikita kuvutia wawekezaji wa ndani na nje katika sekta hiyo ili kunufaika na fursa hizo.
Awali, alisema kuwa mpaka sasa wastani wa viwanda vilivyowekeza kupitia

No comments:

Post a Comment