24 September 2013

BRANDTS: HATUKUSTAHILI KUFUNGWA NA AZAM FC



  •  SASA HASIRA ZAO KUMALIZIA KWA RUVU SHOOTING J'MOSI

 Na Elizabeth Mayemba
  Kocha Mkuu wa Yanga, Ernest Brandts amesema kuwa umakini mdogo wa mabeki wake ndio uliowafanya wapoteze mchezo wa juzi dhidi ya Azam FC ,baada ya kufungwa mabao 3-2 mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Akizungumz a Da r e s Salaam jana, Brandts alisema katika mchezo huo timu yake ilicheza vizuri dakika zote 90, lakini kukosa umakini ndio kulisababisha matokeo yaishe vile. 
"Wachezaji wangu walicheza vizuri dakika zote 90, lakini Azam FC walitumia kasoro yetu kidogo na kuondoka na ushindi katika mchezo huo, hivyo wachezaji wangu wanatakiwa kujipanga upya," alisema Brandts.
Alisema sasa hivi anaangalia mechi ijayo dhidi ya Ruvu Shooting itakayochezwa J umamosi ijayo , hivyo watahakikisha wanaondoka na pointi zote tatu ili kujiweka katika mazingira mazuri katika kampeni zao za kutetea ubingwa wao.
  Kocha huyo alisema mechi na Azam imeshakwisha sasa wanachotakiwa kuangalia ni mechi inayokuja, hivyo wachezaji wake wanatakiwa kurekebisha kasoro zilizopita ili wapate ushindi mechi ijayo.
  Ukiacha mabeki, pia kocha huyo amelia na safu yake ya ushambuliaji kuwa walipata nafasi nyingi za kufunga lakini walishindwa kufanya hivyo na kuwataka wajirekebishe mechi ijayo.
  Kwa upande wa kocha wa Azam FC Stewart Hall alisema kuwa, wapinzani wao Yanga waliwazidi kila idara na wao wameshindia bahati tu. "Ile mechi Yanga ndio waliostahili ushindi lakini wachezaji wangu walitumia makosa kidogo yaliyofanywa na wachezaji wa Yanga na wao kufunga mabao," alisema Hall.

No comments:

Post a Comment