24 September 2013

YANGA, AZAM WAINGIZA MIL.138/-



 Na Mwandishi Wetu

  Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya wenyeji Azam FC na Yanga lililochezwa juzi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, limeingiza sh. 138,188,000 
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema watazamaji waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 33 la VPL msimu wa 2013/14 lililomalizika kwa Azam kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 walikuwa 24,020
. Alisema viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 33,065,409.1 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 21,079,525.42.
  "Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 16,812,919.89, tiketi sh. 5,022,342, gharama za mechi sh. 10,087,751.93, Kamati ya Ligi sh. 10,087,751.93, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 5,043,875.97 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 3,923,014.64," alisema Wambura.
  Alisema mechi iliyopita ya VPL kwenye uwanja huo kati ya Simba na Mbeya City iliingiza sh. 123,971,000.
Wakati huo huo, mechi namba 12 ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya Toto Africans na Polisi Dodoma iliyokuwa ichezwe Jumamosi ijayo Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza imesogezwa mbele kwa siku moja.
   Timu hizo za kundi C sasa zitapambana Jumapili kwenye uwanja huo huo ili kupisha mechi namba 10 kati ya Pamba na Stand United FC ya Shinyanga itakayochezwa Jumamosi (Septemba 28 mwaka huu).
    Mechi nyingine za kundi hilo zitakazochezwa Jumamosi ni Mwadui na Polisi Tabora (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga) wakati Kanembwa JKT na Polisi Mara zitacheza kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigom

No comments:

Post a Comment