07 August 2013

USAJILI LIGI KUU WAKAMILIKA


 Na Mosi Mrisho
HATUA ya kwanza ya usajili wa wachezaji kwa msimu wa 2013/2014 imefungwa rasmi juzi, ambapo klabu zote za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zimewasilisha usajili wa vikosi vyao ndani ya wakati.Akizungumza Dar es Salaam jana Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema baadhi ya klabu zimefanya makosa madogo madogo katika usajili ambapo zilipewa jana kufanyia marekebisho kasoro hizo
.Alisema leo majina ya vikosi vyote yatabandikwa kwenye mbao za matangazo za TFF kwa ajili ya kipindi cha pingamizi kitakachomalizika Agosti 12 mwaka huu.Ofisa huyo alisema Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake, Alex Mgongolwa itakutana Agosti 13 na 14 mwaka huu kupitia na kufanyia uamuzi usajili wa wachezaji wenye matatizo.
"Hatua ya pili ya usajili itaanza tena Agosti 14, mwaka huu ikihusisha wachezaji ambao watakuwa hawajasajiliwa katika Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu na wale kutoka nje ya Tanzania."Hivyo, dirisha la uhamisho kwa wachezaji wa kimataifa litafungwa baada ya hatua ya pili ya usajili kumalizika Agosti 29, mwaka huu," alisema Wambura.

No comments:

Post a Comment