Na Nasra Kitana
KLABU ya Coastal
Union imefanikiwa kuipata saini ya kifaa cha timu ya Mamlaka ya Mapato ya
Uganda (URA), Yayo Kato ambaye alizisumbua Simba na Yanga katika mechi za
kirafiki zilizopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Timu hiyo
ilipata nafasi ya kucheza na URA katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga katika
mechi kali na kuifunga bao 1-0
Akizungumza na
mwandishi wa habari hizi Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Khasim El Siagi alisema
wamemsajili mshabmbnuliaji huyo baada ya kuvutiwa na uchezaji wake wakati timu
yake ya URA ilipokuja kucheza nchini.Alisema
kusajiliwa kwa mchezaji huyo kunaifanya timu yake kuwa na wachezaji wawili wa
kigeni akiwemo raia wa Kenya Jerry Santo, ambaye yupo tangu msimu uliopita.
"Tulivutiwa na mchezaji huyo baada ya
kumuona alivyocheza vizuri katika mechi za Simba na Yanga, na kuona anatufaa na
kuanza kumfuatili ili kupata saini yake," alisema.giAlisema msimu huu wameamu kujipanga
kiushindani na ndiyo maana wamefanya usajili wa umakini, lengo likiwa kupata
nafasi za kuiwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa.
Siagi alisema usajili wa mchezaji huyo,
ndiyo wa mwisho na wana uhakika atakuwa msaada mkubwa kwao akishirikiana na
wachezaji aliowakuta.Licha ya mchezaji huyo raia wa Uganda, Coastal
Union pia imesajili wachezaji nyota Uhuru Selemani, Haruna Moshi 'Boban' na
beki Juma Nyoso waliotokea Simba
No comments:
Post a Comment