28 August 2013

UKWELI NA UWAZI : WALIONASWA NA 'UNGA' WATAJWA

  • WAPO WATANZANIA,RAIA WA MATAIFA MENGINE

 Na Mwandishi Wetu
WAKATI Serikali ikiendelea k u u s a k a m t a n d a o unaofanya biashara ya dawa za kulevya nchini, Jeshi la Polisi Kitengo cha Kupambana na Kuzuia Dawa za Kulevya nchini, limekiri kuwanasa zaidi ya watu 100 waliokuwa na dawa za kulevya na kesi zao zinaendelea mahakamani.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu, akitokea mkoani Dodoma, Mkuu wa kitengo hicho, Kamishna Msaidizi (ACP), Godfrey Nzowa, alisema kati ya watu hao, baadhi yao kesi zao zipo Mahakama Kuu.
A l i s ema k w a k a w a i d a watuhumiwa wanapokamatwa na dawa hizo, hufunguliwa mbele ya mashahidi akiwepo mtuhumiwa mwenyewe ili kuthibitisha na baadaye kupelekwa mahakamani kama kielelezo na mahakama hupata fursa ya kuzifungua na kuziangalia kama ndizo zenyewe.
"Wakati kesi ikiendelea, dawa hizo huhifadhiwa ambapo kesi ikimalizika na kutolewa hukumu, ma h a k ama h u t o a amr i y a kuteketezwa ambapo mwaka 2012, Mahakama Kuu iliteketeza kilo 92.
Kamishna Nzowa alikwenda mbali zaidi na kuweka wazi takwimu za watuhumiwa waliokamatwa na dawa hizo kuanzia mwaka 2009 hadi Mei mwaka huu na kudai kuwa, hadi sasa zaidi ya kilo 841.3 za cocaine, 175.64 za heroine na 10.8 (bangi), zimekamatwa.
Orodha ya majina ya watuhumiwa na dawa walizokamatwa nazo kwenye mabano ni pamoja na Steven Gwaza, (heroin gramu 825.7), Rebecca Wairimu Mwangi (heroine gram 1,800), Khatibu Bakari Khatibu na Khalid Salim Maunga (cocaine gramu 1,007.4).
Wengine Dhoulkefly Awadh (cocaine gramu 893.58), Abdallah Pashua Kipevu (heroine gramu 31,000), Diaka Brama Kaba (heroin gramu 31,000), ambaye alikamatwa akiwa na wenzake Ndjane Abubakar, Sylivia Kaaya Namirembe, Farid Kisuule, Robinson Dumba Teise na Ismail Mugabi.
Wengine ni Rashid Salim Mohamed, (cocaine gramu 1,374.32), Mini Thabo Hamza (cocaine gramu 1,595.74), Hamis Mohamed Mtou (cocaine gramu 850), Kwako Sarfo, Mnigeria (cocaine gramu 1,1951.80), Mustapha Musa (cocaine gramu 286), aliyekuwa na Aman Saidfadhil Daruweshi na Afshin Jalal.
Jack Vuyo, (heroine gramu 42,000) huyu alikuwa na Anastazia Elizabeth Cloete, Simon Eugenio Fadu(cocaine gramu 8,000), Assad Aziz, (heroine gramu 50,000), alikuwa na Isamil Shebe Ismail, Rashid Salim na Majed Gholamghader.
Anna Jamaniste Mboya, (cocaine gramu 1,140), Fredy William Chonde (heroine gramu 175,000), Kambi Zuber, Abdul Ghan na Shahbaz Malik, Livinus Malik (Wapakistani) waliokamatwa na (cocaine gramu 804.7).Chukwudu Denis Okechukwu, Paulo Ekechukwu na Hycenth Stan (Wanigeria) (cocaine gramu 81,000).Shoaib S.O. Mohammed, Fedro Alfredo Chongo, (cocaine gramu 1,530).
Kadiria Said Kimaro (heroine gramu 1,365.91), Abdallah Rajab Mwalimu (cocaine gramu 716.5), Mwiteka Godfrey Mwandemele (cocaine gramu 1,112), Abbas Kondo Gede (cocaine gramu 1,112), Mwanaidi Ramadhan Mfundo (cocaine gramu 5,000), ambaye alikuwa na Sarah David Munuo.
Antony Karanja, Benny Ngare, Almasi Hamis Said, Yahya Haroun Ibrahim, Aisha Said Kungwi, Rajab Juma Mzome na John William Mwakalasya, Ally Mirzai Pirbakhshi (cocaine gramu 97,000) alikuwa na Aziz Juma Kizingiti, Said Mashaka Mrisho, Abdulahman Mtumwa na Hamidu Kitwana Karimu.
Ramadhan Athuman (heroine gramu 3,000) alikuwa na Rashid Mohammed, Ally Mohammed Kichaa na Issa Abdulrahman.
Rashid Ally Mtopea (heroin gramu 12,000) alikuwa na Idd Adam Mwaduga, Nurdin Adam, Maurine Amatus Lyumba, John Adams Igwenma wa (Mnaijeria) ( cocaine gramu 830.19). Upendo Mohammed Cheusi, Abdallah Omar Salum (cannabis sativa gramu 1,000) alikuwa na Cosmos Chukwumezie, Ifeanyi Malven Kalu Oko (Wanaijeria) (heroin gramu 3,185.38), Allan Duller (cocaine gramu 3,882.92), Alberto Mendes kutoka Ghana, (gramu 1,277.10 za heroine)
Wengine ni Joseph Chukwumeka Nwabunwanne ambaye ni raia wa Nigeria, (gramu 1,245.96 za heroin) Kwaku Safo Brobbey Mghana (gramu 13,781.78 za heroine), Princewill Ejike Mnigeria (gramu 981.12 za heroin), Mary Mvula Mzambia (gramu 391.51 za cocaine), Waziri Shaban Mizongi, (gramu 2,013 za heroine) akiwa na Santos Joseph Mpondela, Kelvin Kelven Mwazeni.
Wengine ni Emmanuela Adam, Mghana (gramu 9,838.1 za cocaine), Asha Omary Ramadhan, (gramu 1.56), Mariam Mohammed Said, (gramu 9,857.54 za bangi) akiwa na Abdullatif A. Fundikira.Aliendelea kuwataja Marceline Koivogui, Mghana (gramu 1,073.82 za heroin), Edwin Cheleh Swen Mliberia (gramu 1,509.35 za heroin), akiwa na Benjamin Obioma Onuorah wa Nigeria, Sofia Seif Kingazi, (gramu 3,379.54 za cocaine) na Josephine Mumbi Waithera Mkenya (gramu 3,249.82 za cocaine).
Iddi Juma Mfaume,(gramu 563.25 za heroine), Amina Kassim Ramadhani,(gramu 1,980.11 za heroine) na Vivian Edigin Mnigeria (gramu 797.56 za cocaine), Hadija Tambwe, (gramu 33,507.04 Za cannabis), Sasha Farhan na Mnyeke Sativa, na Mychel Andriand Takahindangeng Muindonesia, gramu 3,932.44 za cocaine).
We n g i n e n i K r i s t i n a Biskavevskaja Mluthenia (gramu 4,000 za cocaine), Stephen Basil Ojiofor Mnigeri (gramu 1,173 za cocaine), Judith Marko Kusekwa, (gramu 1,793 za heroine), Khamis Said Bakari (gramu 1,793 za heroine).Kundi la mwisho ni Tabia Omary au Neema Omary (gramu 994.97 za heroine), Masesa au Habiba Andrew Joseph, (gramu 1,037.9 za heroin). Hivi karibuni Agness Gerald "Masogange" na mwenzake walikamatwa Afrika Kusini wakiwa na kilo 150 za dawa hizo.
Akizungumzia sakata la Mtanzania anayedaiwa kukamatwa Mjini Dubai, Falma za Kiarabu, juzi akiwa na kilo tatu ya dawa za kulevya aina ya cocaine, alisema yupo safarini hivyo suala hilo atalitolea ufafanuzi leo baada ya kufika ofisini.
Dawa hizo zinadaiwa kuwa na thamani ya Diraham milioni tatu, (sawa na sh. bilioni 1,321.7 za Kitanzania).Kwa mujibu wa mtandao wa Yahoo News, ambao haujataja jina la mwanamke huyo, ulisema dawa hizo ziliwekwa kwenye mabegi na baada ya kuhojiwa na Maofisa Usalama wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Mjini Dubai, alidai kuwekewa dawa hizo na rafiki wa mumewe nchini Brazil (hakutajwa jina).
"Mume wangu kupitia rafiki yake, aliamua kunitumia kama punda niweze kuyabeba mabegi haya kwa kuyarudisha nyumbani Tanzania," alisema mwanamke huyo wakati akihojiwa na Ofisa mmoja wa Polisi Mjini Dubai.
Kwa mujibu wa mtandao huo, mwanamke huyo alikamatwa juzi akiwa katika harakati za kurejea Tanzania wakati akitoka mapumziko nchini Brazil ambapo mumewe alimpa nafasi ya kwenda likizo ya miezi mitatu ili akapumzike."Wa k a t i n i k iwa k a t i k a mapumziko nchini Brazil, rafiki wa mumewe alinipa haya mabegi niweze kurejea nayo Tanzania," alidai mwanamke huyo wakati akihojiwa na kuongeza kuwa;
"Mume wangu amenisababishia matatizo kwa kunipa nafasi ya kupumzika miezi mitatu nchini Brazil," aliongeza.Hata hivyo, mtandao huo ulidai mtuhumiwa huyo amepelekwa katika Mahakama ya Umma ili taratibu za kisheria ziweze kuchukua mkondo wake.

5 comments:

  1. Watakao kamatwa siku zote ni wale wanaotumiwa. Wanaowatuma, ambao ni mafisadi papa hata siku moja hawatakamatwa maana wanajuana na mtandao wa maofisa hao wa vyombo vya dola wanaofanya nao hizo dili.

    ReplyDelete
  2. hawa watu pichazo zingewekwa pia, ingekuwa poa sana kwani unaweza kuta hapa anajina hilo lakini kitaa anatumia jingine pia hata watu wangeweza saidia huenda anawatu wa karibu nao wangechunguzwa pia.

    Na hayo majina ni ya mwaka huu tu au toka enzi ya nyerere yakawa bado yanafanyiwa kazi

    ReplyDelete
    Replies
    1. Acheni kuwaumiza njaa kali wakati wenye biashara hizo wapo wametuli wakisema. "jamani tule pozi kidogo hali sio shwari sana kisha tutaendelea"

      Delete
  3. hakuna kitu hapo . hayo majina feki wameweka tu ili serikali isifikirie mbali , ikea kupanga mikakati juu ya hii orodha feki.

    Watanzania wa lei si wa jana . hatudanganyiiiiiiki

    ReplyDelete
  4. JE KULE MEXCO ,VENEZUELA NA AFRIGHANSTAN WANAFANYA NI DAGAA TANZANIA KILA MTU NI POLISI,HAKIMU NA JESHILA MAGEREZA

    ReplyDelete