20 August 2013

TBL YAZINDUA MPANGO WA HAKATWI MTU



Na Mwandishi Wetu
KATIKA kile kinachoonekana kusogeza huduma bora zaidi kwa wananchi na kutambuaumuhimu wa afya zao, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia vinywaji vya Grand Malt na Vita Malt imezindua kampenimaalumu iitwayo ‘Nyumbani Ni Nyumbani’ kwa ajili ya kupeleka bidhaa hizo zisizo na kilevi kwa Watanzania wote. Akizindua kampeni jijini Dar esSalaam jana, 

Meneja Bidhaa zisizo na vileo wa TBL, Consolata Adam alisema, wamezindua kampeni hiyo maalumu ili kuhakikisha vinywaji visivyo na kilevi vinamfi kia kila mtu. "Tumeamua kuzindua kampeni hii ili kuhakikisha kila Mtanzania anafahamu umuhimu wa vinywaji vya Grandmalt na Vitamalt katika matumizi ya kutunza na kulinda afya zao. 
"Kampeni hii itahusisha mabalozi wa Grand Malt na Vita Malt kwa pamoja kutembea nyumba kwa nyumba na kuhakikisha ujumbe huu unamfi kia kila mtu katika nyumba yake ambapo pia kutakuwa na fursa ya kujishindia na kuzawadiwa zawadi mbalimbali wakati wa kampeni hiyo," alisema. Consolata alisema, vinywaji hivyo ni vizuri zaidi kwa afya ya mwanadamu kwani vimetengenezwa vikiwa na virutubisho vya kila aina na vinafaa mno hata kwa mama mjamzito.
 " Tu n a omb a Wa t a n z a n i a wasishangae pale watakapokutana na watu wetu ambao watakuwa wanawatembelea majumbani kwao, kwani lengo ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata fursa ya kutambua faida za kutumia kinywaji cha Grand Malt na Vita Malt katika kulinda afya yake ili tuweze kujenga desturi ya kuwa na matumizi bora kwa ajili ya kujenga afya zetu, alisema.
 Naye Ofi sa Uhusiano wa TBL,Doris Malulu alisema hii ni kampeni ya kwanza kuzinduliwa na vinywaji hivyo kwa lengo moja la kuwawezesha Watanzania kutumia bidhaa hizo zenye faida kubwa kwa mwili wa mwanadamu. "Tunataka vinywaji hivi vipatikane kila mahali na pia kuwasaidia Watanzania umuhimu wa kuvitumia kwani vina faida kubwa kwa wote, kuanzia hata kwa mtoto," alisema Doris. Kampeni hiyo ya Nyumbanini Nyumbani inatarajiwa kuanza katika Mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Kilimanjaro, Mtwa r a , Do d oma , I r i n g a ,Morogoro, Mbeya na Shinyangaambapo itaanzia mji wa Kahama.Vinywaji vya Grand Malt na Vita Malt ambavyo havina kilevi vinazalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

No comments:

Post a Comment