Rachel Balama na Anneth Kagenda
SIKU
chache baada ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini kudai jeraha
alilonalo katika bega la kulia limetokana na risasi aliyopigwa na polisi mkoani
Morogoro, baadhi ya Waislamu nchini wametoa tamko la kumtaka Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi, ajiuzulu mara moja.
Msimamo huo
umetolewa Dar es Salaam jana katika kongamano la Waislamu ambalo lilifanyika
katika Uwanja wa Mwembe Yanga.Akizungumza
katika kongamano hilo ambalo lilihudhuriwa na mamia ya waumini wa dini hiyo,
mmoja wa viongozi wa jumuiya hiyo Shekhe Kondo Juma Bungo, alisema Waislamu
wanatoa muda kwa Dkt. Nchimbi kujiondoa katika nafasi hiyo.
Alisema, mbali
na Dkt. Nchimbi, walisema Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Faustine
Shilogile, anapaswa kukamatwa na kufikishwa mahakamani wakidai ndiye mhusika
mkuu wa kupanga mikakati ya kumdhuru Shekhe Ponda.“Askari
aliyempiga risasi Shekhe Ponda na Kamanda ambaye alisimamia suala zima la
uvamizi kwa kiongozi wetu, wote wanapaswa kuwajibishwa... tunataka iundwe tume
huru ya uchunguzi badala ya timu iliyoundwa na polisi,” alisema.
Al i o n g e z
a k uwa , k ama maazimio hayo yatapuuzwa na wahusika pamoja na Serikali
kushindwa kuchukua hatua stahiki, itakuwa mwanzo na mwisho wa historia ya
Tanzania.
“Kitakachotokea
baada ya hapo, Serikali itaona mwanzo tu lakini haitajua mwisho wake...Waislamu nchi nzima
watafanya maandamano, polisi wanategemea kupandishwa vyeo au kupewa posho
nyingi pale yanapotokea matatizo ya Waislamu.
“Kwa sasa hali
inavyoonesha watapandishwa vyeo kwa uchungu kwani Waislamu hatutakubali,”
alisema Shekhe Bungo na kusisitiza kuwa, Shekhe Ponda ana thamani kubwa sana
kwa Waislamu.
Shekhe Bungo alilihadharisha Jeshi la
Polisi kuacha kuwatisha
Waislamu na kuongeza kuwa, Serikali
isije kuwalaumu kwa kitakachotokea kama madai yao hayatatekelezwa.
Aliwataka Waislamu popote walipo, kutoa
adhabu palevion gozi au wanachama wa Cha maChaMapinduzi (CCM),wa
napoingiamisikitinina kufan yakampeni zakuombawachaguliwe katika uc haguzi uja
o.
Tamko la
CUF
Katikahatuanyingine,
Chamacha Wana nchi (C UF), kimelitaka Jeshila Polis inchin i,limuach ie Shekh
eP ondaa wezeku endeleanamatibab ukatika Taasisi ya Tiba ya Mifupa(M OI).
Chama hicho kimese ma kite ndoalichofanyiwaS
hekhePondacha kuon dolewaMOI wakat ih ali yakekiafya ha ijatengemaa,s
ichakibinadamubal ich akinyam a.
Mwenyek itiw ac hamahicho Taifa,Pro
fesaIbrahim Lipum ba, aliyase mahayo Dar esS alaamjanawak ati akizungumza na
waandishi wahabari.
"Kaulizaviti shonaub abeunaofany
wa naKam an dawa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman
Kova, vinachochea hasira na jazba za wananchi wengine wakiamini kuwa, jeshi
hilo lina lengo la kumuua Shekhe Ponda badala ya polisi kujenga amani, wao wanaibomoa,"
alisema.
Prof. Lipumba alisema, jeshi hilo
limeshindwa kufanya kazi kwa weledi ndio sababu ya kuongezeka vitendo vya
uhalifu na tuhuma nyingi kwa baadhi ya polisi ambao wanashirikiana na wahalifu.
"Polisi wetu wameweka pembeni kazi
yao ya kupambana na uhalifu... wanapoteza wakati mwingi na raslimali
kumshughulikia Shekhe Ponda hivyo nawaomba Watanzania wote tudai jeshii lenye
weledi na linalowajibika," alisema.
Alisema CUF kinaungana na Watanzania
wote kulaani vikali kitendo alichofanyiwa Shekhe Ponda, kumfungulia mashtaka na
kumuondoa MOI alipokuwa akipatiwa matibabu bila taarifa na kumpeleka gerezani
Segerea.
Aliongeza kuwa, jeshi hilo ndio chanzo
cha wananchi kuvunja amani ya nchi ambapo juzi mchana, alikwenda Segerea
kumuona Shekhe Ponda ambapo Mkuu wa gereza hilo alimpa ushirikiano mzuri
uliofanikisha amuone na kuzungumza naye.
" Ta y a r i S h e k h e P o n d a
amepelekewa dawa zake gerezani na amepewa huduma za tiba zinazoweza kupatikana
katika gereza hilo," alisema Prof. Lipumba na kuongeza kuwa, taarifa
alizonazo X-ray imeonesha risasi aliyopigwa imepita karibu na mfupa
ambao umepasuka.
Alisema hali ya Shekhe Ponda inaendelea
vizuri ukilinganisha naawal i baad ayaku fikishwa ger ezanikwanian awe
zakutembeamwenyewe, anafahamu kamili na waliweza kutaniana na mkuu wa gereza
ambaye alimhakikishia kupata huduma nzuri.
Prof. Lipumba aliongeza kuwa, anazo
taarifa kuwa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linataka kumhoji daktari
aliyemtibu Shekhe Ponda, siku alipopigwa risasi.
"Inasikitisha kwamba polisi
hawajapitia Taasisi ya Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), ili iombe kibali cha
kufanya hivyo badala yake wanataka kumsulubu daktari kwa kosa la kumtibu Shekhe
Ponda jambo ambalo linashangaza," alisema.
Aliongeza kuwa, CUF inataka Serikali
iunde tume huru ambayo itaongozwa na Jaji ili kuchunguza tukio la kupigwa
risasi Shekhe Ponda, askari aliyempiga na waliompa amri ya kufanya hivyo
wafikishwe mahakamani na kumfutia kesi ya uchochezi.
Shekhe Ponda alipata mkasa huu Agosti 10 mwaka huu mkoani Morogoro muda
mchache baada ya kushiriki katika Kongamano la Baraza la Eid.
k ama maazimio hayo yatapuuzwa na wahusika pamoja na Serikali kushindwa kuchukua hatua stahiki, itakuwa mwanzo na mwisho wa historia ya Tanzania.
ReplyDeletewewe anon naona kichwa chako hakifanyi kazi. unasema mwanzo na mwisho wa Tanzania? unadanganywa na masheikh wako wasio na elimu! Kwa taarifa yako Tanzania itakuwepo milele, nchi haitishwi na watu wenye mawazo finyu kama huyo Ponda wako, lipumba na wenzako wenye shida ya kufikiri. msijidanganye mtashughulikiwa na mtaikimbia hii nchi, sijui mtaenda wapi? labda Somalia kwa sababu hakuna anayewataka ninyi watu wa fujo mnaofikiria dini kwenye kila kitu ndiyo maana mmebaki nyuma kwa kila kitu isipokuwa kuchonga midomo!
ReplyDeletekama si waislaa nani angepigania uhuru wa nchi hii?inaonekana unajazba tu huna unachokijua katka nchi hii ila udini bila kujali maslahi ya watanzania wote.moto ukiwaka wewe utabaki?askari hawana kazi wakat huo.wewe uliza huko Somalia askar walikuwepo?walienda wapi?inaonekana hujui kitu ktka historia ya dunia lakni iko siku utajua.
ReplyDeletekumbe hujui hata Lipupa ni muislam na Prf,na nafasi yake dunian.
Na wewe sijui unaongea nini? Ina maana umewaona waislaam wenyewe wakipigania uhuru? Hao wengine waliopigania uhuru wasio kuwa waislaam? NDIYO MAANA NASEMA HAO MASHEIKH WENU WASIO NA ELIMU WANAWADANGANYA. Hata kama askari hawatakuwepo haina maana wengine watawaogopa ninyi waislaam wapenda fujo. Mnatutisha tisha hapa mnafikiri ninyi pekee yenu ndiyo mnaweza kupigana? Huyo Li-pumba anafanya kampeni za misikitini na kujaribu kuleta udini lakini kila uchaguzi anakuwa wa pili kutoka mwisho.....Kura zenu hazitoshi!
ReplyDeletehuyo anaemtetea Lipumba eti muislam mwenzao ngoja itokee vita hapa utaona atakvyowatosa na kukimbilia zake huko Marekani alafu ndo atajua kama wakati wa vita dini au Lipumba watakuwepo kwa ajili yako.
ReplyDeletenyie waislamu mnapenda sana udini ndo maana hata Nyerere aliwasoma toka zamani akaona aweke pembeni mambo ya udini.Na kwanza siku zote huwezi changanya dini na mambo ya utawala.
Huyu Shekhe atajuta kuifahamu Serikali.
ReplyDelete