Na Aziz Msuya, Morogoro
VIONGOZI 105 kutoka vyuo vikuu 30 nchini, wamesema
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Bw. January Makamba, ndiye
mwenye sifa za kuwa rais kama atagombea nafasi
hiyo katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Wamesema Bw. Makamba ana
sifa zote za kuwa kiongozi wa nchi ili aweze kulikomboa Taifa ambalo hivi sasa
linakabiliwa na matukio mbalimbali ya uvunjifu wa amani.
Matukio hayo ni pamoja na
vurugu, watu wasio na hatia kutekwa na kufanyiwa vitendo vya ukatili, kumwagiwa
tindikali na kupungua kwa mtangamano wa kijamii.
Viongozi hao waliyasema
hayo mwishoni mwa wiki katika mkutano wao ambao ulihusisha viongozi mbalimbali
wa Serikali za wanafunzi katika vyuo vikuu.
Washiriki wa mkutano huo
ambao haujaandaliwa na Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini
(TAHLISO), ni Marais wa Vyuo Vikuu, Makamu wa Rais, Maspika, Mawaziri Wakuu na
viongozi mbalimbali.
Katika mkutano huo ambao
ulifanyika mkoani Morogoro, viongozi hao walipendekeza jina la Bw. Makamba awe
mgombea wa kiti cha urais kwa tiketi ya CCM 2015.
Mwenyekiti wa mkutano huo
ambaye ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Kampasi ya
Mbeya,
Bw. Theonest Theophil,
alisema wajumbe walichagua majina matatu ya wagombea wa nafasi hiyo.
Majina hayo ni Bw. Makamba
(CCM), Bw. Zitto Kamwe na Bw. John Mnyika wote kutoka Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA).
" M a j i n a h a y a
n d i y o yaliyochomoza katika nafasi tatu za juu lakini jina la Bw. Makamba
likapata kura 72, akifuatiwa na Bw. Kabwe aliyepata kura 20.
"Matokeo ya kura hizi,
atapelekewa Bw. Makamba ambayekama akikubali kugombea, tutazunguka nchi nzima
kumfanyia kampeni kwa sababu nchi hii kwa sasa inahitaji fikra mpya za kiongozi
kijana...uchaguzi wetu haujaangalia itikadi za kisiasa wala dini," alisema
Bw. Theophil.
Alizitaja sifa za kiongozi
wanayemtaka kuwa kwanza awe kijana mwenye fikra mpya, atakayeleta matumaini
mapya, kuwaunganisha Watanzania, asiyeendekeza siasa za kikanda, mdini na
mkabila.
Sifa nyingine ni kiongozi
mwadilifu, asiye na rekodi ya kutuhumiwa mahali popote kwa vitendo viouvu,
mtulivu, mwenye busara na anayepima kauli zake.
"Mkutano umeafiki
kuwa, sifa zote Bw. Makamba anazo na ameonesha ujasiri katika nafasi za uongozi
alizowahi kushika kwani ni mwadilifu, anakubalika na makundi yote ya vijana,
wasomo na viongozi wenzake ndani, nje ya chama chake.
"Vijana sasa wameamka
wanataka kiongozi kijana ambaye ataikomboa nchi yetu bila kujali itikadi yake
kisiasa wala kidini," alisema Bw. William Kanyondo kutoka Chuo Kikuu cha
Tumaini, mkoani Arusha.
Bw. Theophil alisema kama Bw. Makamba atakubali
kugombea kiti hicho na CCM ikakataa kumpitisha, watamshauri agombee kama mgombea binafsi.
Mkutano huo pia ulijadili masuala mengine ambayo ni
tofauti ya kipato cha Watanzania na kudai hali hiyo ni ishara mbaya kwa
amaninaum ojawaWatanzania.
Wal isem aukua ji w a uchumi bado haujaen da sambamba
naahueniyamaishayaMtanzaniawa kawaid a, ubora w aelimu hasa vijijini na fursaz
aaj ira.
Mkutan ohuoulian da liwanaTaasisi yaK upam
bananaMaa dui watatuambaoni u jinga, m aradh i naumaski ni (FPI
D)iliyopojijiniDar es Salaam
Hivi kweli hawa wanajua nchi na ulimwengu unakoelekea? nina wasiwasi na viongozi hawa?
ReplyDelete