Na
Moses Mabula, Tabora
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora imewafutia
shtaka la ugaidi lililokuwa likiwakabili makada watano wa Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (CHADEMA), hivyo kubaki wakikabiliwa na shtaka moja la kutuhumiwa
kummwagia tindikali kada wa CCM, Mussa Tesha.
Akitoa uamuzi huo mjini hapa jana, Jaji Mfawidhi wa
Mahakama hiyo, Simon Lukelerwa, alisema amefikia uamuzi huo kutokana na shtaka
hilo kutokidhi sababu za kisheria zilizotolewa na upande wa mashtaka.
Jaji huyo alisema kulingana na kifungu (C) cha Sheria
ya Mwenendo wa Mashtaka ya mwaka 1985, anaamuru shauri linalowakabili
washtakiwa kwa sasa lihamishiwe katika Mahakama ya Wilaya ya Igunga.
Alisema sheria namba 245 kifungu kidogo (1) kinasema
washtakiwa wanatakiwa katika mahakama ya sehemu ambayo wanadaiwa kutenda kosa
husika.
Jaji Lukelerwa ameamuru washtakiwa wote wapelekwe
wilayani Igunga kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa upya shauri lao na kwamba dhamana
ya washtakiwa hao ipo wazi iwapo watakidhi matakwa ya dhamana.
Awali ya ulinzi mahakamani hapo iliimarishwa na Polisi
waliokuwa na silaha wakati kesi hiyo ikiendelea kutolewa uamuzi. Kesi hiyo ya
ugaidi ilifunguliwa mahakamani hapo Juni 24, mwaka huu, baada ya washtakiwa hao
kuachiwa awali wilayani Igunga, katika kesi ya madai ya kummwagia tindikali
kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tesha.
Watuhumiwa hao ni Evodius Justunian, (30) mkazi wa
Bukoba, Osca Kaijage, mkazi wa Mkoa wa Shinyanga, Seif Magesa, mkazi Nyasaka
Mwanza, Rajabu Daniel, mkazi wa Dodoma na Henry Kilewo.
Mapema Julai 8, mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu
Mkazi wa Mkoa wa Tabora, Hakimu wa Mahakama hiyo, Issa Ibrahim Magori, alisema
alikataa kusikiliza kesi hiyo kutokana na kutokuwa na mamlaka hiyo, ambapo
iliahirishwa.
Wakili wa upande wa utetezi katika kesi hiyo, Peter
Kibatala, aliwaambia waandishi wa habari mjini hapa kwamba, Mahakama Kuu
imetenda haki na ana imani kubwa na mahakama hiyo.
Alisema kwa
kuwa washtakiwa h a o wa l i k ama twa k a t i k a sehemu tofauti hivyo kesi
zao zilipaswa kusikilizwa maeneo waliyokamatiwa.
No comments:
Post a Comment