26 August 2013

MAHAKAMA YA KADHI BALAA



 Na David John
BARAZA Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, limesema kipengele cha uwepo wa Mahakama ya Kadhi kwenye Katiba Mpya, hakiepukiki hivyo ni wajibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, kuhakikisha Waislamu wanapata haki yao ya msingi.

Mwenyekiti wa baraza hilo, Shekhe Mussa Yusufu Kundecha, aliyasema hayo Dar es Salaam jana katika mkutano waliouitisha ili kupitia Rasimu ya Katiba Mpya ulioshirikisha wajumbe kutoka mikoa mbalimbali nchini.
Alisema Mahakama ya Kadhi ni jambo muhimu kwa Waislamu hasa katika eneo la mirathi na mambo mengine ambapo awali waliwasilisha ombi hilo kwa Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji mstaafu Joseph Warioba kabla rasimu hiyo haijatoka.
"Tu l i p e n d e k e z a k uwe p o kipengele cha kuitambua mahakama hii kwenye Katiba Mpya lakini kinyume na hapo, tume imekataa mapendekezo yetu...tunatarajia kuyapeleka tena kwa tume husika ili katiba iweze kuleta matumaini ya Watanzania wote," alisema.
Naye mjumbe wa baraza hilo kutoka Temeke, Dar es Salaam, Shekhe Abubakar Shabani alisema, watahakikisha suala hilo linapigiwa kelele ili liweze kuingizwa katika Katiba Mpya.
Alisema hata ombi lao la kutaka siku ya Ijumaa iwe mapumziko pia limekataliwa na tume hiyo kama ilivyo Jumapili kwa Wakristo hivyo ni wazi kuwa Waislamu hawatendewi haki.
"Ijumaa ni siku ya ibada kwa Waislamu hivyo inastahili iwe ya mapumziko kama ilivyo Jumamosi na Jumapili, kama haiwezekani Serikali ichague siku nyingine ya mapumziko ambayo itakuwa inatendeka haki kwa pande zote," alisema Shekhe Shabani.
Aliongeza kuwa, pendekezo lingine ambalo walilipeleka kwa tume hiyo ni kuruhusiwa kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu Duniani (OIC), lakini imekataa mbali ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Benard Membe kusema suala hilo halina tatizo lolote kwa Waislamu.

9 comments:

  1. BASI TUME IJIAMULIE YENYEWE WATU WASITOE MAPENDEKEZO YAO. AU WANAFANYA HIVYO KWA WAISLAM TU?

    ReplyDelete
  2. BORA TUME IKATAE MANAKE MWISHO WA SIKU MKIKUBALIWA MNAKUAGA TATIZO KWELI..HAPA MAHAKAMA YA KADHI HAIJAKUBALIWA MPO BIZE KUCHOMA MAKANISA JE IKIKUBALIKA ITAKUAJE?ALAFU MNADAI MNAONEWA SIWAELEWI HATA KIDOGO CJUI MNATAKA NINI.

    ReplyDelete
    Replies
    1. NITAJIE MUISLAM AMBAYE KACHOMA KANISA.

      Delete
    2. SIWEZI KUTAJA KWA SABABU HAPA SI ENEO LA KUSHTAKI MTU.NA KAMA SI MUISLAMU NANI KACHOMA AU UNATAKA KUSEMA WAKRISTO WENYEWE NDO WAMECHOMA MAKANISA?BASI MPAGANI NDO KACHOMA LOL!

      Delete
  3. HIVI JAMANI WENZUTU KAMA MNATAKA MAHAKAMA YA KADHI KWA NINI MSIIPITISHE HUKO KWENYE JUMUIYA ZENU BADALA YA KUNG'ANG'ANA LIWE JAMBO LA KITAIFA?HAMUONI KAMA MNALETA UDINI KATIKA TAIFA LETU?ACHENI UDIKTETA.

    ReplyDelete
  4. Mbona BAKWATA hamuitaki kwa kusema kuwa imeanzishwa na serikali? Inakuwaje tena mnaitaka serikali hiyo hiyo ianzishe Mahakama ya Kadhi? Double standards!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mungu wetu asimame katika hili, hawa wenzetu wanaleta shida sana sijui ni mbingu gani wataingia hawa jamaa, mi cwaelewi kabisa, E MUNGU TUNUSURU KATIKA HILI,

      Delete
    2. HATA KIDOGO WEWE SI MUELEWA.TOFAUTISHA KUANZISHWA NA KUWEKWA KWENYE KATIBA.HAYA NI MAONI LAZIMA YAFANYIWE KAZI

      Delete
  5. na nyie bwana mmezidi sasa mnataka watu wasifanye kazi ijumaa...kwa hyo siku za kazi ziwe nne tu.maendeleo yatatoka wapi?

    ReplyDelete