20 August 2013

MADAKTARI KUTOKA CHINA WASHAURIWA KUGEUKIA KINGA



Na Mwandishi Maalumu, Zanzibar
SERIKALI imetoa wito kwa wataalamu wa afya kutoka China waliopo nchini kuangalia pia suala la kinga ya maradhi mbalimbali badala ya kutilia mkazo zaidi suala la tiba wakati wanapokuwa nchini. Wito huo umetolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein wakati alipokuwa akizungumza na timu ya watu 25 ya wataalamu wa afya kutoka Jamhuri ya Watu wa China waliomtembelea Ikulu jana.

Timu hiyo ya wataalamu 21 wakiwemo madaktari bingwa iliwasili nchini mwezi Juni mwaka huu ambayo inatarajiwa kukaa nchini kwa miaka miwili inatoka Jimbo la Jiangsu China ambako wataalamu wa afya kutoka jimbo hilo wamekuwa wakija Zanzibar kufanya kazi tangu mwaka 1964.
"Msijishughulishe tu katika kutoa huduma za tiba badala yake muangalie pia suala la kinga ambalo ni muhimu katika kuimarisha afya za wananchi," aliwaambia wataalamu hao huku akiwataka kuvitumia vyombo vya habari vikiwemo vya Serikali kuelimisha jamii juu ya kinga ya maradhi mbalimbali.
Dkt.Shein amesema timu hiyo ina umuhimu wa kipekee kwa kuwa pamoja na kutoa huduma kwa wagonjwa, lakini pia imekuja kutekeleza mpango maalum wa kusimamia ujenzi wa kituo cha uchunguzi wa maradhi ya njia ya chakula katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Unguja na kituo cha kuhudumia wagonjwa waliopata ajali katika Hospitali ya Abdalla Mzee Pemba.
"Vituo hivyo ni vipaumbele kwetu kwa kuwa vitapunguza gharama kwa serikali ya kuwapeleka wagonjwa nje ya Zanzibar kwa matibabu na wakati mwingine hata kwa uchunguzi," alisema Dkt.Shein.
Alibainisha kuwa hivi sasa wagonjwa wengi wenye matatizo ya njia ya chakula hulazimika kupelekwa Dar es Salaam au hata nchi za nje; hivyo kukamilika kwa kituo hicho kutakuwa faraja kwa Serikali na wananchi.
Kwa upande wa kituo cha watu wanaopata ajali huko Pemba alisema ni muhimu kwa kuwa kumekuwepo na ajali nyingi kisiwani humo hususan katika msimu wa uchumaji karafuu hivyo kujengwa kwa kituo hicho kumekuja wakati mwafaka.
Wakati huo huo timu ya wataalamu wa afya kutoka China imesema imejizatiti kuwahudumia wananchi ili kuhakikisha inatoa mchango wake ipasavyo katika kuimarisha afya nchini.
Kauli hiyo imetolewa na kiongozi wa timu hiyo Dk. Lui Ya Ping wakati alipokuwa akitoa salamu za wataalamu hao kwa Rais.
"Tumejizatiti kufanya kazi kwa bidii kuwahudumia wananchi kwa kuwa tunaamini kufanya hivyo tutakuwa tumetimiza wajibu wetu uliotuleta humu nchini," alieleza Dkt. Lu

No comments:

Post a Comment