02 August 2013

CWT YATOA TAMKO KUFELI KWA WALIMU



 Gladness Theonest na Theophan Ng'itu
RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, amesema matokeo mabaya ya walimu yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) hayawashangazi kwani walishaiambia Serikali iwe inapeleka vyuoni wanafunzi wenye ufaulu mzuri, lakini haifanyi hivyo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mukoba alipozungumza na Majira. Alisisitiza kuwa pamoja na kupigia kelele suala hilo, lakini Serikali imekuwa ikiendelea kupeleka wanafunzi wabovu, hivyo imevuna ilichopanda.
Al i s ema ma t o k e o h a y o pia yamechangiwa na Serikali kutosikiliza madai yao kwani tangu mwaka jana walimu na Serikali wamekuwa na ugomvi usiokuwa na majibu.
Aliongeza kuwa madai ambayo walikuwa wakiyadai ni pamoja na nyongeza ya asilimia 100 ya posho ya kufundishia, asilimia 50 ya mazingira magumu, lakini hadi sasa wamepewa nyongeza ya asilimia 8 tu ya nyongeza ya mshahara.
Mukoba alisema walimu wa vyuo ambao ndiyo wana kazi kubwa ya kufundisha walimu ndiyo waathirika wakubwa kutokana na kutopandishwa vyeo, kutokurekebishiwa mishahara, kutopata fedha za mizigo, likizo na matibabu, ukichanganya hali hiyo inasababisha ufaulu mdogo.
"Ukipanda ujinga unalima uzuzu, sio mara ya kwanza hali hii inatokea, Serikali imeendelea kuziba masikio kwa suala nyeti kama hili la elimu, huku ukitarajia taifa kwenda mbali," alisema Mukoba.
Alisema madhara ya hali hii ya matokeo mabaya ya ualimu jamii haitakuwa na imani na walimu na hata yule ambaye alikuwa anatamani kuingia katika fani ya ualimu hawezi kutamani tena.
Mukoba aliongeza kuwa damu ya taifa ni elimu na pindi inaposimama taifa litakufa, hivyo lawama zote ipewe Serikali kwani imekuwa ikipewa ushauri wa kutosha lakini imekataa kuupokea.
"Nina imani hata katika matokeo haya hawatachukua hatua sahihi, zaidi wataunda tume ambayo itatoa matokeo wanayoyajua tayari na sisi kama CWT hatuwezi kuridhika na kukubali Taifa lididimie mikononi mwetu, lazima tuchukue hatua hata kama hatua hizi hazitakuwa na chembe ya utamu," alisema Mukoba.
Majira ilizungumza na baadhi ya walimu ambao hawakutaka kutaja majina yao gazetini walisema kuwa katika matokeo hayo hakuna kipya, kwani hicho kilichotokea ndicho walichokuwa wanakitarajia

1 comment:

  1. NINARUDIA KUSEMA KWAMBA shetani amevamia elimu ya kitanzania na kufaulu ENYI KINA NDALICHAKO,KAWAMBWA,NA WENGINE SIMAMIENI NA KUHAKIKISH PALE MNAPOSHINDWA SHIRIKIANA NA WENGINE NA KAMA KUNA MIGOGORO SAIDIENI IONDOKE MAANA HAO WALIMU NI WAMINIFU WAMEKUBALIANA KUNIA MAMOJA NA VIONGOZI ILA EPUKENI MIZENGWE KAMA MNAWAPA AHADI ZITIMIZENI ILI TUFIKIE LENGO NDG ZANGU TUFIKE WAKATI TUAMUWE KUJIKOMBOA KIELIMU ILA BADO ELIMU INAYOTOLEWA IKIDHI VIWANGO

    ReplyDelete