Na Rachel Balama
KE S I i n a y o m k a
b i l i aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda jana
imeshindwa kuendelea kutokana na wakili wa upande wa Jamhuri anayeshughulikia
kesi hiyo kutofika mahakamani hapo. Jana ilikuwa tarehe ya mwisho kwa upande wa Jamhuri kuieleza
mahakama kama wanaendelea na ushahidi au wanafunga baada ya mahakama kutoa
agizo hilo
Julai 15, mwaka huu.
Wakili wa Serikali, Beatha Kitau, aliiomba mahakama iahirishe kesi
hiyo kwa kuwa wakili wa Serikali Tumaini Kweka anayesimamia kesi hiyo kutofika
mahakamani hapo.
Baada ya ombi hilo Hakimu Mkazi
Waliarwande Lema aliahirisha shauri hilo
hadi Agosti 14, mwaka huu.
Mbali ya Kibanda ambaye kwa sasa ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya
New Habari 2006, washtakiwa wengine ni aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa gazeti la
Mwananchi, Theophil Makunga na mwandishi wa makala, Simon Mwigamba.
Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka ya kuruhusu na kuchapisha
makala ya uchochezi katika gazeti la Tanzania Daima iliyokuwa na kichwa cha habari
"Waraka maalum kwa askari wote".
No comments:
Post a Comment