30 July 2013

POLISI DAR WANASA NYARA ZA SERIKALI



 Frank Monyo na Theophan Ng'itu

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watuhumiwa 38 kwa makosa mbalimbali yakiwemo kukutwa na nyara za Serikali, wizi wa magari pamoja na funguo bandia. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema Julai 22, mwaka huu maeneo ya Msimbazi Center polisi wakiwa doria walimtia mbaroni mkazi wa Mwananyamala, Ibrahimu Mnyanga akiwa na meno ya tembo vipande 16 vyenye kilo 24.5.


Pia alisema, walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine watatu wakiwa na vifaa vya milipuko kwenye nyumba ya Rose Amel, mkazi wa Salasala wilayani Kinondoni. Kova alisema kuwa, watuhumiwa wengine sita walikamatwa na magari matatu yenye namba za usajili T 723 BXF aina ya Verossa likiwemo T 220 BPE aina ya Toyota Pasoo na T 823 CCS aina ya Suzuki maeneo ya Keko Magurumbasi Wilaya ya Temeke na Kikosi cha Kudhibiti Wizi wa Magari.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Omari Kaisi, mkazi wa Keko, Mohamed Seif, mkazi wa Yombo Kilakala, Abubakari Rashidi, mkazi wa Kiwalani Minazi Mirefu, Shabani Ngonde, mkazi wa Kinondoni Mkwajuni na Shabani Rajabu mkazi wa Tabata.

Kamanda Kova alisema kuwa, polisi wamejipanga kuimarisha ulinzi katika msimu huu wa sikukuu ya Idi inayotarajiwa kufanyika Agosti 8, mwaka huu. Alisema, Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu kuhakikisha ulinzi unakuwepo maeneo yote ya fukwe za bahari, kumbi za starehe na kuhakikisha linadhibiti vitendo vyote vya uhalifu

No comments:

Post a Comment