Na Rehema
Maigala
CHAMA cha Wanahabari
Wa n a w a k e Ta n z a n i a (TAMWA) leo
kitazindua ripoti ya utafiti wa unyanyasaji wa kijinsia uliofanyika Aprili
mwaka huu katika wilaya 10 za Tanzania Bara na Zanzibar.Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari jana Dar es Salaam imesema kuwa ripoti hiyo ni
utafiti unaoonesha hali halisi ya unyanyasaji wa kijinsia katika jamii pamoja
na mambo yanayokwamisha juhudi za vyombo vinavyotetea haki za wanawake na
watoto hapa nchini
Taarifa
hiyo imesema kuwa utafiti huo ulifanywa kwa kushirikiana na waandishi wa habari
kutoka vyombo mbalimbali vya Nipashe, The Guardian, The Citizen, Mwananchi,
Daily News, Zanzibar Leo na Majira.Ilisema kuwa waandishi wa habari waliweza kuwahoji wanajamii mbalimbali
kuanzia ngazi za familia na kupata ukweli wa hali halisi ya unyanyasaji wa
kijinsia ikiwemo, ukeketaji, ubakaji, wanawake na watoto kutelekezwa, mimba
katika umri mdogo na watoto wa kike
kulazimishwa kuolewa.
I l i e l e z a k u w a w i l a y a
ziliyofanyiwa utafiti ni pamoja na Wete (Pemba Kaskazini), Unguja Mjini
Magharibi (Unguja Magharibi), Unguja Kusini, Kisarawe (Pwani), Newala (Mtwara),
Mvomero (Morogoro), Lindi vijijini na Ruangwa (Mtwara), Kinondoni na Ilala Dar
es Salaam.Uzinduzi wa ripoti hiyo ya utafiti ni mwendelezo wa utekelezaji wa mradi
wa kujenga na kuimarisha usawa wa kijinsia na kutokomeza ukatili dhidi ya
wanawake na watoto (GEWE II) unaoshirikisha mashirika yanayotetea haki za jamii
hasa wanawake na watoto yakiwemo TAMWA, Jumuiya ya Wanawake Wanasheria Zanzibar
ZAFELA, Chama cha Wanasheria Wanawake ñ TAWLA, Mtandao wa Jinsia Tanzania
(TGNP), na Kituo cha Usuluhishi cha TAMWA (CRC).
No comments:
Post a Comment