Na Anneth Kagenda, Bagamoyo
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Stadi imegeuka mbogo baada ya kuhoji ni kwanini kuna shule zisizosajiliwa
mitaani na zinaendelea kufumbiwa macho na kutoa elimu kwa wanafunzi jambo
alilosema ni hatari kwa taifa.Pia imewaagiza Waratibu Elimu Kata
kuhakikisha wa n a s amb a a kwe n y e shule zote za sekondari na kuangalia
kama wanafunzi walioingia kidato cha tatu ni wale waliofaulu ama la kwa madai
kuwa kuna shule nyingine wanafunzi walifeli lakini wanaendelea na masomo ya
kidato hicho kama kawaida jambo ambalo ni hatari kielimu.
Hayo aliyasema wilayani Bagamoyo na
Naibu Waziri wa Elimu, Philipo Mulugo mara baada ya kufungua Mafunzo ya
Waratibu Elimu Kata Taifa yanayoendeshwa na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa
Elimu (ADEM). Alisema ni jambo la kushangaza kuona
kuna shule zimetapakaa mitaani wakati waratibu hao wapo na kusema kuwa ni
kwanini wasitoe taarifa ili zishughulikiwe na ikiwa taarifa hazifiki mahali
husika ni bora wakapiga simu yake ya mkononi moja kwa moja kuliko kuzifumbia
macho jambo linalosababisha kuongezeka kwa watoto wengi wanaofeli.
"Kwa mfano hili la shule zisizo
rasmi ninaomba sasa waratibu mnaopata mafunzo haya mara baada ya kutoka hapa
hakikisheni mnatoa taarifa juu ya uwepo wa shule hizo na mkiona taarifa
hazifanyiwi kazi piga simu yangu ambayo nimewapa leo na mkishindwa basi tumeni
ujumbe mfupi wa maneno (sms) nitaukuta na nitajibu," alisema Mulugo.
Ku h u s u wa n a f u n z i kupandishwa
madaraja bila kufaulu alisema: "Niliwahi kwenda katika shule moja
sitaitaja lakini cha kushangaza nilikuta watoto ambao walifeli kidato cha pili
wapo kidato cha tatu nikauliza na hawa vipi..., sikupata majibu hivyo basi
baada ya hapa naomba mkafuatilie na mnipe majibu ili suala hili lifanyiwe
kazi."
A l i s e m a h a k u n a anayependa
kuadhibiwa juu ya matokeo mabaya ya wanafunzi, kulaumiwa na kuambiwa waziri
ajiuzulu hivyo wizara yake itahakikisha kero zote zinazojitokeza inazifanyia
kazi ikiwa ni pamoja na kuwatengenezea mazingira mazuri waratibu hao ili waweze
kuisaidia wizara yake.
Wa z i r i Mu l u g o p i a aliwataka
waratibu hao kuwa wavumilivu wakati Serikali ikishughulikia changamoto
walizonazo ikiwamo zile za kutokuwa na ofisi huku akiwataka kuhakikisha
wanaonesha mshikamano mara baada ya kufika katika shule hizo na kukuta madudu
kwa kutoa taarifa kwake.
Naye Mtendaji Mkuu wa ADEM Dkt. Sisten
Ma s s a n j a , a l iwa t a k a washiriki wa mafunzo hayo mara baada ya
kumaliza ni vyema wakayafanyia kazi ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi
wao.
"Ni matumaini yetu kuwa mafunzo
haya mtayafanyia kazi ili yaweze kuleta matunda na mambo yaliyokuwapo awali
yakiwamo ya wanafunzi kufeli yasiendelee lakini tunaandaa kozi mbalimbali
ambazo mtazipata ili kujiongezea ufanisi katika kazi," alisema.
Mwenyekiti wa Mafunzo hayo, Richard
Chambo alisema zipo changamoto mbalimbali zinazowakabili waratibu hao ikiwamo
kuongezeka kwa majukumu hivyo ni vyema Serikali ikawatupia jicho la pili.
"Pia tunazo changamoto nyingine ambazo ni kutokuwa na ofisi,
vitendea kazi, shule nyingi za kata kutokuwa na usafiri na mambo mengine
mengi," alisema.
No comments:
Post a Comment