25 July 2013

ASAKWA KWA TUHUMA ZA MAUAJI



Na Elizabeth Joseph, Dodoma
MTU mmoja anayefahamika kwa jina la Nyerere Bakari mkazi wa Makirinya, Wilaya ya Kondoa anatafutwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua mwenzake kwa kumpiga risasi.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kuongeza kuwa Bakari alifanya mauaji hayo mnamo Julai 23, mwaka huu, saa nane usiku.

"Marehemu huyo alitambulika kwa jina la Abdallah Mgunda (25) ambaye ni mkazi wa Kwadelo wilayani Kondoa ambapo mtuhumiwa alitumia silaha inayodhaniwa kuwa ni gobore kwa kumpiga risasi zilizompata sehemu ya kifuani na kwenye mapaja na kusababisha kifo chake."
"Chanzo cha mauaji hayo kinadhaniwa kuwa ni ugomvi uliozushwa na mtuhumiwa huyo kuwa marehemu alikuwa amelisha mifugo katika shamba lake," alisema Misime.Aidha alisema kuwa mnamo tarehe hiyo majira ya saa 12 katika eneo la Nkuhungu Manispaa ya Dodoma mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Imani Francis (28) ambaye pia ni mkazi wa eneo hilo alikutwa ameuawa katika eneo la Itega kwa kupigwa na watu wasiojulikana.
M i s i m e a l i e l e z a k u w a uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu huyo alishakuwa na tuhuma za kubaka na wizi wa unyang'anyi ingawa matukio hayo hayakuwahi kuripotiwa polisi.
Hata hivyo alitoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani ni kosa la jinai kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment