Na Jamaal Mlewa
KAMPUNI ya HEIRS
Holdings imeahidi mchango wa dola bilioni 2.5 kati ya dola bilioni saba ambazo
serikali ya Marekani imeahidi katika kufadhili utekelezaji wa mradi wa umeme
unaojulikana kama 'Power Afrika.'
Hayo
yalibainishwa juzi na Mwenyekiti wa HIERS Holdings, Tony Elumelu wakati akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Elumelo ni
mfanyabiashara raia wa Nigeria ambaye amepata mafanikio makubwa katika sekta ya
mafuta.
Alisema, mradi
huo unalenga mambo mawili m a k u b w a i k i w a n i kuhakikisha idadi ya watu
wanaopata umeme inaongezeka maradufu lakini pia kuziwezesha nchi za Afrika
kujenga uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha.
Pamoja na dola
bilioni saba alizoahidi Rais Barack Obama, taasisi mbalimbali binafsi nazo
zimetoa dola bilioni tisa ili kufanikisha mradi huo utakaonufaisha nchi za
Tanzania, Kenya, Liberia, Nigeria, Ethiopia na Ghana.
Awali akizindua
mradi mk u b w a w a umeme unaotekelezwa na Kampuni ya Symbion Power, Rais
Barack Obama ameitaka serikali ya Tanzania kuhakikisha kuwa miradi iliyopangwa
kutekelezwa chini ya ufadhili wa Marekani haicheleweshwi bila sababu za msingi.
"Kwa k u a
n z i a , i l i k u t e k e l e z a d h ami r a yetu, tutahakikisha kuwa
tunawapatia umeme watu milioni 20 katika nchi sita ambako mradi
utatekelezwa," alisema Rais Obama.
Hata hivyo,
takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu milioni 600 kati ya wakazi bilioni moja
barani Afrika hawana umeme.
Mradi huo umekuja wakati ambapo serikali
ina mkakati wa kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka kiwango cha sasa megawati
1,438.24 hadi kufikia megawati 2,780 mwaka 2015.
Kampuni ya Symbion Power ambayo inaelekea
kuwa mkombozi wa kero ya nishati ya umeme nchini ilinunua mitambo ya Dowans
mwaka 2011.
Dowans mpaka sasa ina mgogoro na Shirika
la Umeme nchini (TANESCO) ikidai kiasi cha dola milioni 65 ambazo iliamriwa
kulipwa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi ya Biashara.
Dowans ilirithi mitambo hiyo kutoka kwa Kampuni ya
RICHMOND ambayo ilituhumiwa na Bunge kuwa na uwezo mdogo wa uzalishaji umeme
mwak 2007.
No comments:
Post a Comment