16 May 2013

Walimu wafananisha elimu nchini na maghorofa mabovu


N a Yu s u p h Mu s s a ,
Lushoto


 BAADHI ya walimu wilayani Lushoto wamefananisha elimu nchini na maghorofa mabovu yanayojengwa jijini Dar es Salaam, kwani inazidi kushuka kutokana na mfumo mbovu wa mitaala na uingizaji holela wa vitabu vya kufundishia na kujifunzia shuleni. Wakizungumza juzi kwenye mkutano wa wakuu wa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya Bumbuli, uliondaliwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Bumbuli,Bw. January Makamba, walisema Serikali ishirikishe wadau kwenye
utungaji wa mitaala. "Kama mchakato wa Katiba Mpya unavyoshirikisha wadau, vivyo hivyo utungaji au uanzishwaji wa mitaala m i p y a i w a s h i r i k i s h e wadau ili kupata mitaala itakayokubalika vinginevyo elimu itaendelea kushuka. "Itazidi kuporomoka kwa vile haina misingi mizuri. Hivi inakuwaje mtoto wa darasa la kwanza anakwenda shuleni na madaftari tisa, turudishe utaratibu wa 'K' tatu yaani masomo ya Kusoma, Kuandika na Kuhesabu" alisema Mratibu wa Elimu Kata ya Soni, Bi. Luth Msagati. Mratibu wa Elimu Kata ya Milingano alisema mitaala iliyopo kwa sasa hata walimu hawaijui, hivyo ni vigumu mwalimu kumfundisha mwanafunzi akaelewa, huku akisema changamoto nyingine ni kuwaingiza sekondari wanafunzi waliopata alama 70.Mkuu wa Shule ya Sekondari Kwa Mongo,Bw. Anthony Kihiyo, alisema kwa Serikali kuruhusu  wanafunzi wa shule za kata na zile za Mtakatifu kufanya mtihani mmoja ni sawa na kumpambanisha Francis Cheka na mgonjwa aliyelazwa Hospitali ya Muhimbili. "Wanafunzi wa shule za kata kufanya mtihani mmoja na wale wa shule binafsi ni kuwaonea. Hata mabondia uzito wao unapimwa na unatakiwa ulingane ndipo wapigane," alisema,Bw. Kihiyo. Kwa upande wake Bw. Makamba alisema pamoja na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuunda tume ya kuchunguza kiini cha matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka jana, bado walengwa ambao ni walimu hawajapewa nafasi ya kutoa maoni yao juu ya suala hilo .


No comments:

Post a Comment