24 August 2012

Kagasheki aongeza uwazi Malisili



Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, amebadili taratibu za kuwapata wajumbe wa bodi mbalimbali zilozopo chini ya Wizara hiyo.

Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana kwa vyombo vya habari na Msemaji wa Wizara hiyo, Bw. George Matiko, ilisema kuanzia sasa wajumbe wa bodi hizo watapatikana kwa njia ya ushindani badala ya kuteuliwa moja kwa moja na Waziri.

Alisema hivi sasa kuna bodi nane zilizopo chini ya Wizara hiyo ambazo zimemaliza muda wake au kukaribia kuisha.

Aliongeza kuwa, bodi hizo ni za Taasii za Mashirika ambazo ni Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI), Taasisi ya Utafiti wa Misitu nchini  (TAFORI), Makumbusho ya Taifa, Chuo cha Mafunzo na Usimamizi wa Wanyamapori (MWEKA).

Bodi nyingine ni Chuo cha Mafunzo ya Wanyamapori Pasiansi,  Wakala wa Mbegu za Miti (TTSA) na Leseni za Utalii (TTLB).

Bw. Matiko aliwataka Watanzania wenye sifa za kuwa wajumbe wa bodi hizo, kupeleka maombi yao kwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii. Baadhi ya watu ambao wamezungumzia hatua hiyo, walisema ni nzuri na imezingatia uwazi kupata wajumbe hao.

No comments:

Post a Comment