Na Fatuma Rashid
Timu ya vijana chini ya miaka 20 ya Yanga
B, imefanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali katika michuano ya Uhai Cup baada
ya kuwafunga wenzao wa Ashanti
mabao 2-1.
Katika mchezo huo
uliochezwa Uwanja wa Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, timu zote
zilianza mchezo kwa kushambuliana huku kila timu ikionesha nia ya kutafuta bao
la ushindi ili kuweza kuingia hatua ya nusu fainali.
Timu ya Yanga dakika 15 za
mwanzo walikuwa wakilisakama lango la Ashanti lakini wachezaji wao
hawakuwa makini kwani kila walipokuwa wakipata nafasi walishindwa kuzitumia.
Dakika ya 32 Yanga
walipata bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wake Juma Ally, baada ya kupata
pasi ndefu kutoka kwa Bakari Ally, ambapo aliwachambua mabeki wa Ashanti na
kulenga mpira wavuni.
Pamoja na bao hilo kwa Yanga, Ashanti hawakukata tamaa na badala yake nao
walizidisha kasi dakika ya 42 mshambuliaji Haruna Rashid aliisawazishia timu
yake ya Ashanti
bao baada ya kupiga shuti kali lililomshinda kipa kudaka.
Mp a k a t imu h i z o
zinakwenda mapumziko zilifungana bao 1-1. Kipindi cha pili kilianza huku kila
timu ikishambulia, dakika ya 47 na 48, Ashanti walijikuta wakipoteza
nafasi za kufunga baada ya washambuliaji wao kupata nafasi nzuri za kufunga l a
k i n i wa k a s h i n dwa kuzitumia.
Dakika ya 75 Yanga
walipata bao la pili baada ya mshambuliaji wao Bakari Ally kufunga kwa shuti
kali baada ya kuwatoka mabeki wa Ashanti na kutumbukiza mpira
wavuni.
Mpaka
mpira unamalizika ni Yanga ambao walikuwa washindi na hivyo moja kwa moja
kutinga hatua ya nusu fainali
No comments:
Post a Comment